Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

OLE GUNNAR NA WOODWARD WAGEUKA MJADALA MZITO MAN UTD.



MANCHESTER, ENGLAND . HII Manchester United itawatoa watu roho. Juzi Jumapili, waliteseka sana uwanjani Anfield, wakapigwa 2-0 na Liverpool na baada ya hapo kila mtu anasema lake kwamba huyu hafai, yule hafai.
Beki na nahodha wa zamani wa miamba hiyo ya Old Trafford, Gary Neville kwa kauli moja amemshushia jumba bovu Makamu Mwenyekiti Mtendaji wa klabu hiyo, Ed Woodward kuwa hafai, anapaswa kuondoka haraka.
Neville alisema anashangaa kuona wamiliki wa Man United, familia ya Glazer wanaendelea kubaki na Ed Woodward mtu ambaye anaifanya timu hiyo kuwa ya kawaida kutokana na kufeli kwenye dili zake nyingi za usajili.
Neville alisema Woodward amekuwa akifanya dili za hovyo tu kwenye klabu hiyo kwa kushindwa kusajili wachezaji wa maana na matokeo yake Man United inakuwa na kikosi kichekesho ndani ya uwanja.
Baadhi ya wachezaji waliosajiliwa na Ed Woodward ni Angel Di Maria, Radamel Falcao Bastian Schweinsteiger, wakati wenzao kama Liverpool imewekeza kwa mastaa kama Mohamed Salah, Sadio Mane, Virgil van Dijk.
“Siuelewi kabisa huu uwekezaji wake anaofanya kwenye kikosi kwa kipindi cha miaka mitano, sita au saba sasa iliyopita,” alisema Neville.
“Niliona takwimu fulani wiki iliyopita zinasema kwamba Man United ni timu ya pili inayoongoza kulipa mishahara duniani. Sasa hiyo mishahara wanakilipa kikosi gani? Kwa kweli huyu mtu hapaswi kabisa kusamehewa. Hakika.
“Siwezi kubadili umiliki wa Manchester United, hakuna anayeweza kufanya hivyo. Lakini, nashindwa kuwaelewa hawa wamiliki wanafanyaje kazi na kiungo huyo anayeshindwa kujenga timu ya ubingwa tangu Sir Alex Ferguson alipoondoka. Ona kama hujapoteza kazi kwa kushindwa kufanya uwekezaji wa maana kwenye timu, basi kigezo tu cha kulipa mishahara mikubwa wachezaji wa hovyo ndani ya uwanja hilo linatosha kukuondoa kwenye kiti unachokaria. Lazima niseme, kuna kitu hakipo sawa.”
Wakati Neville akitaka Woodward aondoke, wenzake Roy Keane na Jamie Carragher walikuwa kwenye mjadala wa kuhusu Kocha Ole Gunnar Solskjaer kama anastahili kuendelea kukalia kiti hicho cha ukocha huko Old Trafford. Iliulizwa sana kama kweli Solskjaer ni sahihi kuendelea kubaki Old Trafford na hapo ndipo ulipoanza mjadala mzito, huku Patrice Evra na Graham Souness walibaki kuwa wasikilizaji tu wawili hao wakibishana.Keane alimuuliza Carragher: “Vipi kuhusu makocha waliopita, unasema kwamba nao walikuwa wahovyo?”
Carragher akajibu: “Klabuni Manchester United? Unadhani kwamba walifanya kazi nzuri? Mlimkosoa Mourinho wakati akiwa anainoa timu.”
Keane akajibu: “Lakini, Ole anahitaji muda zaidi.”
Carragher akauliza zaidi: “Anahitaji muda zaidi? Mlimpa muda zaidi Mourinho? Kwa kiwango cha timu yake ilichokionyesha Anfield mwaka juzi?” “Mechi ni kama hii tu. Tuhoji kama kama Ole kwenye ana CV za kuendelea kuwa kocha na zile sababu za wengine zilizowafanya aondoke,” Keane alijibu.
Carragher akamjibu: “Hiyo CV ya Ole ndicho kitu kinachotia wasiwasi.”

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mie nadhani anatumia vijana sana sababu hana option nyingi. McTomminey,DJ,Greenwood na Brandon wanacheza sababu Ole hana mbadala kwa sasa.Na pia matumizi ya vijana wengi ndani ya kikosi ili uwe umefanikiwa inatakiwa matokeo sio kupata matokeo mabovu kama sisi.
Hoja yako ina sound kwa baadhi ya wachezaji. Mictommiyn amemkalisha Matic benchi mara kadhaa. Hivyo hvyo kwa Brandon -Shaw na Young.

Sent using simu mbovu
 
Chelsea 2 - 2 Arsenal

Perfect result

NB: Chelsea wameonesha udhaifu mkubwa sana
Nawatakia kila la kheri mpate draw ya 2 kwa 2

Walioweka GG wapate mboga wapeleke nyumbani

Walioweka Over 2.5/3.5 wafurahie matunda ya beki mbovu za Arsenal na Chelsea

Mashabiki wa United wafurahie United kupunguza gape la top 4 na Chelsea tuzidi kumwacha Arsenal

In the end every body is happy

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye swala la ku'trust young player OGS uwa namuelewa sana, na vijana uwa hawatak kumuangusha wanajituma mno, angalia kama yule Scot Mctomey
Ebu tumvumilie Ole mpaka mechi ya mwisho mwa msimu ndio tum'judge

Sent using Jamii Forums mobile app
Do you know Mourinho ndio alimpa nafasi McTominay na aliamua kabisa kumpiga benchi Pogba na mwisho wa msimu alimpa tuzo ambayo kwenye klabu haikuwepo kabisa
 
Unaweza ukatoa mfano wa mchezaji ambae Man U wamemtaka akachomoa kipindi cha Ole? Sababu issue ya Haaland si mchezaji ametukataa bali ni club chini ya Woodward wamechomoa. Ni kama issue ya Bruno sasa hivi mchezaji yupo Willing kuja ila club haikubaliani na fee. Same kwa Dybala dirisha lililopita.

Na ole ndio amemnoa Haaland kuna kitu gani cha ajabu ukienda kwa kocha aliekuibua?

Na mkuu ni wachezaji wachache sana vijana ambao wanaweza kumkataa ole, So far tumeona anatumia watoto wengi na wengi viwango vyao vime improve zaidi, watu kama Rashford, Martial, James, Williams, Mc tominay, lindelof, AWB etc ni watoto na wapo katika form of their life hawajawahi cheza vizuri kama hivi.

Na kuhusu client wa Raiola mkuu anachukua wachezaji wazuri ndio ila wanakuwa na End mbaya karibia wote, natafuta hapa mchezaji wa Raiola ambae ana End nzuri simpati nisaidie.
So James,AWB,Lindelof,McTominay,Williams,Martial wako kwenye form of life ??? be serious Chief
Why Woodward ambaye alikubali kumpa Sanchez mshahara kufuru na kumpa Raiola agent fee kwenye usajili wa Pogba now anagoma kutoa hizo add ons ?

Pogba alifundishwa na OGS kwenye academy lakini sasa hataki kufundishwa nae kuna factors nyingi za kuangalia kucheza timu na Haaland was right kwenda Dortmund badala ya United kwa sasa tungeanza kumtukana baada ya mechi 5

Mafanikio kwa mchezaji ni kuchukua makombe + fedha ,Nedved (Balon Dior winner) ,Ibrahimovic,Pogba,Matuidi,Maxwell ni miongoni mwa wachezaji waliofanikiwa kwenye soka sijui kwako mafanikio ni nini
 
OLE GUNNAR NA WOODWARD WAGEUKA MJADALA MZITO MAN UTD.



MANCHESTER, ENGLAND . HII Manchester United itawatoa watu roho. Juzi Jumapili, waliteseka sana uwanjani Anfield, wakapigwa 2-0 na Liverpool na baada ya hapo kila mtu anasema lake kwamba huyu hafai, yule hafai.
Beki na nahodha wa zamani wa miamba hiyo ya Old Trafford, Gary Neville kwa kauli moja amemshushia jumba bovu Makamu Mwenyekiti Mtendaji wa klabu hiyo, Ed Woodward kuwa hafai, anapaswa kuondoka haraka.
Neville alisema anashangaa kuona wamiliki wa Man United, familia ya Glazer wanaendelea kubaki na Ed Woodward mtu ambaye anaifanya timu hiyo kuwa ya kawaida kutokana na kufeli kwenye dili zake nyingi za usajili.
Neville alisema Woodward amekuwa akifanya dili za hovyo tu kwenye klabu hiyo kwa kushindwa kusajili wachezaji wa maana na matokeo yake Man United inakuwa na kikosi kichekesho ndani ya uwanja.
Baadhi ya wachezaji waliosajiliwa na Ed Woodward ni Angel Di Maria, Radamel Falcao Bastian Schweinsteiger, wakati wenzao kama Liverpool imewekeza kwa mastaa kama Mohamed Salah, Sadio Mane, Virgil van Dijk.
“Siuelewi kabisa huu uwekezaji wake anaofanya kwenye kikosi kwa kipindi cha miaka mitano, sita au saba sasa iliyopita,” alisema Neville.
“Niliona takwimu fulani wiki iliyopita zinasema kwamba Man United ni timu ya pili inayoongoza kulipa mishahara duniani. Sasa hiyo mishahara wanakilipa kikosi gani? Kwa kweli huyu mtu hapaswi kabisa kusamehewa. Hakika.
“Siwezi kubadili umiliki wa Manchester United, hakuna anayeweza kufanya hivyo. Lakini, nashindwa kuwaelewa hawa wamiliki wanafanyaje kazi na kiungo huyo anayeshindwa kujenga timu ya ubingwa tangu Sir Alex Ferguson alipoondoka. Ona kama hujapoteza kazi kwa kushindwa kufanya uwekezaji wa maana kwenye timu, basi kigezo tu cha kulipa mishahara mikubwa wachezaji wa hovyo ndani ya uwanja hilo linatosha kukuondoa kwenye kiti unachokaria. Lazima niseme, kuna kitu hakipo sawa.”
Wakati Neville akitaka Woodward aondoke, wenzake Roy Keane na Jamie Carragher walikuwa kwenye mjadala wa kuhusu Kocha Ole Gunnar Solskjaer kama anastahili kuendelea kukalia kiti hicho cha ukocha huko Old Trafford. Iliulizwa sana kama kweli Solskjaer ni sahihi kuendelea kubaki Old Trafford na hapo ndipo ulipoanza mjadala mzito, huku Patrice Evra na Graham Souness walibaki kuwa wasikilizaji tu wawili hao wakibishana.Keane alimuuliza Carragher: “Vipi kuhusu makocha waliopita, unasema kwamba nao walikuwa wahovyo?”
Carragher akajibu: “Klabuni Manchester United? Unadhani kwamba walifanya kazi nzuri? Mlimkosoa Mourinho wakati akiwa anainoa timu.”
Keane akajibu: “Lakini, Ole anahitaji muda zaidi.”
Carragher akauliza zaidi: “Anahitaji muda zaidi? Mlimpa muda zaidi Mourinho? Kwa kiwango cha timu yake ilichokionyesha Anfield mwaka juzi?” “Mechi ni kama hii tu. Tuhoji kama kama Ole kwenye ana CV za kuendelea kuwa kocha na zile sababu za wengine zilizowafanya aondoke,” Keane alijibu.
Carragher akamjibu: “Hiyo CV ya Ole ndicho kitu kinachotia wasiwasi.”

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimefurahi watu senior like Garry Neville kuanza kumyoshea kidole Woodward hadharani, haiwezekani kila kocha awe mbovu uku yeye akiwa boss

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwa team OSG basi leo wanatoa sare au wanapoteza utazania ka bet Manchester United aiwezi kumaliza juu ya Chelsea
OLE OUT
ED OUT
GREAZER FAMILY OUT
 
Back
Top Bottom