Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Ole ameuza wachezaji wazuri sana ambao wangetumiwa na Allegri.

Allegri akija atakuta makapi ambayo hayatampa mafanikio.

Ndio maana najiuliza kama hatuna DoF hatutafika popote kwasababu kila kocha anakuja na wachezaji wake.

Ila katika yote Ole sio kocha, anafanya makosa ya wazi kabisa ambayo yanaigharimu timu na anaona yupo sahihi wakati yupo wrong.

Kwanza, kutumia mfumo ambao haumpi mafanikio kila siku.

Pili, kuuza wachezaji muhimu na kubaki na takataka ambazo zinasuasua.

Tatu, kukubali kuanza msimu na kikosi dhaifu na kuwa comfortable kabisa.

Glazers na Ed ni kansa pale Utd.
Mkuu
1. Ole amefanya usajili wa wachezaji watatu na wote mpaka Sasa Hivi wamehit, James mwezi wa Pili Sasa mfululizo yupo nominated mchezaji Bora wa mwezi, na mwezi uliopita ameshinda, Huyu Ni replace ya Sanchez aliecheza miezi 18 na kufunga goli 3 tu. AWB na Maguire wote wapo vizuri Sana.

2. Wachezaji walioondoka Nani alikuwa anatusaidia? Lukaku? Sanchez? Smalling? Hebu tuwe realistic jamani, tulikuwa kila siku tunasema wachezaji wanalipwa mishahara mikubwa na hawafanyi lolote uwanjani, timu Sasa Hivi mishahara inabalance ukitoa De Gea wote Ni chini ya 300K na Hilo Ni Jambo zuri, ndio maana japo timu haifanyi vizuri sijawahi kusikia dressing room imegawanyika.

3. Kikosi Ni dhaifu kweli mkuu lakini tuwe wavumilivu maana huu ndio wakati, wakujua magarasa na United quality, trust me Kama Ole ana guts za kuwatoa kina Sanchez Kuna wachezaji wengi tu watakula panga, jamaa Ni mkali na hataki mchezo usione muda wote yupo positive anacheka cheka kwenye interview, mwacheni Ole ajenge timu, tukishakuwa na wachezaji angalau 11 kila position Kuna mtu then tunaweza Leta kocha wa kubeba makombe.

Timu yetu Kuna position kibao hakuna watu miaka nenda Rudi, hatuna winga wa kulia, hatuna creative midfield tofauti na Pogba, namba 10 Tia maji Tia maji, beki wa kushoto Ni luke Shaw anaspend muda mwingi Majeruhi. Tunahitaji mtu ajenge timu zaidi, tusijifananishe kabisa na hao kina Man city na Liverpool.
 
Simkubali sana Allegri kwangu mimi my choice would be
1 Eric Ten Hag
2 Nagelsman
3 Leornado Jardim
4 Eddie Howe
5 Allegri
Kwa man U ya Sasa hata aje Nani Ni majanga tu, kitu kitakachotuokoa sisi Ni man U ipate hasara miaka Kama 2 hivi, kina glazzer wakiona hakuna Faida watauza tu,

Tajiri mkuu wa Uingereza anaitaka Man U bila kusahau prince wa Saudia.

Ila tukimpata van De sir, Ten Hag anakuja bila wasi wasi.
 
Wewe ndio ulisema lingard ni hatari sana akiwa hana mpira
Mkuu
1. Ole amefanya usajili wa wachezaji watatu na wote mpaka Sasa Hivi wamehit, James mwezi wa Pili Sasa mfululizo yupo nominated mchezaji Bora wa mwezi, na mwezi uliopita ameshinda, Huyu Ni replace ya Sanchez aliecheza miezi 18 na kufunga goli 3 tu. AWB na Maguire wote wapo vizuri Sana.

2. Wachezaji walioondoka Nani alikuwa anatusaidia? Lukaku? Sanchez? Smalling? Hebu tuwe realistic jamani, tulikuwa kila siku tunasema wachezaji wanalipwa mishahara mikubwa na hawafanyi lolote uwanjani, timu Sasa Hivi mishahara inabalance ukitoa De Gea wote Ni chini ya 300K na Hilo Ni Jambo zuri, ndio maana japo timu haifanyi vizuri sijawahi kusikia dressing room imegawanyika.

3. Kikosi Ni dhaifu kweli mkuu lakini tuwe wavumilivu maana huu ndio wakati, wakujua magarasa na United quality, trust me Kama Ole ana guts za kuwatoa kina Sanchez Kuna wachezaji wengi tu watakula panga, jamaa Ni mkali na hataki mchezo usione muda wote yupo positive anacheka cheka kwenye interview, mwacheni Ole ajenge timu, tukishakuwa na wachezaji angalau 11 kila position Kuna mtu then tunaweza Leta kocha wa kubeba makombe.

Timu yetu Kuna position kibao hakuna watu miaka nenda Rudi, hatuna winga wa kulia, hatuna creative midfield tofauti na Pogba, namba 10 Tia maji Tia maji, beki wa kushoto Ni luke Shaw anaspend muda mwingi Majeruhi. Tunahitaji mtu ajenge timu zaidi, tusijifananishe kabisa na hao kina Man city na Liverpool.
 
Wewe ndio ulisema lingard ni hatari sana akiwa hana mpira
Ndio nimesema na sio Mimi tu Kuanzia Fergie, Moyes, lvg, Mou na Mpaka Ole wote wanamrate vizuri tu. Na pia nikasema uchezaji wake unafanana na ji sung park, ana mechi zake na ana umuhimu wake, Ni strategic player, angekuja Dybala Wala usingemuona akianza Kama 10.
 
Naumia sababu timu yetu haijielewi Kama kuku aliekatwa kichwa, hatuna identity Bora liende tu.

Mkuu Mimi nilimtetea lvg humu asitimuliwe, nikamtetea na Mou asitimuliwe na nitamtetea na Ole vile vile, Tatizo la man U halijawahi kuwa Kocha.

Hata AlleGri akija baada ya Muda watu wataanza vile vile kumtupia maneno kwamba hawamtaki.
Mkuu embu tuwe critical kidogo kwenye hili swala

Ni kweli Shida yetu sio kocha??..kwanini shida sio kocha??...kama fedha tumetumia sana na improvement imekuwa ni ndogo sana tokea 2013

Mfano Ole amepewa mahitaji yake(hata kama siyo yote)..yeye akaidhinisha kuuzwa kwa Lukaku bila ya replacement na maamuzi mengine..Tunaanza msimu timu inachechemea..Mechi saba za ligi tumeweza kushinda zaidi ya goli moja kwenye mechi moja tu..Then why Kocha asihusike kwenye Perfomance mbaya ya timu??
 
Oya we sister unawadhalilisha washabiki wenzako wa man united wenye akili timamu....hii JF hujui unabattle na nani usije kukuta Mimi ni baba yako au wewe no bi mkubwa wangu itakuwa sio FRESH.
Dully senous naye ni kahaba wa kiume
 
Mkuu embu tuwe critical kidogo kwenye hili swala

Ni kweli Shida yetu sio kocha??..kwanini shida sio kocha??...kama fedha tumetumia sana na improvement imekuwa ni ndogo sana tokea 2013

Mfano Ole amepewa mahitaji yake(hata kama siyo yote)..yeye akaidhinisha kuuzwa kwa Lukaku bila ya replacement na maamuzi mengine..Tunaanza msimu timu inachechemea..Mechi saba za ligi tumeweza kushinda zaidi ya goli moja kwenye mechi moja tu..Then why Kocha asihusike kwenye Perfomance mbaya ya timu??
Mkuu Lukaku ameuzwa tarehe 8 mwezi wa 8 na dirisha linafungwa tarehe 9, na kwenye mahitaji ya Ole striker Alikuwepo, Tofauti ya Ole na Mou au LVG Ni kwamba OLE Hana tabia ya kuongea Negative kwenye vyombo vya habari wakati Mou yeye hakopeshi anakuchana hata Kama Ni bosi wake.

Tulikuwa linked na Mandzukic + Dybala wote Hawa walikuwa wanakuja pamoja na Wana magoli Yao, tunajua ilikwamishwa na imaging Rights za Dybala, Ila Tetesi zinaendelea January mandzukic anakuja Man UTD.

Bila kusahau majina mengine Kama Ben yedder na Dembele ambao walikuwa linked na Man UTD.

Hata ole mwenyewe badala ya Dirisha kufungwa ameshakiri Mara 2 kwamba anahitaji striker.

30/8 hata kabla timu haijaanza kufanya vibaya alisema Man UTD Ina short ya striker mmoja na juzi siku 2 zilizopita amesema January akipatikana striker ambae anaendana na uchezaji wake atasajiliwa. Anafahamu yeye kwamba timu inahitaji striker.

Kuhusu kutumia Hela nyingi mkuu Ni kweli tumetumia lakini Nani anaezitumia? Ni Woodward mwenyewe mtu mwenye zero Football knowledge. LVG anamtaka Robben na Muller analetewa Falcao na Di Maria, Mou anataka perisic yeye anaona sio Hana market anamleta Sanchez, kocha anasema anamtaka Maguire Woodward anakataa anasema una beki wa kutosha, then baada ya mwaka mchezaji huyo huyo unamnunua ghali zaidi. Hela zetu zinasajili Woodward anavyotaka na kuhakikisha wachezaji wanaingizia timu Hela na sio kuziba mapengo ya Timu, mwaka wa 7 huu bila winga wa kulia timu iliokuwa Tajiri duniani, LVG, Mou na hata ole kila mmoja ametaka winga wa kulia hajakuja hata mmoja.

Na ukiachana na Kocha na wachezaji timu yetu pia Ni ya kizamani sana, angalia tunavyoandamwa na Majeruhi, angalia mascout wetu, angalia wataalamu mbalimbali structure ya Timu ipo hivyo, uwanja, academies na infrastructure mbalimbali za mazoezi hata haziwi improved, glazer hajatoa hata shilingi 10 yake mfukoni ku invest man UTD anachojua yeye Ni kuchomoa Hela tu, kila miaka inavyokwenda tunazidi kuwa outdated. AWB kacheza msimu mzima Crystal palace mwaka Jana Ila toka kaja man U kashakuwa Majeruhi mara 2, Huyo Luke Shaw alikuwa anamaliza msimu Soton Ila toka aje man UTd tunajua wenyewe, angalia Jones, martial, Sanchez, Baily, na wengineo Ni coincidence? Wakija tu man U Ni Majeruhi?.
 
Mfumo anaotumia Ole hata Wenger alijaribu kuutumia haukufanya kazi vizuri alikuwa na matokeo ya kubahatisha bahatisha tu kitu pekee kilichokuwa kikimbeba Wenger alikuwa na wachezaji wanaoweza kucheza vizuri katika mfumo huo na EPLhaikuwa na timu nyingi ambazo ni title contender kama hivi sasa.

Asipobadilika na kuwa pragmatic ataonyeshwa mlango wa kutokea mapema sana najaribu kujiuliza sipati jibu kama Ole akifungwa na Liverpool halafu akawa na matokeo mabaya dhidi ya Newcastle sidhani kama ataendelea kuvumiliwa.

Kama hatabadilika Ole sioni kama ataimaliza October akiwa kocha wa United.
Kiongoz ,nadhan kama sijakosea umemfahamu Wenger miaka 3-4 ya mwisho pale Arsenal
 
na game ya jana sikuielewa hiyo var niliona wachezaj wa arsenal wamenawa mpira mara mbili kwenye box na var hawakufwatilia chochote akat najua kuwa epl hakuna sheria ya mpila kufwata mkono ikionekana mtu kashika ni penalt tu spain ndo wanahiyo sheria ya ball to hand
Mkuu sasa hivi acha mbanwe tu, mmeshafaidika sana na maamuzi ya ovyo
 
Mourinho alitwaa EUROPA league na
Ibrahimovic
Rooney
Blind
Mikhtaryan
Carrick
Rojo
Bailly
Etc
Hivi sasa ukomavu wa aina hii haupo Man united
Mkuu embu tuwe critical kidogo kwenye hili swala

Ni kweli Shida yetu sio kocha??..kwanini shida sio kocha??...kama fedha tumetumia sana na improvement imekuwa ni ndogo sana tokea 2013

Mfano Ole amepewa mahitaji yake(hata kama siyo yote)..yeye akaidhinisha kuuzwa kwa Lukaku bila ya replacement na maamuzi mengine..Tunaanza msimu timu inachechemea..Mechi saba za ligi tumeweza kushinda zaidi ya goli moja kwenye mechi moja tu..Then why Kocha asihusike kwenye Perfomance mbaya ya timu??
 
Back
Top Bottom