Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tim crul huwa tunamfunga kwa tabu kila mechi
Kwa wasiomjua Tim Krul kwenye kudaka/kutoa penati

Huyu ndio kwenye World Cup, zilipokuwa zinakaribia dakika za penati, kipa namba moja wa Uholanzi alitolewa ili kumpisha yeye akae katikati ya milingoti

Ila inauma sana kukosa penati
 
Mkuu asubuhi ulisema huyu Tominay bado sana mpaka tupate mid experienced mara hii umebadili msimamo ?

Jaribu kuwa na akiba ya maneno unatuchangaya sisi mashabiki wenzako
Huyu dogo sina wasiwasi nae hakika tumepata namba 6 akifikisha miaka 25 ni noma mourinho hapa nampongeza
 
Baada ya game ya Liverpool vijana wameongeza confidence wanatake risks ya kushambulia.

Ugonjwa pekee kwa sasa ninaouona ni full backs zetu kutokuwa na makali ya kushambulia na tunashambuliwa zinakuwa vulnerable sana.

Kushoto Young hajapiga hata cross moja kulia hivyo hivyo wan Bisaka hata kupiga cross hajui kama Young kibaya zaidi Bisaka anakabia deep sana.
 
Good Perfomance,3 goals 3 points

√McTominay my MOTM,sema kafanya kutuchoma kiboya sana dakika za mwishoni

√James alikuwa poa,Rashford alikuwa poa,Martial alikuwa poa

√Bissaka anafanya kazi yake vizuri kabisa..japo contribution yake inahitajika zaidi wakati timu ikiwa inapanda..

√Young kazeeka hadi akili,pia anapitwa kizembe kabisa

√Fred akipasiwa mpira ninapata hofu kwekweli..maana ninakuwa sijui kama atapiga basi nzuri au atatoa boko..though amepambana kiasi chake leo

√Garner kacheza poa dakika alizopewa..kocha inabidi aendelea kumtafutia dakika za kucheza hata kama ni kidogo

Next stop Darajani..Chelsea atakufa??
 
Njoo ushangilie matokeo sasa, unajaji mechi kwa dk 10?
Nakushauri usitazame huu mpira mkuu,nimetazama dakika 12 nimepata kichefuchefu.

Ole sijui anafundisha nini hawa vijana wake,utumbo mtupu. Hata wakiwa na mpira huoni kitu wanafanya.
 
Angalau leo tumetengeneza nafasi nyingi za kuscore... Nimeiona faida ya Uwepo wa RASH + MARSH.
Ila timu inapungukiwa viungo wa kupandisha timu, yaani ni JAMES peke yake ndio anaonekana kupandisha timu na kutengeneza nafasi, tofauti na hapo mpaka Rash afate mipira nyuma aanze safari.
Scott atafutiwe watu wawili wekundu usoni kama yeye wamsaidie kumwaga damu za watu hapo kati.
 
Huyu jamaa huwa namkubali sana, tangu alipo ondoka Herrera huyu ndio my favorite player pale United.

Pereira.
images%20(3).jpeg
 
Mkuu asubuhi ulisema huyu Tominay bado sana mpaka tupate mid experienced mara hii umebadili msimamo ?

Jaribu kuwa na akiba ya maneno unatuchangaya sisi mashabiki wenzako
Mkuu soma hapo nimekwambia akifikisha miaka 25 kwa sasa bado sana
 
Mid ya Tominay, Fred na Pereira imeanza kusettle soon tutaanza kupata mwanga
Hutaweza kuwaona hao madogo mech na city au liverpool walipobadili mbinu kipindi cha pili bado tunahitaj watu wa kazi

Angalia timu kama
Buyern munich
Juventus
Atletico madrid
Real madrid
Barcelona
Angalia sehem ya kiungo kisha njoo kwetu hizi mech za wakina norwich sio kipimo sahihi sema vile tunashangilia ushindi tu lakin ukija uhalisia sisi bado sana ktk eneo la kiungo hizo timu kama tunapambana nazo basi had wakina rashford watakuwa mabek
 
Mkuu asubuhi ulisema huyu Tominay bado sana mpaka tupate mid experienced mara hii umebadili msimamo ?

Jaribu kuwa na akiba ya maneno unatuchangaya sisi mashabiki wenzako
Pia nafikir hukuelewa post yangu ipo wazi sana kwa sasa siwez kumuweka scott kwenye level ya viungo makin bado sana nimetoa na muda hapo angalau miaka 25 mtu anaanza kuwa mkomavu huwez hiyo sehem ya kiungo ikaenda pambana na top 5 teams in europe utegemee tutapona kwa jina la timu na wachezaj tulionao ni vitu viwili tofaut class of 92 ilikuwa na wacheza kama 7 wazoefu unaweza kuona namna gan wakina giggs na scholes walikaa muda mrefu kwenys game

Scholes kaja kuwa top kwenye level yake miaka 26 leo uniambie scott na pereira ni kiungo unaweza mtegemea mpambane na top teams lazima mnyanyasike tu


Na tangu Roy Kean alipoondoka hatukuwahi kupata mbadala japo wakina scholes walikuwepo lakin hawakupiga kazi kama ya Roy Kean sehem anayocheza scott ni ngumu sana mkuu yaani hadi muda huu pengo lipo unaweza kuona namna gan sir alex alihangaika kupata mbadala kasajili sana lile eneo lakin wap had wakina veron wamepita pale

Na ndio maana tunaweza kuona walau kanajitahidi tuone akikomaa atakuwa bora? Nasema hivyo wakina lingard,cleverly,welbeck na januzaj walianza na moto huo wanapokaomaa wanarudi nyuma Huenda akaja kuziba pengo la mud mrefu sumbufu
 
Ushindi nimeupokea kwa mikono miwili, timu bado bado kuna kazi kubwa ya kufanya.
Ushindi mmoja na timu tuliyocheza nayo si vitu vya kufurahi sana wengi tunajisahau hapa unakutana na timu inayoziba nafasi kama wolves na crystal palace story inakuwa tofaut hawa norwich tumewafunga wanafunguka sana
 
Back
Top Bottom