Mkuu pep anaenda Bayern ndani ya miaka 4 wameingia fainali 3 za Uefa, kaingia fainali na Inter 2010, fainali na Chelsea 2012 mpaka kuja kuchukua na Dortmund, je kwa timu ilioingia fainali 3 ndani ya miaka 4 kuifikisha nusu fainali Ni Mafanikio?
Hapo man city kwenyewe pelegrini kaifikisha nusu fainali ya champions league Pep ameshindwa mpaka leo.
Na ubingwa wa ligi hata Kama angechukua na point trilioni 1 still ni ubingwa, hio Ni Kama sukari tu juu ya keki, na Fergie mara kibao alikuwa na uwezo wa kuvunja rekodi ya point, tumewahi pia kuchukua ubingwa unbeaten man U Kama kumbukumbu zangu zipo sahihi, Ila kawaida ya Fergie akishachukua ubingwa anapanga watoto wa academy mpaka league iishe. Unakuta watoto ndio wanaanza kutoa draw ama kufungwa.
Hapo Barcelona velverde Hana kina xavi na Iniesta Ila nikukumbushe Karibia rekodi zote za Pep kazivunja Enrique kipindi Cha MSN (Messi/suarez/Neymar) kuanzia magoli, ubingwa wa Uefa, Ligi etc) je na Enrique nae Ni kocha Bora zaidi kupata kutokea?
Na Hapa mkuu hatuongelei kupoteza mechi, pep alipigwa 7 na Bayern siwezi tumia hio mechi kumshusha na kusema Ni kocha mbaya, Ila Hapa tunaongelea ili uwe regarded best ever coach unahitaji kufanya extra ordinary things, vitu ambavyo watu walidhani haviwezekani,
Mfano Pep leo hii akiwapa man City Uefa, Atakuwa ameingia kwenye list ya makocha Bora zaidi sababu Atakuwa amefanya Jambo ambalo makocha wote waliokuja city wameshindwa na atapewa status ya ulegend pale.