Najua we are comfortable now, na kitendo cha Haaland kusajiliwa Dortmund hakiwaumi watu wengi sababu ma strikers wetu wote kwa sasa wapo fiti na wapo form, sidhani kama watu wangekuwa na mtazamo huo huo mwezi septemba, Oktoba na Novemba mwaka huu unaokwisha
Unasema tungesajili senior striker ili awafundishe, nimewahi kuuliza huko nyuma, senior striker unayewaongelea ambao wapo sokoni ni akina nani, sikupata majibu. Utanishangaza ukinitajia Mandzukic, Falcao, Ibrahimovic wakati tumemuacha Lukaku ambaye angeweza kufanya hiyo kazi ya "kuwafundisha madogo" kama unavyoshauri
Kwa sasa hivi kikosi chetu kina pure striker wawili, Martial na Greenwood ambaye bado hajacheza senior football kiasi cha kwamba akaaminiwa na kupewa majukumu ya timu, Rashy sio striker (sio namba 9), DJ sio namba 9.
Haaland sio senior (kwa idadi ya miaka aliyonayo), lakini ni senior kwa uzoefu wa kucheza senior football. Pamoja na kumbeza kwamba ametokea ligi laini, lakini kote huko amekuwa outstanding. Ligi ya mabingwa Ulaya ameng'ara, je na hayo ni mashindano nyoronyoro? Wachezaji wakubwa wote Ulaya tunawapitisha kuwa ni bora au wabovu kwa namna watakaocheza ligi ya mabingwa Ulaya.
Haaland ana magoli 8, ni wa pili nyuma ya Lewandowski mwenye magoli 10, na wanaomfuata wana goli 6, kwenye chati ya wafungaji wa UCL 2019/2020. Kuliweka suala hili ili lieleweke vizuri, Haaland kiufungaji yupo juu ya mchezaji anayetajwa kuja kuwa Ballon'dour winner siku zijazo, Mbape ambaye ana goli 5 kwenye UCL. Kwahiyo hapa tusikaririshane uongo kwamba dogo anafunga magoli ligi nyepesi nyepesi tu, huyu dogo ametoboa safu za ulinzi chini ya Koullibaly na VVD, kwa taarifa yako.
Nakukumbusha pia RB Salzburg, timu unayodai inacheza ligi nyepesi ndio imewaleta kwenye ulimwengu wa soka, akina Mane, Naby Keita, Minamino (Liverpool) Upemecano (RB Leipzig) n.k. Kwanini Haaland asiwe bora kisa tu ametokea ligi ya Austria.
OGS akiwa mchezaji alitokea Norway, Nesterloy alitokea Uholanzi, Delle Ali ametokea MK Dons timu ya ligi daraja la 3, Ibrahimovic alitokea Malmo ya Sweden, orodha ni ndefu sana.
Pia nikukumbushe, kuwa scouts wapo kwa ajili ya hiyo kazi, ya kutafuta diamonds kwenye mashimo na si kwenda kununua almasi kwenye masoko yaliyopo mjini
Mwisho nikwambie, kusajili siku zote huwa kuna asilimia flani ya gambling, kuna wakati unaweza ukasajili mchezaji na akacheza kwa kiwango ambacho haukukitazamia au akang'ara, kwa United kufanya gambling ya £20million tu kwa Haaland isinge disturb pochi nene ya Glazers.
Kitu pekee kilichonifurahisha kwa huyu dogo kwenda Dortmund na sio kuja United, ni kutoongeza wigo wa kufanya biashara na tapeli Mino Raiola
Huyu dogo ameshakwenda, tuangalie mambo mengine
Sent using
Jamii Forums mobile app