Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kumekucha
IMG-20200729-WA0019.jpg
 
Hajanifanya chochote mkuu.

Ila sioni mantiki ya kutoa hela nyingi kwa mchezaji below average kama hela tuliotoa kwa kumnunua Maguire.

Scouts wa Man Utd wanaweza kuleta mchezaji mzuri zaidi yake kwa gharama ndogo kabisa. Vilevile kwa Sancho, unatoa £100M kwa lipi la maana pale? Kisa tunashida ya winger?
Hela ya Grealish unampata Partey na VDB na chenji inabaki.
Mawazo ya Arsene Wenger haya eti unatoa £100mil kumnunua Neymar wkt kina Neymar wapo wengi matokeo yake tm ikawa ya kawaida zama zote za uongozi wake mpk leo, mkuu unapotaka kutengeneza tm wachana na mawazo km hayo man u ni tm kubwa usitegemee kupata mchezaji kwa pesa ndogo hata huyo Bruno unayesema kanunuliwa kwa pesa mbuzi lkn ukiingia deep mpunga wake utakimbia.
 
Mawazo ya Arsene Wenger haya eti unatoa £100mil kumnunua Neymar wkt kina Neymar wapo wengi matokeo yake tm ikawa ya kawaida zama zote za uongozi wake mpk leo, mkuu unapotaka kutengeneza tm wachana na mawazo km hayo man u ni tm kubwa usitegemee kupata mchezaji kwa pesa ndogo hata huyo Bruno unayesema kanunuliwa kwa pesa mbuzi lkn ukiingia deep mpunga wake utakimbia.
Wachezaji kama kina Neymar hawaji kila mara.

Pia suala ni bei na unachokipata kwa mchezaji husika. Bruno angekuwa muingereza angeuzwa kwa £200M.

Naunga mkono kuwanunua hata kwa £300M ila sio Grealish.
 
Kuna rumours kwamba UTD wanamtaka JAMES RODRIGUEZ wa madrid na wanajiandaa kuweka dau la £25MILL

MY TAKE; aje tu ila gharama isizidi £30mill maana tunahitaji squad depth.
Wa nini tena huyu?
Huyu si kaflop?

Kwa yaliyotokea kwa Sanchez, united hawawez kumchukua. Labda mkopo .

Rumors nyingine za ajabu, wanachofanya nikuchukua jina la mchezaji. Then wanamhusisha na Man U.
 
Kila baada ya dakika 62, Sancho anakupa goli au assist

Kwa msimu huu, kwa Ulaya, kwenye ligi kubwa ndiye namba 2 kwa assists akiwa na assists 15 baada ya De Bruyne na Muller wenye assists 16 (japo magoli kawaacha mbali)

Kwa Ulaya kwenye ligi kubwa ni kati ya wachezaji wenye magoli mengi ya ligi, magoli mengi, yaani magoli 14

Ukitaka kulinganisha na vijana wetu pale OT

Rashford anakupa goli au assist kila baada ya dakika 104, Martial anakupa goli au assist kila baada ya dakika 134 na Greenwood anakupa goli au assists kila baada ya dakika 129. Ooh... , nilitaka kumsahau DJ, yeye anakupa goli au assist kila baada ya dakika 241.

Kwa misimu kadhaa sasa, timu bingwa EPL imekuwa ikilazimika kufunga magoli zaidi ya 80 ili iwe bingwa. Ukiwa na Sancho na wachezaji wetu tulionao unaweza kuwa na matumaini ya kufikisha hizo goli kupitia magoli na assists zake. Je mwakani tunataka kufukuzia ubingwa au tunataka kufukuzia nafasi ya 3 au ya 4 mpaka siku ya mwisho ya ligi?

Sancho pia yupo mbele ya wachezaji wetu kwenye dribbling na passes success rate. Kwenye ku track back amezidiwa na wote ila kamzidi Martial

Wakati msimu uliopita Sancho alikuwa ana wastani wa magoli au assist kila baada ya dakika 94, unaona ana consistent na anazidi kupanda kiwango, na labda baadhi yetu tunasahau kwamba ndio kwanza ametimiza miaka 20 mwezi March, hii inaonesha ana nafasi ya kujifunza na kuongezeka kiwango kadiri miaka inavyoenda.

Katika msimu uliopita Salah alikuwa ana wastani wa goli au assist kila baada ya dakika 108, Mane kila baada ya dakika 134 na Firminho kila baada ya dakika 145. Na msimu huo tuliwaona jamaa ni wa moto hatari.

Hapa najaribu kumuweka Sancho kwenye uzani ili tujue tunamfukuzia mchezaji wa aina gani. Kama Neymar alinunuliwa kwa £200, tunashangaa vipi Sancho kuuzwa £80+. Je Neymar ni mchezaji mwenye uwezo mara mbili ya Sancho? HAPANA.

Sipigi debe United tupigwe bei kubwa kwa Sancho, ila kwa kuwa kuna watu wanamchukulia poa Sancho, nimeona niseme neno.

Pepe amenunuliwa na Arsenal £70+, msimu uliopita Cristal Palace walitaka kwa Zaha £80M kutoka kwa Arsenal. Soko lilishachafuka tangu tulipomnunua Pogba kwa £89M, soko lilishachafuka tangu Neymar aliponunuliwa na PSG kwa £200M, likiendelea kuchafuka kwa Jadon Sancho I will not care so much.

Nimejaribu kumfananisha Jadon Sancho na wachezaji wetu ili kuona kuwa analeta kitu kikubwa endapo tutamsajili. Lakini kwa mchango wake wa mwaka huu unaweza ona amewazidi wachezaji wengi wakubwa ulimwenguni.

Hapa tunaweza kupata picha kwanini United wanamtaka Sancho kwa udi na uvumba
 
Bruno na CR7 tumewapata kwa right price na Sporting Lisbon ni timu kubwa Ureno. Aston Villa inapambana kushuka daraja EPL.

Grealish ana nini cha zaida cha kununuliwa kwa £80M? Au uuziwe Sancho kwa £130M kwa lipi??
Hakuna timu italipa £80 kumnunua Grealish, huyo akiuzwa ni chini ya hapo, au nusu ya hiyo bei(£40)
Tena Man u hawawezi kulipa hiyo hela, kwa kuwa anakuja kuanzia benchi..

Man U walilipa hela ndefu kwa Maguire na AWB, kwa sababu waliwahitaji kama first eleven.

Kuhusu Sancho hiyo bei uliyoitaja ni kubwa mno.
Huyu anaweza kununuliwa around bei aliyonunuliwa Pogba.
 
Man U wameiona kama vile ni sehemu ya kutajirisha club zao,,, Yaani Grealish mwanzoni thamani yake ilikuwa ni 59M Euro , sasa baada ya kuona kuwa dau la Sancho ni zaidi ya 100M Euro na wenyewe wakaamu kupandisha dau. Jamani kwani hakuna mbadala wa Mchezaji mwingine kuliko kutoa 80M Euro kwa Grealish?

Haya mambo ya kuuza mchezaji kwa bei kubwa sana ndio matokeo yake wanaenda kucheza kwa pressure kubwa sana, hivyo kucheza chini ya viwango,,,,, Labda kama watakuwa na roho ngumu kama ya Bruno Fernandes.
 
Sidhani kama United atatoa zaidi ya £60M endapo itaamua kumnunua Grealish

Kinachompandisha thamani zaidi ni Uingereza wake na kubaki ligi kuu, wangeshuka daraja ilikuwa inasemekana Aston Villa walikuwa tayari kumuuza hata kwa £45M

Grealish akija United hana uhakika wa namba hivyo ni ngumu United kulipa kupindukia.

Bei ya Grealish inaweza kushuka endapo Grealish atatia msukumo ili auzwe.

Kuna mbadala wa Grealish unaotajwa, Van De Beek

Kwa sasa kipaumbele cha United ni Sancho

Man U wameiona kama vile ni sehemu ya kutajirisha club zao,,, Yaani Grealish mwanzoni thamani yake ilikuwa ni 59M Euro , sasa baada ya kuona kuwa dau la Sancho ni zaidi ya 100M Euro na wenyewe wakaamu kupandisha dau. Jamani kwani hakuna mbadala wa Mchezaji mwingine kuliko kutoa 80M Euro kwa Grealish?

Haya mambo ya kuuza mchezaji kwa bei kubwa sana ndio matokeo yake wanaenda kucheza kwa pressure kubwa sana, hivyo kucheza chini ya viwango,,,,, Labda kama watakuwa na roho ngumu kama ya Bruno Fernandes.
 
★Ila dau alilosajiriwa nalo Ole Gunnar Solskijær walimkatili jamani £1.5M ★
IMG_20200729_192222_204.jpeg
 
Whoscored :

David de Gea finished the 2019/20 Premier League campaign with the second best save success rate of goalkeepers with 25+ appearances (73.3%)

First was.... Dean Henderson (75.2%)

manutd |
IMG_20200729_193508_230.jpeg
 
Back
Top Bottom