Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Liverpool hawana hela labda ajigharimie mwenyewe jambo lisilowezekana
Screenshot_2020-07-29_224014.jpg
 
Mawazo ya Arsene Wenger haya eti unatoa £100mil kumnunua Neymar wkt kina Neymar wapo wengi matokeo yake tm ikawa ya kawaida zama zote za uongozi wake mpk leo, mkuu unapotaka kutengeneza tm wachana na mawazo km hayo man u ni tm kubwa usitegemee kupata mchezaji kwa pesa ndogo hata huyo Bruno unayesema kanunuliwa kwa pesa mbuzi lkn ukiingia deep mpunga wake utakimbia.
Acha kupotosha umma wewe, labda kama umesimuliwa hizi habari, unasemaje Wenger timu yake ilikuwa ya kawaida zama zote za uongozi wake???
Kipindi cha Wenger timu imechukua EPL kadhaa na kufika final UCL ikiwemo kuchukua ubingwa wa ligi bila kupoteza mchezo alafu wewe simple tu unakuja kutema hili shudu...
 
Acha kupotosha umma wewe, labda kama umesimuliwa hizi habari, unasemaje Wenger timu yake ilikuwa ya kawaida zama zote za uongozi wake???
Kipindi cha Wenger timu imechukua EPL kadhaa na kufika final UCL ikiwemo kuchukua ubingwa wa ligi bila kupoteza mchezo alafu wewe simple tu unakuja kutema hili shudu...
Ukifuatilia vzr historia ya Wenger na Arsenal yake utagundua kwamba wachezaji wengi waliompa mafanikio yale hakuwasajiri yeye ila baada ya wale aliowakuta kutundika daluga naye habari yake ikawa imeisha.
 
Acha kupotosha umma wewe, labda kama umesimuliwa hizi habari, unasemaje Wenger timu yake ilikuwa ya kawaida zama zote za uongozi wake???
Kipindi cha Wenger timu imechukua EPL kadhaa na kufika final UCL ikiwemo kuchukua ubingwa wa ligi bila kupoteza mchezo alafu wewe simple tu unakuja kutema hili shudu...
To be precise 22 years at Arsenal and 3 epl titles! What about Mourinho at Chelsea? Guardiola at Man city?
 
Kila baada ya dakika 62, Sancho anakupa goli au assist

Kwa msimu huu, kwa Ulaya, kwenye ligi kubwa ndiye namba 2 kwa assists akiwa na assists 15 baada ya De Bruyne na Muller wenye assists 16 (japo magoli kawaacha mbali)

Kwa Ulaya kwenye ligi kubwa ni kati ya wachezaji wenye magoli mengi ya ligi, magoli mengi, yaani magoli 14

Ukitaka kulinganisha na vijana wetu pale OT

Rashford anakupa goli au assist kila baada ya dakika 104, Martial anakupa goli au assist kila baada ya dakika 134 na Greenwood anakupa goli au assists kila baada ya dakika 129. Ooh... , nilitaka kumsahau DJ, yeye anakupa goli au assist kila baada ya dakika 241.

Kwa misimu kadhaa sasa, timu bingwa EPL imekuwa ikilazimika kufunga magoli zaidi ya 80 ili iwe bingwa. Ukiwa na Sancho na wachezaji wetu tulionao unaweza kuwa na matumaini ya kufikisha hizo goli kupitia magoli na assists zake. Je mwakani tunataka kufukuzia ubingwa au tunataka kufukuzia nafasi ya 3 au ya 4 mpaka siku ya mwisho ya ligi?

Sancho pia yupo mbele ya wachezaji wetu kwenye dribbling na passes success rate. Kwenye ku track back amezidiwa na wote ila kamzidi Martial

Wakati msimu uliopita Sancho alikuwa ana wastani wa magoli au assist kila baada ya dakika 94, unaona ana consistent na anazidi kupanda kiwango, na labda baadhi yetu tunasahau kwamba ndio kwanza ametimiza miaka 20 mwezi March, hii inaonesha ana nafasi ya kujifunza na kuongezeka kiwango kadiri miaka inavyoenda.

Katika msimu uliopita Salah alikuwa ana wastani wa goli au assist kila baada ya dakika 108, Mane kila baada ya dakika 134 na Firminho kila baada ya dakika 145. Na msimu huo tuliwaona jamaa ni wa moto hatari.

Hapa najaribu kumuweka Sancho kwenye uzani ili tujue tunamfukuzia mchezaji wa aina gani. Kama Neymar alinunuliwa kwa £200, tunashangaa vipi Sancho kuuzwa £80+. Je Neymar ni mchezaji mwenye uwezo mara mbili ya Sancho? HAPANA.

Sipigi debe United tupigwe bei kubwa kwa Sancho, ila kwa kuwa kuna watu wanamchukulia poa Sancho, nimeona niseme neno.

Pepe amenunuliwa na Arsenal £70+, msimu uliopita Cristal Palace walitaka kwa Zaha £80M kutoka kwa Arsenal. Soko lilishachafuka tangu tulipomnunua Pogba kwa £89M, soko lilishachafuka tangu Neymar aliponunuliwa na PSG kwa £200M, likiendelea kuchafuka kwa Jadon Sancho I will not care so much.

Nimejaribu kumfananisha Jadon Sancho na wachezaji wetu ili kuona kuwa analeta kitu kikubwa endapo tutamsajili. Lakini kwa mchango wake wa mwaka huu unaweza ona amewazidi wachezaji wengi wakubwa ulimwenguni.

Hapa tunaweza kupata picha kwanini United wanamtaka Sancho kwa udi na uvumba
Basi natoa agizo,,
vijana watumwe wamlete huyo Sancho mara moja[color/]
 
Ukifuatilia vzr historia ya Wenger na Arsenal yake utagundua kwamba wachezaji wengi waliompa mafanikio yale hakuwasajiri yeye ila baada ya wale aliowakuta kutundika daluga naye habari yake ikawa imeisha.
Acha uwongo mzee, hivi unajua hata Arsene Wenger ameanza kuifundisha lini Arsenal???
Hebu taja hao wachezaji unaosema waliompa mafanikio na hakuwasajili yeye,
Kwanza ulisema katika maisha yake yote ya soka hapo Arsenal hakuwahi pata mafanikio, sasa hivi umekuja na lingine kuwa kapata ila wachezaji hakusajili yeyehaya wataje.....


Msiwe mnasikiliza stori za vijiweni jamani.
 
To be precise 22 years at Arsenal and 3 epl titles! What about Mourinho at Chelsea? Guardiola at Man city?
Hapo unaongelea comparison, na hoja sio hoja sio hiyo,
Hoja ni mafanikio,
Au na wewe unataka kusema kuwa ni kweli Wenger hajawahi pata mafanikio katika maisha yake ya soka?
Utajidhalilisha mkuu.
Je, Pep hapo city mpaka sasa ana mafanikio gani?
Mourinho akiwa Chelsea ana mafanikio gani?

Kumzidi Prof????!
 
Hapo unaongelea comparison, na hoja sio hoja sio hiyo,
Hoja ni mafanikio,
Au na wewe unataka kusema kuwa ni kweli Wenger hajawahi pata mafanikio katika maisha yake ya soka?
Utajidhalilisha mkuu.
Je, Pep hapo city mpaka sasa ana mafanikio gani?
Mourinho akiwa Chelsea ana mafanikio gani?

Kumzidi Prof????!
Miaka 22 vikombe vitatu ni kitu cha ajabu? Unaniuliza Mourinho Chelsea amepata nini? Angalia kakaa muda gani na ameshinda epl ngapi? Angalia Pep amekaa city muda gani ameshinda epl ngapi?
Miaka 22 kwenye epl na kushinda vikombe vitatu sio mafanikio,at least by my standards.
 
Acha uwongo mzee, hivi unajua hata Arsene Wenger ameanza kuifundisha lini Arsenal???
Hebu taja hao wachezaji unaosema waliompa mafanikio na hakuwasajili yeye,
Kwanza ulisema katika maisha yake yote ya soka hapo Arsenal hakuwahi pata mafanikio, sasa hivi umekuja na lingine kuwa kapata ila wachezaji hakusajili yeyehaya wataje.....


Msiwe mnasikiliza stori za vijiweni jamani.
Arsene Wenger amekuja Arsenal mwaka 1996 alikikuta kikosi cha kina Tonny Adams, David Seaman, Wintuburn, Ian Wright kikiwa fire, na ndicho kikosi hicho hicho kilichochukua ubingwa mwaka 1998 na baadaye wachache wakastaafu lkn asilimia kubwa walibaki na ndiyo wakachukua tena epl mwaka 2002, kikosi pekee ambacho Wenger at least atajisifia kwa asilimia kubwa alikijenga yeye (na sio chote) ni kikosi cha 2004 ambacho ndicho kikosi cha mwisho kuchukua epl ni kile cha Thierry Henry.

Ss Wenger amekaa Arsenal miaka 22 kikombe kikubwa anachojivunia ni epl, no ucl, no europa hv apo utasema ana mafanikio kweli? Na baada ya wale wachezaji alowakuta kustaafu wote hapo ikamuwia vigumu kuendeleza consistence na huo ndio ukweli japo unauma but statistics don't lie.
 
Back
Top Bottom