Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kuna andazi moja limezunguka nyuzi za watu kusema "Njooni muone pressing za hatari" sijui limejificha wapi.

Anyway, Man U ili kufika hapo ilipita kwa penati. Gemu imeanza bwana Bruno Penalties akapata penati goli la Sevilla unaona kabisa move ya goli inatengenezwa na watu wanascore.

Yaani kwa kifupi. Man U na Simba zikija kwenye swala la kucheza na Sevilla Simba ni bora kuliko man u.
 
★Hata hamu ya kulala sina hamu ya kuchat sina hamu ya kuwazia mechi iloisha ndio sina kabisa Hapa mapigo ya Moyo yanaenda hovyo hovyo tu ningekuwa mlevi ningekunywa hata barafu ya konyagi nazani ingemaliza haya machungu Usiku Mwema
 
Hakuna mchezaji aliye cheza vibaya, timu imejituma mwanzo mwisho ila Sevilla wanabahati kwa Man u, Sevila wametengeneza nafasi chache sana, man u wametengeneza nafasi nyingi ila mpira uligoma kuingia wavuni.
Mbinu za kocha zilikua sahihi timu imeshambulia sana ikabaki mpira kuingia wavuni lakini haikua siku ya Man u. Kuna siku kwenye soka inakua ivyo.
Acha kujifariji mkuu. Hakuna bahati kwenye soka . Ukishindwa kutumia nafasi unazopata lazima utaadhibiwa tu

Umesema kabisa hapo kuwa timu imetengeza nafasi nyingi ila mpira uligoma kuingia wavuni , maana yake ni kuwa Man u weren't clinical. Sevilla wao 5 shots 3 on target 2 goals. They took their chances .

Man Hakuna natural number 9 pale mtu ambae ni muuaji type ya Aguero, Lewandowski Cavani .,martial sio NATURAL number 9

Katika game hizi 2 copenhagen na sevilla Man wamepiga zaidi ya shots 30 lakini magoli mawili yaliyopatikana ni kwa njia ya penat . Nafasi zinatengenezwa kweli ila umaliziaji hafifu

Enewei body language ya wachezaji wenyewe ilikua inaonesha kuwa nafasi ya 3 inawatosha na msimu ujao watacheza UCL hivo waliona hawana presha sana
 
CB: Magalhães (£18)
DM: Neves (£45) // Ndidi (£40)
RW: Sancho (£108)
ST: Mitrović (£18)

Magalhães, huyu ni kama Wan-Bissaka wa katikati. Akija United ataimarisha ukuta wetu vizuri sana.

Neves // Ndidi. Hawa ni aina ya wachezaji muhimu sana katika eneo la kati, ukizingatia Matić umri umeenda tukimpata mmoja wapo kati ya hao kiungo chetu kitakuwa imara sana.

Sancho. Tumeteseka miaka mingi sana kumpata mtu sahihi wa kucheza kama Right Winger, James kaja ila bado ana mengi ya kujifunza. United wanapaswa kuvunja kibubu. Sancho ni mtu sahihi tunapaswa kuitumia hii nafasi kujiimarisha.

Mitrović. Sio mchezaji ambaye yupo sokoni ila ni cheap option ya nafasi ya striker. Huyu jamaa sipatii picha akizungukwa na Rashford, Sancho, Pogba, Bruno. He's far better than Martial. Ni moja ya mmaliziaji mzuri sana.

Hawa wachezaji wote umri wao unaendana na sera za timu. Kwa umri wao wanakupa muda mzuri kuunda kikosi huku bado wakiwa katika umri mzuri kucheza soka.

NOTE: HIZI TRANSFER ZOTE HAZITAFANYIKA MSIMU HUU ILA HIVI NDIYO JINSI UNITED WANAPASWA KUINGIA SOKONI.
 
Timu ikifungwa mashabiki wana haki ya kukosoa na kulaumu na ata kocha ujiteteee vipi unaonekana unamapungufu. Hii timu ya Man u kwaleo imepoteza ila haikucheza vibaya.
Kule timu ilipokua mwanzo kwa sasa imepiga hatua kubwasana tatizo mashabiki wanataka makombe kwakua man u ni timu ya makombe. Hii timu kama haito vurugwa inaitaji misimu miwili irudi pale ilipokua na Fugerson na ina nafasi ya kutamba kwa misimu zaidi ya kumi. Uyu kocha ni sahihi kwa ii timu. Tuvute subra.
Wewe hauko serious, kutoka kuchukua Europa na kuwa wapili kwenye ligi afu unasema mpo vizuri kwa kutolewa nusu fainali tena usajili kabambe ukiwa umeshafanyika? Au sijaelewa vizuri mpo vizuri katika lipi?!
 
Hata hapo Ole alipofika ni wa kupewa pongezi, record yake kubwa katika soka ni kushusha timu daraja.
Bruno pasi zote anazotoa hazifanyiwi kazi yaani kiukweli striking force inamuungasha. Ole hatakiwi kulaumiwa maana walioshindwa kutumia nafasi walikuwa uwanjani ,, huku kwenye sub hakuna fighter yoyote ambaye angeleta mabadiliko. Ndio maana pale front 3 mbele hakuna mwenye mpinzani hadi kocha anajiuliza aweke nani.
 
Man Utd kwa sasa wana kikosi bora kabisa, tatizo ni mwalimu na mbinu zake za uchezaji. Man Utd iliyokuwa inafungwa na Sevila ni ile mbovu iliyokuwa imejaa wazee walioflop, kwa uwekezaji uliofanyika haya ni matokeo mabovu.
Ole hata sub hawezi mi nilisema hii timu huwa inashinda kwa mizuka tu ya wachezaji siku wakifurahi wanaupiga siku wakivurugwa ndo kama hivi.
Mi sijui tunacheza mpira wa aina gani kwakweli Ole hawezi kuipa hii timu hata kombe la carling hana huo uwezo ni hovyoo kabisa wahedii.
Tusubiri EPL sasa na mambo yatakua kama haya tu sioni mapya hata kidogo yanayokuja acha nilale nimestream sijui GB ngapi zimekata.
 
Dah
1597632459761.jpg
 
Back
Top Bottom