Alexander Lukashenko
JF-Expert Member
- Sep 9, 2017
- 4,103
- 9,529
Ko mkuu unadhani hapendi kufanya subs au hakuna wa kuingia....anayeingia na anayetoka sawa tu.....Ole sio kocha bali mhamasishaji wa kuitafuta morali ya wachezaji. Tangu usajili wake alitutia mashaka kwa kuonekana kupendelea mazao ya academy au waingereza kuichezea united.
Pili,huoni mfumo au muunganiko wa utengenezaji mashambulizi zaidi ya asilimia kubwa kuwa magoli ya juhudi binafsi ya wachezaji (achilia mbali goli la Martial dhidi ya Cardiff mwaka jana),huoni la maana analofanya hapo.
Upangaji kikosi nao umekuwa wa mazoea zaidi,haiwezekani mechi dhidi ya city,Watford, westham kikosi ni kile kile,mbinu ni zile zile na mbaya zaidi mfumo pia haubadiliki.
Amekuwa na tabia ya kuogopa kuwafanyia mabadiliko wachezaji wenye majina makubwa kiasi mfano martial, rashford na pogba,au anakuwa hajui afanye nini.
Hadi sasa ana mwaka na zaidi lakini sioni jipya tunalolifanya chini ya huyu jamaa zaidi ya kupata ushindi usiotabirika tu. Wachezaji hawamuogopi kabisa,kiwango cha leo na kesho ni sawa sawa. Mbaya zaidi,makosa wanayoyaona watu wasio na taaluma kama yake,yeye bado anatudanganya kuwa mambo yako sawa. Mfano usajili wa kiungo na striker tangu majira ya joto,yeye anaongelea majeruhi wakirudi utakuwa sawa na usajili mpya. Hivi kweli tunategemea jipya toka kwa pogba na baily kuiimarisha united?
Atatufanya tustaafu mapema kuangalia mpira huyu jamaa,