Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Lakini hii ya kutaka kununua timu nzima huwezi saidia vijana wanaokuja. Ndio maana hujawahi kuona Barca wananunua karibu galactico nusu timu
mkuu sidhani kama kuna sehemu nimeandika maneno ya kutaka klabu inunue nusu ya timu nzima ya galacticos kama ulivyoandika hapo juu, bali nilichokihitaji mimi kwa nguvu yetu ya ushawishi wa kifedha na scouting waliojaa kila pembe ya dunia kama anavyojisifia ed woodward basi tuzibe nyufa zetu zinazotuandama kwenye jengo letu kama walivyofanya matajiri wengine mfano real madrid.

ila tulichokifanya ni kujificha kwenye kivuli cha academy pamoja na kuwatumia wachezaji wale wale waliofeli.

upande upi upo sahihi kimtazamo na upi haupo sahihi utatambulikana baada ya ligi kuanza rasmi kwa upande wa manchester united.
tutaianza rasmi ligi kuu ya uingereza wiki ijayo tutakapocheza na wolverhampton, ndivyo ninavyojiaminisha​
 
My tommorow starting lineup

De Gea

Bissaka Lindelof Maguire Shaw

Perreira McTominay Pogba

Greenwood Martial Rashford
Kikosi hiki umekipatia pale central. Akifanya Ole ni mwake kabisa. Ila kwenye flangs aanze Dany badala ya Mason
 
Tuko pamoja mkuu, niliwahi kushabikia Man U iliyokuwa ikimtegemea Striker Chadwick sembuse hii ya Rashford na Martial?
huyo luke chadwick unayemzungumzia wewe kutoka mwaka 1999 hadi mwaka 2004 alicheza mechi 25 tu za kikosi cha kwanza na alifunga magoli mawili.

unaposema man united walikuwa wanamtegemea mchezaji aliyecheza mechi 25 tu kwa miaka mitano huoni kuwa unatuongopea?
andy cole + dwight yorke + sherringham + solskjaer = ndio walikuwa washambuliaji wa kila siku wa bwana fergie kabla hajasajiliwa van nistelrooy mwaka 2001.​
 
Screenshot_20190810-174244~2.jpeg
 
Aman iwe nanyi wapendwa

Man u ndo inaenda kuwa pombe ya ngoman musimu

Kila mtu atakuwa anajichotea tu

Saiz wamejificha kwenye mgongo wa Chelsea


LONDON BOY
Biera boy chelsea hamjasajili. Mmeuza bek.. mmeuza mshambuliaj ambae icon . Halaf mnawaita man u wana hali mbaya...?
Wale watoto wenu watawaaibisha
 
Utajuta kuzaliwa kwa mpira utaopigiwa kesho na watoto wa darajan
Biera boy chelsea hamjasajili. Mmeuza bek.. mmeuza mshambuliaj ambae icon . Halaf mnawaita man u wana hali mbaya...?
Wale watoto wenu watawaaibisha
 
Kwa lingard labda. Maana ni wa hovyo sana..
Ndio maana hata kikos cha kwanza hana number.

Ila martial sidhani. Kipind amekuja alikuwa akicheza kama striker.. na alikuwa effective akiwa CF.. kiwango kilishuka aliporudihwa winga ya kushoto.

Martial bado ana kitu na umri unaruhusu. Ambao siwaamini ni lingard na rushford. Hawa hamna kitu
Ngoja tuone kesho masho ata fanya nini
 
Nawasalimu wakuu. Na mimi naomba nitoe Mtazamo wangu kuhusu timu yetu kabla ligi haijaanza.

Kwanza nadiriki kusema tumefanya usajili nzuri(kiasi) kutokana na matakwa ya kocha japo hatujafikia hatua tuliyo penda(wengi wetu).
Usajili wa Wan na HM, kurudi kwa Mensah na Tuamzabe utatusaidia kuimarisha defense yetu ambayo kwa muda mrefu ilikuwa majanga. Kwa upande wa ulinzi tume improve kutoka tulipo Kuwa misimu kadhaa iliyo pita. Tuombe MUNGU injuries zikae mbali na wachezaji wetu.

Kati kati bado tuna tatizo. Kwa Kuwa kuna watu wamepungua na ilibidi tutafute replacement, ila kwakuwa Malengo yetu sio kugombea ubingwa(ukweli mchungu) na basi tuwape muda watoto ambao wako talented kama Mctomminay,Perreira na back up ya (Tuanzabe na Mensah) + Fred+Pogba+Matic(japo amechoka ila hakuna kijiji kisicho na wazee) huku tukifanya addition ya kiungo katika madirisha mawili yajayo(January+next summer).

Japo binafsi nilitamani sana kama tunge mpata BF.

Kuhusu wings, naona tume improve,hasa kutokana na uwepo wa WB upande wa kulia ambako kulikuwa na tatizo sugu. Naamini AW+James/Dalot tutakuwa na Uwezo wa kupeleka mashambulizi kutokea kulia pia. Kushoto ndio ilikuwa strength yetu na haijavurugika, huku tukiomba Shaw asiende wodini tena.

Upande wa ushambuliaji. Kwa mtazamo wangu naona Ole amefanya uamuzi sahihi kumuacha Lukaku na kuto sajili mtu. Kwa nini nasema amefanya kitu sahihi?

Kwanza Ole alikuwa haamini kama Lukaku ana fiti Kwenye profile yake(hii haimaanishi Kuwa Lukaku ni mbovu na sita shangaa kama atakiwasha huko aliko kwenda). Ni jambo la kawaida hasa Kwenye Mpira wa sasa.

Lakini pia ukiangalia tetesi Nyingi za washambuliaji tulio Kuwa tuna husishwa nao hawana tofauti sana kiuchezaji na Lukaku. Na kwa nilivyo muelewa Ole hataki timu iwe na mshambuliaji mmoja wa ku stick mbele, anahitaji wachezaji wanyumbulikaji, na hii itasaidia Kuwa na vyanzo vingi Vya magoli. Kutoka kati kwenda mbele. Rashford,Martial,Sanchez,green wana fit Kwenye hiyo profile. Kwa hiyo hakukuwa na haja ya kuongeza MTU kama hawa watu wapo na
Note: Malengo yetu sio kugombea ubingwa.

Kwangu Mimi kitu alicho feli OLE ni kuidhinisha Jones,Smalling,Young,Rojo kupewa mikataba mipya wakati wangeweza kuondoka na kusiwe na madhara.

Mwisho niwashauri mashabiki wenzangu Kuwa msimu huu inabidi tushushe matazamio yetu(lower expectations) na tujiandae kwa Matokeo yoyote. Njia rahisi ya kufuzu uefa ni kushinda Europa.
 
Back
Top Bottom