Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Asante, walau kuna mtu ameelewa what i am talking about, wacha Glazer na woodward waendelee na huu upuuzi, hawa wahumu nao watakuja kuelewa what am talking about.

We can laugh about City, but in reality we are jelous of them kwa sababu wana mtu ambae ame invest heavily in football sisi tuna mtu ambae haweki investment but is ripping from our club.

Sasa ivi Fans tunaishia kuzungumzia historia, mambo ambayo yalikuwa yanafanywa na fans wa liverpool.

Najaribu kuwaelewesha kuwa shida ya City ni kwamba makinda hawana game time ndio maana Academy ya United inaonekana inazalisha sana, mfano, solkjear kajipanga na watoto wa academy kibao kuwachezesha, wakati city wanao vijana wa academy lakini hawana time ya kuwapa uwanjani. City wanataka wachezaji waliokwisha iva saiv, they are on the road to build an empire, na guardiola akiendelea kukaa pale, tutashuhudia dream yao ikifanikiwa.

Nakushukuru kuwatajia wachezaji waliotoka City Academy.....

They will realize soon, and i hope it will not be too late!

Watu wanafikiri labda tunataka kuona club ikichukua ubingwa tu, no, tunataka kuona ushindani, kuiona timu ina fight for title hata wakikosa, unajua kuwa dah vijana wamepiga kazi hawa ku give up.

Mtu anakwambia Pogba karudi MUFC kwa mapenzi yake.... 😀 Halafu anatoa statement kuwa anataka challenge somewhere else!!!

Wenye mapenzi na MUFC walibaki hata baada ya matusi ya Babu Fergie....
 
Kwa hiyo wa Man United unataka wa tangu 2013

Lakini wa Man City unataja wa tangu Adam na Eva
 
Mkuu hapo kuna mambo 2,unaweza kununua mchezaji kuziba pengo ambalo lilikuwepo lakini je hiyo inakuwa ni upgrade au ni kuziba pengo tu ilimradi?

Kwa mfano Man United tulikuwa tunahitaji beki wa kati, je tungemchukua David Luiz ungejihisi comfortable kama tulivyomchukua Maquire? After all David Luiz sio addition ila ni replacement ya Koa scienly ambaye akiwa fit ni mzuri kuliko Luiz

Kwa Tierney nimewapongeza, japo sio premier League proven. Lakini sidhani kama amemzidi kiwango sana yule baunsa wao au Monreal.

Kwa Pepe ndio wamelamba dume for sure
 
Mkuu huwezi kuwa na sera ya Galacticos halafu ukaweza ku apply na sera ya kutumia wachezaji kutoka academy wakang'ara

Mfano Chong atang'ara vipi ukimletea Pepe (japo mimi pia nilitamani aje), Greenwood atapata vipi playing time ukimletea Lukaku mwingine, Gomes atang'ara vipi ukimletea Griezeman

Diego Dalot mwenyewe tulikuwa hatutaki aletewe Wan Bissaka kwa sababu hizo hizo

Angalia Madrid kwa miaka 10 hii, kuna makinda hata 5 wametokea academy yao na sasa wanang'ara duniani? Labda unikumbushe.

Ndio maana nasema huwezi kuwa na vyote viwili kwa wakati mmoja, kusaini wachezaji wakubwa 5 au 6 kwa wakati mmoja na wakati huo huo kuendeleza vipaji kutoka academy.

Mimi binafsi sikumbuki ni lini mara ya mwisho SAF alisajili wachezaji 4 wakubwa kwa mkupuo. Akijitahidi sana ni wawili halafu anaongezea na potential mmoja au wawili kisha maisha yanaendelea.
 
kwenye comment yangu ulioinukuu nimezungumzia kosa walilolifanya arsenal la kununua mlinzi wa kati kwa bei kubwa baadae wakakubali kipengele cha kumruhusu abaki klabuni kwake kwa mkopo wa mwaka mmoja, jeuri kama hiyo walipaswa wafanye klabu kama vile juventus iliobarikiwa utajiri wa mabeki wa kati wenye viwango na si arsenal inayoadhibiwa kila msimu kwa kukosa walinzi mahiri wa katikati.

kuhusu tierney sijawahi kumuona lakini ujio wake kama ataonyesha kiwango itakuwa ndio chanzo cha kumrudisha kolasinac eneo la mlinzi wa kati na si kuendelea kucheza upande wa kushoto.

unamuonaje dani ceballos?
 
mkuu kama ni hivyo basi hakuna faida ya klabu kufanya usajili wa wachezaji kama ishu ni kuhofia young players kutoka academy hawatopata game time ya kutosha, hata huyo maguire kwa mujibu wa hoja yako ujio wake utasababisha tuanzebe na vijana wengineo kutoka academy watumie muda mwingi kukaa benchi au kucheza mechi za under 23.

nilichokuwa nakihitaji mimi ni kuona kwanza tunaziba madhaifu yetu kwa kufanya usajili wa sehemu zote zenye ufa baadae ndio tuwape nafasi vijana ila alichokifanya OGS msimu huu ni kuwabebesha mzigo wa misumari vijana wadogo wasiokuwa na uzoefu wa mapambano kwa kuwategemea wawe wazibaji wakubwa wa nyufa zetu.

nitatoa mfano mwengine wa manchester city tumeona timu yao jinsi ilivyoimarika kila eneo kiasi ambacho hata ikitokezea david silva amewekwa benchi nafasi yake inazibwa vizuri na kijana phil Foden kutoka academy.

kwa nini phil foden anacheza vizuri?
jibu ni rahisi tu ni kwamba pindi akiwa uwanjani hujikuta amezungukwa na mafundi wa mpira kila pembe jambo ambalo humpunguzia presha ya kuwa tegemeo kwenye mechi husika.

lakini ukija kwetu sisi unapomuanzisha angel gomez au greenwood kwenye kikosi kinachoundwa na dead players mfano wa ashley young, fred,jones, perreira, matic na wengineo wanajikuta wanabeba mzigo mkubwa sana wa matumaini ya kuwa wabebaji wakubwa wa timu kimatokeo.

nikatoa mfano wa barcelona nyakati ambazo kwa muda tofauti wanawakuza kisoka sergio bosquets, messi, gerrard pique,pedro, sergio roberto, thiago alcantara, cristian tello, bojan krkik na wengineo hawakuwabebesha majukumu sana kwa sababu walikuwepo wachezaji watakaowafanya ile presha ya kuibeba timu isiwepo kwenye mabega yao.
yupo henry, etoo, gaucho, deco,guily, abidal, toure, puyol, marquiz,xavi, iniesta, david villa, zambrotta, dani alves,alba na wengineo kwa nini usiufarihie mpira wako?

kama ni young players kwa nini usiufurahie mpira wako kwenye timu inayozungukwa na kevin debruyne, gundogan,aguero, sane, sterling, silva double, concelo, mendy,otamendi, walker, aguero?

kama ni young player kwa nini usiufurahie mpira wako kwenye timu inayoundwa na roy keane, rooney, scholes, giggs, ferdinad, vidic, evra, nistelrooy na wengineo?
 
Unadiriki kuitaja Chelsea kama giant msimu huu😂

Kwanza nianze kwa kusema nashukuru kama umejua hizi game saba za mwanzo hakuna atakae pona wakiwemo chelsea,

Pili nikukumbushe tuu baada ya mechi saba hatutabadilisha kikosi, moto ni ule ule

Tukutane kesho Ollachuga Oc
 
Yani mashabiki wako bize wanalialia tuu kama vitoto vya ndege,
Nani amewaambia tunataka kufika ilipo Liverpool?

Lengo ni kufanya vizuri na kushinda mataji, wimbi la mashabiki wa timu pinzani kuja kulinganisha timu zao na timu yetu limechukua akili za wenzetu kiasi kwamba na sisi tuko bize tunalinganisha timu yetu na Liverpool, Barcelona, madrid, man city

Tunasahau kama kuna sterling wa man city hawezi kuwepo na wa man u, kwamba wacheze mchezo unaofanana, kila mtu atumie raslimali alizo nazo, mwisho wa siku tukumbuke panga na shoka vyote vina ncha kali na vinaweza kukata mwanzi ni suala la utumiaji tuu.

Kwani goli akifunga greenwood mwenye miaka 17 na akifunga sterling si bado ni goli?
 
Kuhusu Tuanzebe ipo tofauti na context ninayoongelea mimi. Kwa kuwa ameleta mtu mwenye quality na wanaondoka watu wenye experience lakini bado hawajawa na quality Man Utd anayoitaka

Tuanzebe bado hajawa tayari, lakini lazima atapata game time. Na ili kuhakikisha anapata game time ndio maana Man Utd Baada ya kumleta Maquire sasa hivi kwa udi na uvumba wamemuweka sokoni Rojo na Smalling (japo mimi nilitaka iwe Rojo na Jones) sokoni. Yote hiyo ni kumpa nafasi Tuanzebe

Lakini hii ya kutaka kununua timu nzima huwezi saidia vijana wanaokuja. Ndio maana hujawahi kuona Barca wananunua karibu galactico nusu timu
 
Kama huyo kocha atakuwa free.

Makocha wa maana wote wana timu. Labda ummchomoe kwenye hiyo timu.
 
Rahisi kuongea kama konda wa kike.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…