Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

SANCHO??? WA NINI? MCHUKUENI HARRY KANE




MKONGWE Steve McClaren amewaambia Manchester United kuweka mkazo kwenye kuwasajili mastraika Erling Haaland na Harry Kane kwa ajili ya manufaa ya timu na sio kuhangaika na saini ya Jadon Sancho
Man United kwa muda mrefu wameng’ang’ania kumfukuzia Sancho, huku klabu yake ya Borussia Dortmund mara kwa mara ikisema kwamba haina mpango wa kumuuza winga huyo.
Jumapili iliyopita, Man United ilichapwa 2-1 na Sevilla kwenye nusu fainali ya Europa League, huku safu yao ya ushambuliaji ikikosa nafasi nyingi kwenye kufunga mabao jambo linalomfanya McClaren, aliyewahi kuwa kocha msaidizi wa timu hiyo chini ya Sir Alex Ferguson kuwataka wasajili namba 9 badala ya winga kama Sancho.
“Wale wachezaji wanne pale mbele wapo haraka sana, wapo vizuri na wamekuwa wakisababisha matatizo mengi sana kwa mabeki wa timu pinzani. Hata Anthony Martial naye amekuwa na kiwango kizuri,” alisema McClaren.
“Lakini, kwenye mechi kubwa wanaonekana kuwa na tatizo hawaonekani kama ni wafungaji wa kweli. Wanahitaji wachezaji wa daraja la juu kwenye nafasi hiyo. Sidhani kama Lukaku angefiti kwenye kikosi cha Man United, hivyo wanahitaji mtu kama (Erling) Haaland. Atawafaa zaidi.
“Nimemtazama Jadon Sancho sana kwenye mechi za Dortmund na anavutia, lakini amewazidi kidogo sana Martial, Rashford na Greenwood, hivyo nashangaa kwanini wanamhitaji kwa nguvu zote hizo?
“Yeye si namba tisa, na Martial, Rashford na Greenwood nao si namba tisa. Lazima uwe na mnyama kwenye boksi, mfungaji na namba tisa wa ukweli.”
Kutokaa na hilo, Haaland ndiye mchezaji ambaye McClaren anataka asajiliwe Man United badala ya Sancho na kama ikishindikana basi wavamie Tottenham Hotspur kwenda kumsajili Kane.
 
MANCHESTER United imeripotiwa kupanga kuvamia kwenye kikosi cha Barcelona dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi kuwanasa Ousmane Dembele, Arturo Vidal, Ivan Rakitic na Samuel Umtiti.
Miamba hiyo ya La Liga imepanga kuondoa baadhi ya mastaa baada ya kukumbana na udhalilishaji mkubwa kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya walipochapwa 8-2 na Bayern Munich Ijumaa iliyopita. Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, wachezaji hao ni miongoni mwa wataofunguliwa mlango wa kutokea na kwa nyakati tofauti, Man United ilihusishwa na wachezaji wote na kikosi hicho cha kocha Ole Gunnar Solskjaer kinahitaji Barcelona tu washushe bei zao iende kunasa huduma zao fasta.
Kwenye dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi, chaguo la kwanza la Man United ni staa wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho - lakini kutokana na bei kubwa anayouzwa, miamba hiyo ya Old Trafford inapiga hesabu ya kunasa wabadala wake ambao itawapata kwa bei ndogo.
Dembele anatazamwa moja kwa moja kama mbadala wa Sancho na huduma yake itapatikana kwa gharama ya chini huku Barcelona wakiwa tayari kumuuza kutokana na rekodi yake ya kuwa majeruhi mara kwa mara.
Umtiti naye anaweza kupatikana, huku Rakitic aliambia Man United kwenye dirisha la Januari kwamba hana mpango wa kujiunga na timu hiyo, lakini kwa sasa kila kitu kinaweza kuwa tofauti.
Miamba mingine itakayochuana kusaka huduma za wakali hao ni Arsenal, Chelsea, Liverpool, Tottenham Hotspur na Manchester City ukiweka kando timu za nje ya Ligi Kuu England.
Sidhani kama chelsea inaweza enda barcelona kusajili player yyt barce player ambao wako sokoni wengi ni 30+ sisi huku kwetu tuna tunakazi ya kupunguza wazee hatuwezi ongeza
 
MANCHESTER United imeripotiwa kupanga kuvamia kwenye kikosi cha Barcelona dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi kuwanasa Ousmane Dembele, Arturo Vidal, Ivan Rakitic na Samuel Umtiti.
Miamba hiyo ya La Liga imepanga kuondoa baadhi ya mastaa baada ya kukumbana na udhalilishaji mkubwa kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya walipochapwa 8-2 na Bayern Munich Ijumaa iliyopita. Kwa mujibu wa Mundo Deportivo, wachezaji hao ni miongoni mwa wataofunguliwa mlango wa kutokea na kwa nyakati tofauti, Man United ilihusishwa na wachezaji wote na kikosi hicho cha kocha Ole Gunnar Solskjaer kinahitaji Barcelona tu washushe bei zao iende kunasa huduma zao fasta.
Kwenye dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi, chaguo la kwanza la Man United ni staa wa Borussia Dortmund, Jadon Sancho - lakini kutokana na bei kubwa anayouzwa, miamba hiyo ya Old Trafford inapiga hesabu ya kunasa wabadala wake ambao itawapata kwa bei ndogo.
Dembele anatazamwa moja kwa moja kama mbadala wa Sancho na huduma yake itapatikana kwa gharama ya chini huku Barcelona wakiwa tayari kumuuza kutokana na rekodi yake ya kuwa majeruhi mara kwa mara.
Umtiti naye anaweza kupatikana, huku Rakitic aliambia Man United kwenye dirisha la Januari kwamba hana mpango wa kujiunga na timu hiyo, lakini kwa sasa kila kitu kinaweza kuwa tofauti.
Miamba mingine itakayochuana kusaka huduma za wakali hao ni Arsenal, Chelsea, Liverpool, Tottenham Hotspur na Manchester City ukiweka kando timu za nje ya Ligi Kuu England.
Sidhani km hii taarifa ina ukweli
 
Mpira una maajabu na lolote lawezekana ila tukubakiane hii Kanuni haiwezi apply game ya leo Lyon v Bayern. Lyon hawezi pata matokeo aslani
 
Mpira una maajabu na lolote lawezekana ila tukubakiane hii Kanuni haiwezi apply game ya leo Lyon v Bayern. Lyon hawezi pata matokeo aslani
Mi Bayern inacheza kwa spidi na fiziki ya kutosha..Lyon kazi wanayo
 
Bayern alishachukua tahadhali zote kwa kuangalia mechi za juve na city ingawa kwa leo Lyon wamekosa umaliziaji mzuri tu maana mwanzoni wametengeneza nafasi 2-3 za wazi kabisa. Depay,toko ekambi na cornet
 
Tukimchukua Grealish tunapigwa tena, Aston Villa wata-take advantage ya kubaki Premier League kupiga pesa. Kuliko kumchukua Grealish kwa £80 ni bora tufufue dili la Brooks (Bournemouth) Umri mdogo (23) na pesa ndogo, hazidi £25 ukizingatia wameshuka daraja, ni bora kubet hapo kuliko kwa Grealish. Msimu wake wa kwanza akitokea Sheffield United ali-perform vizuri. Msimu huu majeruhi yaliathiri kiwango chake na hakucheza karibia msimu mzima ila bado aliporudi baada ya break ya Covid-19 ali-manage kupata goli moja. Ni Premier League proven. Kumpata huyu bado dili la Sancho linapaswa kushughulikiwa, tupate na CB na Striker, msimu tutauanza vizuri sana.
Likely to happen.....

David Brooks to Man. United. Tetesi zinasema Manchester United wapo mbioni kusaka saini ya Brooks kama mmbadala wa dili la Sancho.

Niliwahi kuandika kipindi cha nyuma tumpate Brooks ila naona United kama wanataka kumtumia kama cheap option ya Sancho. Kimsingi Sancho bado anahitajika hata Brooks akija.

NB: Siku Brooks akisaini na United nitatoa picha yake akiwa na uzi wa The Cherries na nitaweka akiwa na The Red Devils. 😂
 
CB: Magalhães (£18)
DM: Neves (£45) // Ndidi (£40)
RW: Sancho (£108)
ST: Mitrović (£18)

Magalhães, huyu ni kama Wan-Bissaka wa katikati. Akija United ataimarisha ukuta wetu vizuri sana.

Neves // Ndidi. Hawa ni aina ya wachezaji muhimu sana katika eneo la kati, ukizingatia Matić umri umeenda tukimpata mmoja wapo kati ya hao kiungo chetu kitakuwa imara sana.

Sancho. Tumeteseka miaka mingi sana kumpata mtu sahihi wa kucheza kama Right Winger, James kaja ila bado ana mengi ya kujifunza. United wanapaswa kuvunja kibubu. Sancho ni mtu sahihi tunapaswa kuitumia hii nafasi kujiimarisha.

Mitrović. Sio mchezaji ambaye yupo sokoni ila ni cheap option ya nafasi ya striker. Huyu jamaa sipatii picha akizungukwa na Rashford, Sancho, Pogba, Bruno. He's far better than Martial. Ni moja ya mmaliziaji mzuri sana.

Hawa wachezaji wote umri wao unaendana na sera za timu. Kwa umri wao wanakupa muda mzuri kuunda kikosi huku bado wakiwa katika umri mzuri kucheza soka.

NOTE: HIZI TRANSFER ZOTE HAZITAFANYIKA MSIMU HUU ILA HIVI NDIYO JINSI UNITED WANAPASWA KUINGIA SOKONI.
Understand Lille have agreed to sell Gabriel Magalhães to Arsenal for a fee of €30million.
Brazilian centre back due to take medical tomorrow before completing transfer to the Premier League club.
Gabriel was also targeted by Everton, Manchester United and Napoli. #AFC #BRA
IMG_20200820_013147.jpg
 
DIRECTOR OF FOOTBALL NI NANI? ANAFANYA NINI NDANI YA KLABU?

Na Tom Thomas

MICHAEL Zorc. Anatajwa kama 'director of football' bora zaidi duniani. Amekua akiifanya kazi hii kwa zaidi ya miaka 20 sasa akiwa Borussia Dortmund. Klabu yake ya maisha. Ndio. Borrusia Dortmund ni klabu ya maisha yake. Misimu 17. Mechi zaidi ya 500 kama mchezaji. Misimu 21 sasa kama 'director of football'.

Alianza kuitumikia Dortmund tangu akiwa na miaka 16, akastaafu mwaka 1998. Muda mfupi baada ya kuachana na soka, alianza majukumu mapya kama 'director of football' wa Dortmund. Amekua akiifanya kazi hii kwa mafanikio makubwa. Ndio maana amekua akitajwa kuwa bora.

Dortmund inasifika kwa kutengeneza wachezaji wengi mahiri na bora. Inasifika pia kwa kuwa na mfumo bora wa uongozi kuanzia kwa wachezaji, makocha hadi bodi ya klabu. Mfumo wa utendaji kazi ndani ya klabu upo chini ya Michael Zorc.

Wakati anacheza soka, alifahamika zaidi kwa jina la utani la 'Susi'. Jina lililotokana na staili yake ya kuachia nywele ndefu kichwani. Alishawahi kuwa nahodha wa Dortmund kwa kipindi kirefu. Anakumbukwa pia kwa uwezo wake mkubwa wa kufunga mabao kwa penati.

Mwanzoni mwa mwaka 2017 alihusishwa kujiunga na Arsenal. Ili aifanye kazi yake ya 'director of football'. Kwenye kipindi hiki, Arsenal haikuwa na mtu kwenye nafasi ya 'director of football'. Shughuli zote zinazoihusu klabu zilikua chini ya Sir Chips Keswick kama mwenyekiti wa klabu na Arsene Wenger kama kocha.

Mzee Arsene Wenger alishangazwa sana na habari hii. Aliiona ni habari isiyokua na ukweli. Tangu aanze kuifundisha Arsenal hakuwahi kuwa na mtu kwenye nafasi ya 'director of football'. Hakuamini na hakuwa akiifahamu kazi ya mtu wa aina hiyo ndani ya klabu.

"Director of football? Ni nani mtu huyu? Siijui kazi yake. Au ni mtu anayesimama na kuawaelekeza wachezaji huku ni kulia na huku ni kushoto?". Haya yalikua ni majibu yake baada ya kuulizwa kuhusu habari za Arsenal kutaka kumuajiri Michael Zorc.

Wenger aliendelea kusimama kwenye kile alichokiamini. Hakuwa anaiona kazi ya 'director of football' ndani ya klabu. Aliamini yeye ni kocha na maneja wa Arsenal. Ataamua mambo yote ndani ya uwanja. Yeye ndiye bosi wa Arsenal, maswala yote ya kiufundi yapo chini yake. Atahusika na mipango yote ya klabu.

Siku chache zilizopita Ed Woodward ambaye ni makamu-mtendaji wa Manchester United aliulizwa swali kuhusu uwezekano wa klabu yake kuajiri mtu akayefanya kazi kama 'director of football'.

Alijibu, "tutaendelea kufanya uwekezaji muhimu kwenye kikosi chetu cha kwanza, akademi yetu na kwenye kitengo chetu cha kusaka vipaji. Huu ni mpango wa muda mrefu wa kukijenga kikosi chetu na ni mpango sahihi".

Maneno yake yalimaanisha kwamba, Manchester United haina mpango wa kuongeza mtu mwingine kwenye nafasi ya uongozi wa klabu. Hii ina maana kwamba klabu haijaona umuhimu wa 'director of football' ndani ya klabu. Kwamba mfumo wa utendaji kazi ndani ya klabu ni 'sahihi'.

Sikushangazwa na kauli hii. England ni moja kati ya nchi barani Ulaya ambayo klabu zake zilichelewa sana kuajiri mtu kwenye nafasi ya 'director of football'. Nafasi na kazi yake ndani ya klabu ilikua haifamiki au imekua ikileta mgawanyiko mkubwa.

Swali la msingi la kujiuliza. 'Director of football' ni nani? Ana kazi gani ndani ya klabu? Ukimuuliza Michael Zorc swali hili, atabasamu kidogo kabla ya kulijibu. Hii ni kwa sababu amekua akiifanya kazi hii kwa miaka mingi. Anajua kila kitu kuihusu kazi hii. Huwa anatamani kazi yake ifahamike zaidi kwa watu wengi. Kama vile kazi ya kocha inavyofahamika.

Kwa miaka mingi, kocha amekua na majukumu ya kuhakikisha anakisimamia kikosi cha kwanza, akademi na vikosi vya vijana kama bosi. Anafundisha falsafa zake ambazo anaamini ni bora kwenye kupata ushindi. Anakua na kazi ya kusimamia uhamisho wa wachezaji. Kuuza na kununua.

Anasimamia vitengo vyote ndani ya klabu. Kuanzia kile cha kutafuta wachezaji vijana hadi kitengo cha madaktari. Kocha anakua na kazi ya kutengeneza na kusimamia mipango ya muda mrefu ya klabu. Ndio maana kocha hakutambulika kama kocha pekee. Alitambulika kama meneja wa klabu. Alikua na majukumu mengi.

Kocha si mtu aliye na uhakika wa kudumu kwenye nafasi yake kwa muda mrefu. Ikaonekana kwamba, si busara kocha kupewa majukumu yote makubwa ndani ya klabu. Ni vyema kuwe na mtu mwingine atakayehakikisha anaisimamia mipango ya klabu. Halafu kocha awe na jukumu la kusimamia na kuifundisha timu.

Hapo ndipo nafasi ya 'director of football' ilipoanzishwa na klabu mbalimbali kuanza kuajiri watu kwenye nafasi hii. Kazi yake ndani ya klabu ikawa ni kusimamia vitengo vyote ndani ya klabu.

Kusimamia upatikanaji wa wachezaji vijana, wachezaji wa kikosi cha kwanza na kusimamia upatikanaji wa kocha mpya. Yaani 'director of football' ndiye anayetafuta na kupendekeza jina la kocha mpya kama yule wa zamani ataondoka.

Anakua na kazi ya kuanzisha na kusimamia falsafa ya klabu. Falsafa ya klabu inajumuisha mambo mengi ikiwemo namna timu inavyocheza. Falsafa hii hufundishwa zaidi kwenye akademi na vikosi vya vijana.

Huku kwenye kikosi cha kwanza kocha anakua na uhuru wa kufundisha soka lake ingawa ni vyema kama kocha huyu ataindeleza falsafa na tamaduni ya klabu. Ndio maana jukumu la kutafuta kocha linakua chini ya 'director of football'. Yaani kocha atakayeajiriwa ni yule aliyeaminika mbele ya 'director of football' kuendeleza falsafa ya klabu.

'director of football' anakua na kazi ya kuhakikisha wachezaji waliopendekezwa na kocha wanapatikana. Yaani 'ana-negotuate' bei na gharama ya usajili na kusimamia mikataba yao. Hapa anakua na kazi ya kujadiliana na kocha kwanza kabla ya kumsajili mchezaji aliyependekezwa.

Ndio maana kazi hii inahitaji mtu ambaye alishawahi kucheza soka zamani. Huyu ni mtu anayefahamu zaidi jinsi soka lilivyo. Anafahamu mchezaji gani atakua muhimu na ataleta faida ndani ya klabu kulingana na falsafa ya klabu ilivyo.

'director of football' anasimama kama daraja kati ya kocha na bodi ya klabu. Mabosi, wakurugenzi na wamiliki wa klabu. Mapendekezo yote ya klabu kutoka kwa kocha yanapitia kwake kwanza kabla ya kufika kwa viongozi wa juu wa klabu.

Anakua na kazi ya kusimamia shughuli zote za klabu zinazokihusu kikosi. Wakati mwingine analazimika kuhudhuria mazoezi kila 'session' na kuhudhuria mechi zote za klabu. Kwa kufanya hivi, atatambua makosa na mapungufu ya kikosi kwa undani zaidi.

Cheo cha 'director of football' wakati mwingine hujulikana kwa majina tofauti. Anaweza kuitwa 'sporting director' au 'technical director'. Hapa huleta mgawanyiko na kuwafanya wengi wasielewe. Hii ni kwa sababu majukumu hubadilika na kuwa tofauti kati ya klabu na klabu au nchi na nchi.

Mfano, muda mfupi kabla ya Arsenal na Arsene Wenger kutengana, kulikua na mabadiliko makubwa ya kiungozi ndani ya klabu. Aliajiriwa Bwana Raúl Sanllehí kuwa 'director of football'. Arsenal waliona Sanllehí pekee hatoshi. Wakamuajili Edu kuwa 'technical director'.

Kimsingi 'director of football' hufanya kazi za 'technical director' ingawa kuna utofauti wa majukumu kati yao. 'Technical director' ana kazi ya kusimamia na 'ku-organise' shughuli zote za kikosi cha kwanza na akademi ya klabu. Ana kazi ya kutafuta wachezaji watakaendana na falsafa ya klabu. Majukumu yake ni machache ukilinganisha na yale ya 'director of football'.

Mwishoni mwa mwaka 2016, kwa mara ya kwanza Liverpool walimuajiri bwana'mdogo Michael Edwards. Huyu aliajiriwa kama 'sporting director' yaani kama 'director of football' ingawa majukumu yake ni tofauti na ya 'ma-football director' wengine.

Damien Comolli alishawahi kuwa na 'director of football' ingawa majukumu yake si sawa na haya anayoyafanya Michael Edwards. Agosti 2015, Comolli alibadilishiwa majukumu na kuwa 'technical director'. Uwepo wake ndani ya klabu ulikua unamchanganya sana kocha Brendan Rodgers.

Rodgers alishawahi kusema "kwangu mimi nilifikiri naenda kufanya kazi na kundi la watu kwa pamoja, sikudhani kama naenda kufanya kazi na 'director of football'. Mimi naamini kwamba, kocha ndiye 'technical director' kwenye kikosi". Hivi sasa Rodgers amebadilika. Akiwa Leicester City anafanya kazi pamoja na Jon Rudkin ambaye ni 'director of football'.

Pale Merseyside, kazi ya Michael Edwards ni kuisimamia Liverpool kwenye maswala ya kifedha, mauzo na maendeleo ya klabu kwa ujumla. Majukumu ya ufundi na majukumu mengine ya kikosi na wachezaji yanabaki kuwa chini ya watu wengine.

Chelsea wao baada ya kuachana na Michael Emenalo ambaye alikua kama 'technical director' aliajiriwa mwanamama Marina Granovskaia ambaye anafanya kazi kama 'director' wa klabu. Inasemekana hana uelewa mzuri kuhusiana na mambo ya kiufundi 'technical' kama alivyokua Emelano.

Mhipaniola Txiki Begiristain anafanya kazi kama 'director of football' pale Manchester City. Huyu ni mtu bora sana kwenye kazi hii. Alishawahi kuifanya kazi hii akiwa Barcelona. Ni mbobezi kwenye kazi hii. Yeye ndiye aliyesimamia usajili wa Pep Guardiola na wachezaji wengi pale City.

Manchester United wao bado hawaelewi kama kuna umuhimu wa kuajiri 'director of football', 'technical director' au 'sporting director'. Kama alivyosema Ed Woodward siku chache zilizopita, bado wanaona mfumo wao wa uongozi ni 'sahihi'. Hawana shida na mtu wa aina hiyo...

Madaraka Ya Kulevya......Ed!!!!!!!
 
Back
Top Bottom