Hii timu kwa kweli inanipa hasira sana. Hivi hawa wachezaji wa Man U wanakosa kitu gani ambacho wengine wanapata?
Vitoto vidogo vinalimbikizwa mishahara mikubwa pasipo kazi yoyote ya maana kweli!!!! Wolves wana aina gani ya wachezaji wenye kuzidi Man U, au hawa Newcastle wamesajili wachezaji wa level ipi ambao wachezaji wetu hawawezi kucheza nao na wapate matokeo?
Hatuwezi kuishi kujisifia mafanikio ya miaka kadhaa wakati tunateketea, tangu atoke Sir Ferguson hakuna lolote la maana limefanyika.
Ina maana uongozi wa Man U hauoni haya madudu au upo kwa ajili ya kutengeneza faida (pesa) msimu wa usajili unafika tunaondoa wachezaji huku tukiacha wazee na watu wasio na umuhimu kwenye timu.
Unaona huwezi kufanya kazi ya Lukaku mwenye kuijua EPL vyema na kwa umri wake akiwa na mabao zaidi ya 100 ya EPL tunabaki na Rashford kweli!!! Tuliuza Lukaku kisa nini sasa kama hatukuwa na replacement yake?
OGS nacho kinafiki kweli hiki kijiti yaani kinashindwa kuwa na msimamo na kupata wachezaji anabaki kuwa NDIYO MZEE hivi kuna mizungu minafiki kumbe.
Lampard anaichukua Chelsea wakiwa na ban ya usajili ila anaunganisha timu na kila mmoja anaona wazi kuwa Chelsea ina jitahida iwapo uwanjani. Tumekuja kuua kipaji cha Wanna na James kwa upumbavu wa uongozi wetu.