Darmian
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 17,299
- 46,753
Yaani Rashford aliniboa sana jana..Atleast basi ufanye vitu basic kama hujapick form yako..yeye ndo kwanza anaharibu mambo,kila saa anapoteza mpira.Timu nzima iko exhausted sana hivyo expect kabisa hali kama hii tuliyonayo.
Kucheza back to back mfululizo kunachosa sana wachezaji halafu kibaya zaidi wachezaji wengi wamerudi kutoka lockdown wakiwa off form sana.
Fred na Scot wamerejea lakini wakiwa hawako form kama tulivyowazoea pamoja na Rashford hayuko sawa sawa sana.
Defence yetu namuona Lindelog tu ndiyo ana afadhali japo wengi tunamlalamikia humu bila kujua kuwa tatizo liko wapi.
Kuhusu AWB toka amerudi kutoka Lockdown naona Solkjaer hali ya kwenda kushambulia imecompromise sana uwezo wake defensively anapanda mbele sana au au analazimika kuingia ndani pale Lindelof au Maguire wanapopanda kufanya build up hivyo eneo lake kuonekana free space.
Brandon William's kwa mechi hizi mbili pamoja na makosa mengine amejitahidi sana kuziba pengo la Luke Shaw mechi zote tatu tulizocheza kuanzia Southampton Midfield na Front three zetu zilikuwa zinapoteza sana mipira kwahiyo defence ilikuwa kwenye wakati wa tahadhari muda wote kufukia makosa ya mara kwa mara ya kina Pogba na Rashford.
Imagine mechi ya jana Rashford hakuvuka mstari kuja kusaidia defence na kila mpira alipata aliupoteza kizembe na hakufanya juhudi za kutafuta hali kama hii lazima ingetusumbua sana.
Martial hata akiwa off-form bado kuna vitu basic anafanya unaona sio mbaya

,kuna saa natamani Ole aendelee kubaki kuna saa nachoka ila anyway tumpe nafasi zaidi pengine mazuri yaweza kuja km kwa Klopp

