Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Hatuwezi kushinda kila mechi mkuu. Hata hao City na Liver wanafungika

Mkuu tunazungumiza makosa tunayofanya ktk post zangu hamna nipopost nimechukizwa na ile drooo sema ningechukia kama tungecheza hovyo nimependa uchezaj wa jana nimekasirishwa na martial kawekwa central striker anacheza kiulegevu tu anapoteza mipira first touch hakuna hapo tu
 
Cha kukusaidia hapo "" kwamba mkono ulizidi Wakati anatoa pasi ya goli""
Offside Inakuwa pale tu kiungo ambacho kinaweza kufunga kikizidi.
Sasa mkono Hauwezi kufunga ndo mana haikuwa offside.
So mkono unapozidi sio offside.
Labda mimi ndio nikisaidie

Kiungo chochote cha mwili kikizidi na mchezaji akafunga goli, hiyo itahesabiwa kuwa ni off side position

Labda hiyo ya kiungo kinaweza kufunga ni sheria mpya ya offside ambayo imeanza kutumika msimu huu
 
Muda sio mrefu Maji na Mafuta vitaanza kujitenga,kila kimoja kitarudi mahali pake.
Wewe mkuu umeanza na Norwich na Southampton una points 6

Mimi nimeanza na Chelsea iliyokupa tabu Super Cup na Wolves nyumbani kwao

Huwezi ona tofauti hapo?
 
Katika sheria za offside kuzidi mkono sio offside but viungo vengine vyote (Kichwa, Mguu, tumbo, mgongo n.k.) vikizidi ni offside.
Duh...... Hii ni sheria iliyobereshwa ambayo imeanza kutumika msimu huu Mkuuu
 
unasemaje?
 
Kimpira uko sahihi kabisa, ila kiushabiki hatuangalii hizo. Imagine baada kumfunga Chelsea maneno tuliyoambiwa mtaani.

Leo kimya, sioni status za GGMU WhatsApp.
Yeah mm siko upande wa kishabiki zaid. Niko upande wa mpira zaidi. Ushabiki ni kama siasa so sija base sana huko
 
timu yako haina hela ya kununa hao wachezahi kwa mpigo
 
Muda flani unatamani timu ifungwe mfululizo ili kocha na wamiliki angalau washtuke kuwa kuna mahala hapako sawa. Lakini hii siyo sahihi ni timu unayoipenda sana...ikizingua sana ndo mambo yatazidi kuwa magumu.
Kwa kweli kama hakuna nidhamu kwa timu ni bure kabisa, na pogba akiendelea kuwepo atatuchomesha sana, jombaa ana kipaji lakini hajitumi, mipira inapotea kizembe halafu bro hana muda vile. Sijui ndo anafanya mgomo baridi.
Mbona tumewahi kuwa na kiungo ya fletcher na carrick na tuliendelea kuwepo, rud van, beckham, tevez, ronaldo wote waliondoka..why huyu lakini?
mzee fergie alionaga mbali sana kumwachia pogba aende juventus. Aliona roho ya kiburi na dharau iliyo ndani yake. Mwenyewe alishasema anataka kuondoka, hapendi kuwa hapo na yupo tayari hata mshahara upunguzwe ili mradi tu asiwe man united..mtu wa hivi eti bado ndo tunamng'ang'ania.
Kweli kabisa tulishindwa kusajili angalau viuongo wawili wakatusaidia.
 
Ni lini ole alisema penalti zinapigwa na rashford?

Navyojua mpigaji penalti wa man u ni pogba na katika interview ya mechi ya chelsea rash alisema wapiga penalti wana rotate ili kuepusha timu pinzani kukariri mpiga penalti mmoja na ndio maana akapewa ile penalti ya chelsea.

Sometimes tupunguze ushabiki jamani.
 
Hivi Mtu anaposema "Tungepata kuwanunua Bruno Fernandez, Eriksen na Dyabala" ambapo tayari ameshasajiliwa Bissaka na Maguire huwa anazungumzia mpira wa Ulaya au wa Bongo? Hebu afanye majumuisho ya Kimakisio ya hela za hao wachezaji.
 
Kasome kwa umakini sio kiungo chochote, bali kiungo kinachoweza kufunga goli halali hivyo kama ni mkono tu (not including bega) sio offside. Nasema hivyo kama refa mbobezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…