Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mapema kuliko tulivyotazamia?
Screenshot_20191129_145959_com.instagram.android.jpeg
 
Mambo Ni

Kunakofukuta kwingineko

The hammers wa pande za Upton park zamani...

Toffee wa pale Kati Midland, godson park

Ongeza na wewe list ya kwenye mwishi......
Screenshot_20191129-154201.jpeg
 
Ole anafurahisha bana, kipindi cha kwanza yupo benchi amekodoa na kuvuta vuta goti, kipindi cha pili hivyo hivyo tumepigwa mpaks Dk ya 80 ndio anainuka na kuhamasisha wapress pumbavu, dakika zote alikuwa wapi?
Ole hakupanga kikosi ili tushinde, tumeshafuzu na sasa anawapa tu uzoefu watoto.

Na Europa ni Tofauti na Uefa haijalishi umemaliza wa kwanza au wa pili kuna washindi wa 3 wa makundi toka Uefa unaweza pangwa na yoyote.
 
Ole hakupanga kikosi ili tushinde, tumeshafuzu na sasa anawapa tu uzoefu watoto.

Na Europa ni Tofauti na Uefa haijalishi umemaliza wa kwanza au wa pili kuna washindi wa 3 wa makundi toka Uefa unaweza pangwa na yoyote.


Kumbe asee! Ila naongelea mechi nyingi bana hata Sheffield anatakiwa ainuke awakemee Rashford na Martial wakileta uboya.


Na huyu Commando Jones. 😂😂 Jinga sana hilo jamaaa.
 
Anahitaji kujengewa confidence tu na team work otherwise ni mchezaji mzuri
hata mimi sielewi kwa nini wadau wengi wanamchukia tahith chong, kiupande wangu namuona kama ni future asset kwa timu yeyote itakayofanikiwa kupata huduma yake.

viongozi wakuu wa klabu wanapaswa kumpa mkataba mpya wa muda mrefu na baadae wampeleke kwa mkopo ligi kuu ya ujerumani, nadhani ndio sehemu sahihi zaidi itakayomuwezesha tahith kujijenga zaidi kisoka la ushindani hususani kimwili na kimbinu.

wajerumani wapo vizuri sana kwa miaka hii ya karibuni linapokuja suala la kukuza vipaji vya wachezaji.
 
Mlioangalia mechi msiache kutupa Positivities kwenye mechi dhidi ya Astana
  • garner na levitt kama upo uwezekano wa kuingia kikosi cha kwanza basi wapewe nafasi na si vibaya kama atapumzishwa andreas perreira kwa kipindi hiki ambacho scott ni majeruhi kwa dhumuni la kupewa nafasi mmoja wao kati ya hao wawili acheze pamoja na fred. Kama haiwezekani basi wapelekwe kwa mkopo japo wa miezi mitano nchini spain wapate kuzidi kujifunza ufundi wa kumiliki mpira eneo la kiungo na si kuwabakisha uingereza sehemu ambayo hawatajifunza chochote cha maana zaidi ya kuwa midfield waliojaa woga nafsini mwao. kama waingereza wanataka kufanikiwa kisoka basi wawapeleke wachezaji wao vijana kwenye ligi ya spain, bundesliga na uholanzi wapate kujifunza soka la kisasa na si mpira huu wa kucover space. paul scholes ndiye kiungo pekee wa kiengereza aliyecheza soka la ushindani kwa muda mrefu ambaye hakuwa na uoga wa kumiliki mpira eneo lolote lile haijalishi amezungukwa na adui kila upande. sijamtaja jack wilshere kwa maana yangu....... hao kina super captain gerrard na super frank lampard walikuwa hawamuwezi yule mzungu kichaa japokuwa kuna baadhi ya maeneo walimzidi sana.
  • wachezaji wenye sifa kama alizonazo gomes haipendezi kuwachezesha eneo la kiungo wa pembeni, sehemu pekee itakayomfanya afurahie soka lake ni namba 10 mwenye jukumu la kushambulia tu na si kuhangaika kukaba, kwa mara nyengine tena kama itatokezea scott akarudi dimbani basi namba 10 itakuwa ni kichekesho kuendelea kumtumia andreas perreira aliyekwishafeli, tuna machaguo mawili muhimu wenye uwezo wa kutupa huduma zaidi ya ile anayoitoa perreira na machaguo hayo ni juan mata na angel gomes...... ole apunguze mapenzi yaliojaa upofu ndani yake, sijawahi kumuona mchezaji aliyekuza kiwango chake akiwa benchi bali kiwango na uzoefu huongezeka pindi mchezaji anapopewa nafasi ya kucheza mara kwa mara
  • achana na yule mlinzi wa kulia anayeitwa Laird, aliyenivutia zaidi ni bwana mdogo aliyejifunga goli, anaitwa bernard........ ni ngumu sana kuamini ila yule dogo anamzidi tuanzebe kiutulivu....... tuanzebe ana tabia za eric bailly
1575057040514.png
 
  • garner na levitt kama upo uwezekano wa kuingia kikosi cha kwanza basi wapewe nafasi na si vibaya kama atapumzishwa andreas perreira kwa kipindi hiki ambacho scott ni majeruhi kwa dhumuni la kupewa nafasi mmoja wao kati ya hao wawili acheze pamoja na fred. Kama haiwezekani basi wapelekwe kwa mkopo japo wa miezi mitano nchini spain wapate kuzidi kujifunza ufundi wa kumiliki mpira eneo la kiungo na si kuwabakisha uingereza sehemu ambayo hawatajifunza chochote cha maana zaidi ya kuwa midfield waliojaa woga nafsini mwao. kama waingereza wanataka kufanikiwa kisoka basi wawapeleke wachezaji wao vijana kwenye ligi ya spain, bundesliga na uholanzi wapate kujifunza soka la kisasa na si mpira huu wa kucover space. paul scholes ndiye kiungo pekee wa kiengereza aliyecheza soka la ushindani kwa muda mrefu ambaye hakuwa na uoga wa kumiliki mpira eneo lolote lile haijalishi amezungukwa na adui kila upande. sijamtaja jack wilshere kwa maana yangu....... hao kina super captain gerrard na super frank lampard walikuwa hawamuwezi yule mzungu kichaa japokuwa kuna baadhi ya maeneo walimzidi sana.
  • wachezaji wenye sifa kama alizonazo gomes haipendezi kuwachezesha eneo la kiungo wa pembeni, sehemu pekee itakayomfanya afurahie soka lake ni namba 10 mwenye jukumu la kushambulia tu na si kuhangaika kukaba, kwa mara nyengine tena kama itatokezea scott akarudi dimbani basi namba 10 itakuwa ni kichekesho kuendelea kumtumia andreas perreira aliyekwishafeli, tuna machaguo mawili muhimu wenye uwezo wa kutupa huduma zaidi ya ile anayoitoa perreira na machaguo hayo ni juan mata na angel gomes...... ole apunguze mapenzi yaliojaa upofu ndani yake, sijawahi kumuona mchezaji aliyekuza kiwango chake akiwa benchi bali kiwango na uzoefu huongezeka pindi mchezaji anapopewa nafasi ya kucheza mara kwa mara
  • achana na yule mlinzi wa kulia anayeitwa Laird, aliyenivutia zaidi ni bwana mdogo aliyejifunga goli, anaitwa bernard........ ni ngumu sana kuamini ila yule dogo anamzidi tuanzebe kiutulivu....... tuanzebe ana tabia za eric bailly
View attachment 1276671
Gomez hata mimi ananifurahisha sana uchezaji wake muda wote anawaza kutengeneza tu nafasi, nadra sana kumkuta anacheza back pass, ila nafkiri bado kwa premier league, Ngoja apate uzoefu huku huku kwenye cup games. Amecheza mechi zote ambazo yupo fit.

Na Perreira ametolewa mkopo miaka miwili spain ila hajajifunza hilo soka la kispaniola, kuna wengine mkuu viwango vyao vipo hivyo tu.
 
Gomez hata mimi ananifurahisha sana uchezaji wake muda wote anawaza kutengeneza tu nafasi, nadra sana kumkuta anacheza back pass, ila nafkiri bado kwa premier league, Ngoja apate uzoefu huku huku kwenye cup games. Amecheza mechi zote ambazo yupo fit.

Na Perreira ametolewa mkopo miaka miwili spain ila hajajifunza hilo soka la kispaniola, kuna wengine mkuu viwango vyao vipo hivyo tu.
mwanzoni andreas perreira alikuwa vizuri sana kipindi kile anacheza academy ila sijui ukubwani amekutwa na balaa gani.
brother kama umeangalia mechi yetu kipindi cha kwanza bila ya shaka utakuwa umeuona uwezo wa garner na levitt.

unaikumbuka combination ya joe allen na britton pale swansea city ya brendan rodgers?
ile combination nimeiona tena jana kwa wachezaji wa kiingereza.
nakubali si kila mchezaji aliyekwenda spain amefanikiwa kisoka ila wachezaji wengi waliopitia spain hawana ugonjwa wa kutetemeka ovyo pindi wanapokuwa na mpira ndio maana nikapendekeza wapelekwe spain, tatizo kubwa linalotusumbua nyakati hizi ni kukosa midfield wenye ufundi wa asili kwenye timu yetu ukimuondoa labile.

garner na levitt ni assets zisizostahili kupelekwa kwa mkopo stoke city.
 
Hivi tunasubiri nini kumtimua huyu jamaa
  • wachezaji wetu bado hawajachoshwa na uwepo wa OGS,
  • sababu kubwa inayopelekea kufukuzwa kwa makocha wengi barani ulaya ni baadhi ya wachezaji kumwekea mgomo baridi kocha mkuu
  • uongozi wa juu kuchoshwa na mwalimu...................... barcelona kwa mwaka wa tatu huu wameshindwa kufuzu fainali ya champions league lakini bado wameendelea kumuamini ernasto valverde licha ya mashabiki kukosa imani naye
  • matokeo mabovu yanayoendana na speed ya muda, kama unataka ole atimuliwe basi omba dua zaidi mwezi huu wa december apoteze mechi mfululizo............................................... mara nyingi sana mwezi huu ndio hukumu ya makocha inapotolewa
sababu hizo hapo juu zote zinamuhusu unai emery ndio maana alifukuzwa licha ya kufanana kimatokeo na OGS
 
Nadhani ni mchezaji mzuri, lakini not good enough kwa United. Anapoteza mipira sana, nguvu hana, ana piga pasi fyongo. Hata Januazaj alikuwa ana dalili nzuri kuliko huyu. Ninakubali baadae anaweza kuwa mzuri lakini naona chance yake ni ndogo sana.

Tusisahau pia klabu hata ikitoa bachi moja ya wachezaji wa academy 3 wakawa ma superstar, hiyo bachi inaonekana ina mafanikio sana (rejea class of 1992 na hata akina Pogba). Bachi zilizobaki hazitoi au zinatoa wachezaji mmoja mmoja tu

Kwa bachi hii, Chongy yupo nyuma ya Greenwood, Gomes, Williams, Garner & Co.
hata mimi sielewi kwa nini wadau wengi wanamchukia tahith chong, kiupande wangu namuona kama ni future asset kwa timu yeyote itakayofanikiwa kupata huduma yake.

viongozi wakuu wa klabu wanapaswa kumpa mkataba mpya wa muda mrefu na baadae wampeleke kwa mkopo ligi kuu ya ujerumani, nadhani ndio sehemu sahihi zaidi itakayomuwezesha tahith kujijenga zaidi kisoka la ushindani hususani kimwili na kimbinu.

wajerumani wapo vizuri sana kwa miaka hii ya karibuni linapokuja suala la kukuza vipaji vya wachezaji.
 
  • wachezaji wetu bado hawajachoshwa na uwepo wa OGS,
  • sababu kubwa inayopelekea kufukuzwa kwa makocha wengi barani ulaya ni baadhi ya wachezaji kumwekea mgomo baridi kocha mkuu
  • uongozi wa juu kuchoshwa na mwalimu...................... barcelona kwa mwaka wa tatu huu wameshindwa kufuzu fainali ya champions league lakini bado wameendelea kumuamini ernasto valverde licha ya mashabiki kukosa imani naye
  • matokeo mabovu yanayoendana na speed ya muda, kama unataka ole atimuliwe basi omba dua zaidi mwezi huu wa december apoteze mechi mfululizo............................................... mara nyingi sana mwezi huu ndio hukumu ya makocha inapotolewa
sababu hizo hapo juu zote zinamuhusu unai emery ndio maana alifukuzwa licha ya kufanana kimatokeo na OGS
Kinachomfanya Ole asichukiwe na wachezaji ni upole wake na....

Kinachomfanya asichukiwe na uongozi ni NDIO MZEE

Mwenendo huu sio mzuri kwa afya ya timu kubwa kama MAN
 
Back
Top Bottom