Mechi ya leo tumecheza vizuri

Tumetengeneza nafasi za kutosha japo tumeshindwa kuzitumia

Naona United iliyoboreka ukilinganisha na ile iliyopigwa na Wolves msimu uliopita

Bado sijaelewa kazi ya VAR, mchezaji wa Wolves alizidi mkono wakati anatoa pasi ya goli

Kukosa penati ni jambo linalovumilika kwa mchezaji katika soka, swali ni je Pogba ameng'ang'ania kupiga penati wakati si mteule wa kocha au?

Hapa naona vidudu mtu wengi wanazengea zengea, lakini amini nakwambia katika big six timu itakayochukua pointi angalau 1 nyumbani kwa Wolves basi hao ni wanaume

By the way, Uwanja uliinama

GGM
2 shot on target ndio nafasi za kutosha ????

Sijaelewa tumeboreka upande upi ukilinganisha na last season game tulizocheza against Wolves
Offensive last season tuli-create more chance kuliko game ya jana
 
Kupunguza ushabiki una maana gani? Tuache kushabikia mpira au kujadili?

Mchango wangu ulitokana na tukio kabla ya kupigwa kwa ile penalty, Rashford ndio alitaka kupiga,Pogba akaenda 'kuililia' na Rashford akamuachia.

Hili la kutokuwa na mpigaji maalumu wa penalty ni jambo jengine linalothibitisha timu ina matatizo. Hata kama wapigaji wanazunguka, huyo Pogba hapaswi kujisogeza kabisa kupiga penalty kwasababu sio mpigaji mzuri.
Acha hizo, how sure are you that Rash asingepoteza hiyo penalty?
 
Dyabala angeweza kuja kwa swap na Lukaku (au kwa hela ya kumuuza Lukaku). Japo mimi sio shabiki wa Dyabala kiivyo

Bruno Fernandez angekubalika na scouts ya Man Utd angekuja, nakumbuka press ya OGS kabla ya mechi ya Chelsea, alisema fedha sio shida, lakini hawakupata wachezaji waliowataka japo hela ilikuwepo

Mfano, tungekuwa tupo champions league Sancho angesajiliwa

Ericksen au Bruno, hakuna namna tungeweza kuwasajili wote, lakini sio kwa sababu ya fedha ila ni kwa sababu ya wote wanacheza position moja
Unataka kuniambia kati ya wachezaji maelfu dunia nzima unasema hujapata unaowataka?

Man Utd ina scouts wengi kuliko timu yeyote ile. Wameshindwa kuona vipaji?

Huu ni uongo wa wazi kabisa.
 
Acha hizo, how sure are you that Rash asingepoteza hiyo penalty?
Hebu acha vituko mkuu,unataka sasa tuanze kujadili madhanio? Kwamba hata angepiga Rashford au Martial wangekosa kama Pogba? Hiyo kazi sifanyi mimi.

Hata hivyo,Rashford ni bora zaidi kwa hiyo kazi hasa ukiangalia mikwaju aliyowahi kupiga na ilikuwa na presha kiasi gani.

Nipe idadi ya penalty alizowahi kukosa Rashford nami nitakupa alizokosa Pogba.


 
2 shot on target ndio nafasi za kutosha ????

Sijaelewa tumeboreka upande upi ukilinganisha na last season game tulizocheza against Wolves
Offensive last season tuli-create more chance kuliko game ya jana
Hivi kutengeneza nafasi ni sawa na shots on target. Mnaweza mkatengeneza nafasi hata 10 lakini zote zikawa shots off target. Kimsingi tumetengeneza nafasi nyingi jana

Pili una uhakika jana United alipiga shots on target 2? Kwa haraka haraka kuna goli la Martial, Penati ya Pogba, shuti la Shaw..... Zipo 3 jumla. Nikienda Google nadhani kuna mifano mingi.

Unauliza kuhusu improvement kati mwaka jana na mechi ya jana. Kwanza kumiliki tu tuna position kubwa kuliko mwaka jana, mwaka jana tumepigwa kwa kuzidiwa, mwaka huu tume draw kwa kuwazidi sana tu

Kama hujaona improvement nadhani mechi uliyokuwa unaangalia wewe na mimi ni tofauti
 
Mkuu Kuna watu sio, wastaarabu humu

Kwa hiyo inabidi kwenda nao hivyo hivyo

Jana ilikuwa siku ya bahati kwa Wolves, lakini tuliwazidi kila kitu

Hao Leicester mkuu ni wababe wako mkuu, naona ulijipiga ban kama kawaida yako
Sawa mkuu ni kweli muna timu nzuri tu cjui Ole anakwamia wap sasa. Pangeni kikosi cha maana mumfumue Liverpool, Man city ..Arsenal najua ni uhakika lazima mushinde ...

Come one United..

Kila la kheri Chelsea
 
Mkuu naamini utakuwa umecheza mpira kwa kiwango chetu hiki cha makaratasi

Hivi unamlaumu vipi Lingard kukosa goli lile, wakati ilipigwa pasi halafu yule beki Wily Boly akaigusa kubadili mpira welekeo? Sometime tuseme ukweli, kumlaumu dogo kwenye ile nafasi ni kumuonea

Kwenye bulid up ya goli/penati dhidi ya Chelsea, chanzo alikuwa Lingard. Kwenye build up ya goli la jana pia alihusika

Wakati huo huo sioni watu wakimlaumu Martial kwa kupoteza nafasi ile ya kwanza ambapo krosi ilipigwa na Rashy.

Kuna mpira mwingine Martial aliuacha nyuma (japo mimi simlaumu, najua sometime inatokea kwenye soka) na ilikuwa ni nafasi ya goli kabisa. Ule mpira angeuacha Lingard au Lukaku enzi hizo ungesikia oooh first touch mbovu

Umakini tu bado ule mpira haukuwa mbali nae hata ukiangalia
 
Mkuu umehesabu mipira aliyopoteza Pogba?

Lingard ni kama Ji Sung Park enzi hizo au Darren Fletcher, unsung heroes

Pia Pogba alicheza vizuri, lakini kimchango dogo Lingard alicheza sana

Scot pia alicheza vizuri mkuu

Una mapenzi mabaya mkuu yaani lingard aungie kwenye hao miamba?
 
Dyabala angeweza kuja kwa swap na Lukaku (au kwa hela ya kumuuza Lukaku). Japo mimi sio shabiki wa Dyabala kiivyo

Bruno Fernandez angekubalika na scouts ya Man Utd angekuja, nakumbuka press ya OGS kabla ya mechi ya Chelsea, alisema fedha sio shida, lakini hawakupata wachezaji waliowataka japo hela ilikuwepo

Mfano, tungekuwa tupo champions league Sancho angesajiliwa

Ericksen au Bruno, hakuna namna tungeweza kuwasajili wote, lakini sio kwa sababu ya fedha ila ni kwa sababu ya wote wanacheza position moja

Ni kawaida kwa scout wa hii timu kubet kisha tunaambulia wakina sanchez na darmian kaangalie kule yule dogo João Félix Sequeira anachofanya atletico madrid sisi tulianza kubishana bei mwisho dogo akaona mapuuzi kaenda spain
 
Mashabiki acha kulalamika. Man U iliyocheza jana ndo niliyokuwa nataka huoni hata ollachuga OC first half alikuwa anachungulia yaani Kazi kazi, wolves shots on target chache sana walipata bahati maana ule mpira ungekuwa usawa wa kuingia bila kugonga mwamba De gea angefanya yake.


Inshu ya pogba kumbuka penati haina ubabe!


Kwangu mimi niliona timu iko poaa kazi kazi dk 90. Ila huyu Shaw Bana angetuliza na kufumua ili tupate usingizi vizuri.


I was happy na mchomoko wa David James, Kazi kazi Wan Bissaka. Chuma Lindelof na Maguire safi sana yaani hawaingii kupitia katikati bali pembeni ila mara nyingi upande wa wan Bissaka mpinzani hafui dafu.


Hata kama tumedroo i am happy maana nilichoka kuona magarasa ya young, smallling, Jones yanaleta mpira golini bila sababu.


Kuhusu martial naona dogo anabadilika taratibu goli safi. Kukosa nafasi duh mpira unadunda.


All in all! Mpira uko poah tukiendeleza soka hilo hilo daily huku forward ikisahihisha makosa Guardiola na Klopp watakuwa na presha.



GGMu
Sasa mkuu Wolves mimi nitapiga nje ndani ..uhakika wa kubeba kama sio point sita basi ni nne ..kama uyo umemshindwa ukikutana na Leicester ci mutapata tabu sana. Japo Muna timu nzuri ya kuweza kuifunga Liverpool au hata Man city goli nyingi tu achilia mali uhakika wa kumfunga arsenal ..lakini naona Ole anakwama ..yani bado hajui fist XI yake ni ipi. Na hii itampa tabu sana..

Kila la kheri Chelsea
 
Unataka kuniambia kati ya wachezaji maelfu dunia nzima unasema hujapata unaowataka?

Man Utd ina scouts wengi kuliko timu yeyote ile. Wameshindwa kuona vipaji?

Huu ni uongo wa wazi kabisa.
Man Utd haichukui mchezaji yoyote katika maelfu, ingekuwa hivyo tungekuwa tuna kiwango cha mtibwa..... Na utd isingekuwa United. Not all players can be United players

Pili OGS ana vigezo vyake anavyovitaka kwa mchezaji kwa hiyo sio kila mchezaji atakayekuwa identified atasajiliwa. Huyo Bruno Fernandez tumemscout kwa msimu mzima wa mwaka jana lakini hatukumchukua (japo mimi pia namkubali sana). Unaambiwa kwa structure ya sasa pale United katika usajili kuna scouts, kuna Phelan+OGS, kuna mtu anaitwa Mat Judge na Murtough (hapa kuna Head of Corporate Development na Chief Scout na negotiator mkuu) hawa wakiafiki kununua mchezaji wanampelekea Ed ili aandike check.

Tatu United wamebadili sera kwenye kusajili wachezaji. United imepigwa kwa wachezaji wengi, kuna Sanchez, Fred (haendani na bei aliyonunuliwa)na wengine wengi, hivyo hawataki kurudia makosa ndio maana pengine hawajawaona hao maelfu unaowataja. Ukishaumwa na nyoka, jani likitingishika tu lazima uogope.

Pia sio kwamba United haoni wachezaji. Kati ya wachezaji waliokuwa wanawataka ni Sancho ambaye tumeshindwa kumpata sababu ya kutoshiriki Champions League.

Tulimtaka Varane lakini alikuwa kwenye category ya impossible targets. Tulimtaka Koullibally, Napoli wakahitaji £150milion. Scout walimuona Longstaff lakini Newcastle wakataka £50milion, je tungemnunua hivyo hivyo? Nakubali United kuna sehemu tunafeli kwenye transfers, lakini sometime nawaelewa wanavyokuwa makini ili wasikurupuke kama tulivyokurupuka huko nyuma.

Kwa hiyo kusema United hawaoni wachezaji ni kujidanganya. Akina Bailly, Lindelof, Daniel James, Martial, Pogba (alivyokuja academy), na hawa watoto wote unaowaona leo pale United ni kazi ya scouts
 
Nimefuatilia nimegundua upo sahihi,

Lakini kwa miaka mingi ya kuangalia soka nimeona mchezaji akiadhibiwa kama yupo offside kwa kuwa tu kamkono kamezidi

Marefa wanaandamwa na Vitu viwili:

1) Utashi/Mapenzi/Chuki
2) Kukosea/Kutoona tukio kwa usahihi

• Mfano
i) Chuki
Kuna refa anaitwa Michael Oliver:
Huyu ni kijana mdogo tu lakini ni Refa ambaye anaichukia Chelsea na akichezesha game ya Chelsea lazima aifungishe goli au awakoseshe goli halali.

Kuna marefa hawa
1) Craig Pawson
2) Mike Deen
3) Anthony Taylor
4) Lee mason
5) Martin Atkinson
6) John Moss

Hao ni marefa walioichukia Liverpool Kupita maelezo yani wakiichezesha game yake lazima wataikamua Liverpool.

ii) Mapenzi
1) Michael Oliver: Ni refa anayeipendelea Liverpool kupita kiasi na akichezesha lazima atafanya maamuzi ya Kutufavour tu. Lakini sijui ni mshabiki wa timu gani but probably huenda akawa ni mshabiki wa Spurs.

2) Anthony Taylor: Ni mnazi mkubwa wa Manchester United kiasi ya kwamba Akichezesha game ya Man United anawafavour kama ilivyokuwa kwa Howard Webb.

iii) Kutoona tukio kwa usahihi:
Ni matukio mengi ya Penalties za utata (Za kudive) au mchezaji kushika mpira kwa mkono na refa asione tukio hilo.

iv) Utashi:
Ni kama lile tukio la John Moss kwapa Spurs Penalty 2 dhidi ya Liverpool katika msimu wa 2017/18 ambapo hazikuwa sahihi (Diving) kutokana na yeye kulazimisha kutumia TV iliyopo kwa Kamisaa (Fourth official) kutazama tukio la Penalty ya pili wakati VAR ilikuwa haitumiki EPL.

Hayo ni baadhi ya Madhaifu ya Marefa kwahiyo usishangae Refa kumuadhibu mchezaji aliyezidi Mkono na akamuacha aliyezidi Mguu.

Mimi sifuatilii Wachezaji tu bali hupenda Sana pia Kufuatilia Marefa na tabia zao
 
Ni sheria ya offside mda mrefu tu.
Sasa kama Unataka kujifunza jifunze ,ila kama unaleta ushabiki ambao hautaki kujifunza Sawa pia.

Ila hapa tuko kujifunza
Labda mimi ndio nikisaidie

Kiungo chochote cha mwili kikizidi na mchezaji akafunga goli, hiyo itahesabiwa kuwa ni off side position

Labda hiyo ya kiungo kinaweza kufunga ni sheria mpya ya offside ambayo imeanza kutumika msimu huu
 
Ni kawaida kwa scout wa hii timu kubet kisha tunaambulia wakina sanchez na darmian kaangalie kule yule dogo João Félix Sequeira anachofanya atletico madrid sisi tulianza kubishana bei mwisho dogo akaona mapuuzi kaenda spain
Mkuu kwa sehemu upo sahihi lakini kwa sehemu haupo sahihi

Kutokana umahiri wa dogo kila timu ingependa kuwa naye. Lakini si kwamba dogo alikuwa ni target kuu ya United

Target ilikuwa beki ya Kati, ya kushoto, midfielder wa kati, right winger na probably striker kutokana na Rom kutaka kuondoka. Pia kulikuwa na mpango wa kumleta left back japo sio kipaumbele kikubwa.

Sasa Joao hakuwa kipaumbele kwani he is neither a striker nor a right winger. Kwahiyo kwa namba yake hatukuwa mtu tunayemhitaji saaaana. HAPA NAONGELEA MAHITAJI.

Lakini pia tukumbuke, wakati tunasema tungemchukua Joao mwenye miaka 20/21 tayari na Angel Gomes na Greenwood ambao nao wanaweza kucheza namba za ushambukiaji mbele wanakuja kwa kasi. Je tungemleta Joao halafu hawa madogo waende wapi?

Pia Joao sio premier League proven, na kwa umri wake na bei ambayo aliyokuwa anauzwa (£107m)na hali ya United kwa sasa kutokuwa stable ni ngumu kumpa majukumu ya kubeba United mgongoni na akaiweza. Pengine angekuwa flop of the season. Tusi assume kwa kuwa kule anakinukisha basi na physical league kama Uingereza pia angekinukisha
 
Back
Top Bottom