Kila baada ya dakika 62, Sancho anakupa goli au assist
Kwa msimu huu, kwa Ulaya, kwenye ligi kubwa ndiye namba 2 kwa assists akiwa na assists 15 baada ya De Bruyne na Muller wenye assists 16 (japo magoli kawaacha mbali)
Kwa Ulaya kwenye ligi kubwa ni kati ya wachezaji wenye magoli mengi ya ligi, magoli mengi, yaani magoli 14
Ukitaka kulinganisha na vijana wetu pale OT
Rashford anakupa goli au assist kila baada ya dakika 104, Martial anakupa goli au assist kila baada ya dakika 134 na Greenwood anakupa goli au assists kila baada ya dakika 129. Ooh... , nilitaka kumsahau DJ, yeye anakupa goli au assist kila baada ya dakika 241.
Kwa misimu kadhaa sasa, timu bingwa EPL imekuwa ikilazimika kufunga magoli zaidi ya 80 ili iwe bingwa. Ukiwa na Sancho na wachezaji wetu tulionao unaweza kuwa na matumaini ya kufikisha hizo goli kupitia magoli na assists zake. Je mwakani tunataka kufukuzia ubingwa au tunataka kufukuzia nafasi ya 3 au ya 4 mpaka siku ya mwisho ya ligi?
Sancho pia yupo mbele ya wachezaji wetu kwenye dribbling na passes success rate. Kwenye ku track back amezidiwa na wote ila kamzidi Martial

Wakati msimu uliopita Sancho alikuwa ana wastani wa magoli au assist kila baada ya dakika 94, unaona ana consistent na anazidi kupanda kiwango, na labda baadhi yetu tunasahau kwamba ndio kwanza ametimiza miaka 20 mwezi March, hii inaonesha ana nafasi ya kujifunza na kuongezeka kiwango kadiri miaka inavyoenda.
Katika msimu uliopita Salah alikuwa ana wastani wa goli au assist kila baada ya dakika 108, Mane kila baada ya dakika 134 na Firminho kila baada ya dakika 145. Na msimu huo tuliwaona jamaa ni wa moto hatari.
Hapa najaribu kumuweka Sancho kwenye uzani ili tujue tunamfukuzia mchezaji wa aina gani. Kama Neymar alinunuliwa kwa £200, tunashangaa vipi Sancho kuuzwa £80+. Je Neymar ni mchezaji mwenye uwezo mara mbili ya Sancho? HAPANA.
Sipigi debe United tupigwe bei kubwa kwa Sancho, ila kwa kuwa kuna watu wanamchukulia poa Sancho, nimeona niseme neno.
Pepe amenunuliwa na Arsenal £70+, msimu uliopita Cristal Palace walitaka kwa Zaha £80M kutoka kwa Arsenal. Soko lilishachafuka tangu tulipomnunua Pogba kwa £89M, soko lilishachafuka tangu Neymar aliponunuliwa na PSG kwa £200M, likiendelea kuchafuka kwa Jadon Sancho I will not care so much.
Nimejaribu kumfananisha Jadon Sancho na wachezaji wetu ili kuona kuwa analeta kitu kikubwa endapo tutamsajili. Lakini kwa mchango wake wa mwaka huu unaweza ona amewazidi wachezaji wengi wakubwa ulimwenguni.
Hapa tunaweza kupata picha kwanini United wanamtaka Sancho kwa udi na uvumba