Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mimi nadhani tuwape nafasi makinda wanaweza kutusogeza mbele kidogo kuliko kutegemea wachezaji kama Dyabala ambao hawako tayari kupigania team.

Ole kajitahidi kusajili sehemu zenye mapungufu hasa eneo la ulinzi,bado kiungo na mshambuliaji wa kulia.Pia tukumbuke usajili ulikuwa mgumu kweli kweli hasa bei za wachezaji zipo juu sana.

Tumefanikiwa kuziba pengo mlinzi wa pembeni kulia na baki wa kati,naamini Fred,Pereira,Fosu Mensah na McTominary wana uwezo wa kuziba pengo la Hereira na Manywele.Sehemu pekee bado tutaumiza kichwa ni mshambuliaji wa kulia.

Lukaku sidhani kama kaacha pengo kubwa kinda Mason ana uwezo mkubwa kuliko kubwajinga Lukaku.Sijui kwanini mpaka sasa naamini Sanchez anaweza kutusaidia msimu huu.

Tupe team yetu moyo badala ya kulalama.

Sipingani na wewe mkuu shida inakuja unaachaje wachezaj wazur wakat huna replacement mfano lukaku na harrrera?

Tunajenga timu watu muhimu tunaacha wasepe binafsi naona hapo kidogo pana upungufu
 
Sidhan kama lingard anategemewa. Namba tisa atarudishwa martial
Kama rashford,+lingard ndio fowad mnazozitegemea. Lakini hakuna msimu waliowahi kufikisha hata goli13 kwenye ligi. HAKUNA! sasa kama hamna fowadi hapo mnategemea nini
 
Mkuu I feel your pain, but I also try to understand the fact

Kwa upande wa beki ni ukweli usiopingika tumejiimarisha msimu huu, ni kweli tulitamani Shaw awe na compitition na back up pindi akiumia lakini huwezi kusajili timu nzima katika msimu mmoja.

Back four ya Wan Bissaka/Dalot, Tuanzebe/Lindelof, Maguire, na Shaw sio mbaya kama baadhi ya watu wanavyotaka kutuaminisha. Ni timu ngapi zenye subs za beki kama Smalling, Bailly na Rojo aliye mzima bila majeraha? Ni chache sana.

Lingard. Kabla hatujamuhukumu, tunapaswa kujiuliza kwanini pale Three Lions lazima apate namba piga uwa. Hiyo ni ishara kuwa ana kitu flani. Lakini nikukumbushe kwa United hana uhakika wa namba.

Tatizo kwa usajili wa msimu huu ninaloliona ni kuongeza angalau mid fielders wawili, defensive 1 na creative 1. Pia tulipaswa ku replace magoli ya Lukaku kwani Rashford hana uwezo, ila Sanchez mzima anaweza kutufungia magoli kama false number 9 na Martial akiaminiwa (kama ilivyokuwa msimu wake wa kwanza United) anaweza kufunga magoli. Namuunga mkono Lukaku kuondoa, United fans hatukumuonesha upendo kabisa.

Kwa mtazamo wangu hata Lukaku angebaki bado asingetusaidia kwani kocha hampi nafasi. Hivyo ni bora tu alivyoondoka. Angebaki ni wale watoto wangeendelea kuanza, ameondoka bado ni hao watoto wataendelea kupata namba, kwa hiyo mbadala au bila mbadala ninaona ni yale yale

Kuna watu walitamani tuwaondoe wachezaji wote tusiowataka. Rojo, Jones, Lingard, Sanchez, Smalling, Young, Mata, Lukaku, Matic na wengine,wote waondoke. Je tungesafisha timu nzima?Je tungepata wanunuzi kwa bei tunayotaka? Kumbuka mashabiki huwa tunataka quick fix, je unajua wamiliki nao wanataka hela? Hata ungekuwa wewe ndio mmiliki ungewaondoa tu ili uwaondoe bila kujali hasara?

Je kwa soko la sasa hao wachezaji wote unawa replace vipi? Muda unao wa kuwa replace dirisha lenyewe ni fupi, tuchukulie una muda. Kwa soko la sasa una hela ya kuwa replace hao wachezaji?

Utasema hela ya kuwauza akina Lingard, sasa ukiwa desperate utawauza kwa hasara je hela ya kuwauza wote hao utapata hela ya kununua hata wachezaji wawili wenye kiwango ukitakacho? Na kumbuka hapa utatakiwa ununue wachezaji wa kujaza squad sio unaondoa 8 unaleta wawili au watatu.

Kuna maswali mengi kuliko majibu. Nakubaliana na wewe kuna shida kwenye hierarchy ya United, lakini kuna mambo tunayakuza sana.

Mfano, kuna baadhi yetu tunamlaumu OGS kwenye usajili, je ni kweli OGS hakumtaka BF au hakumtaka winger wa kulia. Tunapenda sana kulaumu.

Ed Woodward ni shida, hilo halina ubishi, Glazers ni shida, hilo halina ubishi, Board ni shida hilo halina ubishi. Wote hao wanaangaalia zaidi commercial aspect pale klabuni kuliko football aspect.

Angalau tukipata Sporting Director tunaweza kufanya vizuri zaidi kwenye madirisha ya usajili yajayo.

Nakuelewa sana mkuu kwa hii timu yetu toka sir alex awepo na kasepa bado hatujapata DM na linafahamika lakin tunarudia kosa lilelile wakina jones na smalling waliweza kuwa poa kwa kuwa wakina scholes walizuia haya matatizo sasa hawapo kupo open uje striker mchezaj wamwisho kuwa nae van persie toka hapo hamna kitu

Dirisha lilifunguliwa mwez wa 5 angalau tungafanyia kazi hizo sehem tatu muhimu sana zingine ni addition tu
 
Hao watu wawili ndio kelele zote hizi? Kwa herrera i am conerned. Lakin lukaku nope.
Msimu uliopita lawamazote zilimuangukia kwakuwa alikuwa mzito.. na kufunga kwake magoli ni kwa ku nyatanyata.
Mpaka mashabiki wakataka auzwe dirisha dogo. Leo kaondoka nyie nyie mnalala tena? Mna shida gani?
Yes team haina key strikers kwa sasa. Lakin haimaainish kuwa watu hawapo. Martial ni moja ya wachezaj waliovaa namba 9 na akaitendea hali.
Mpaka hapo alipokuja zaltan.. akakabidhiwa namber sababu ya usupa star.. wkt martial alikuwa kwenye form. Karudishwa kushoto mambo yamekuwa si mambo.
Ushauri wangu martial arudishwe kama namba 9. Winger arud rushford.
Herrera na lukaku mapengo yao yamezibwa?
 
Chelsea sio dhaifu kama akili zako zinavyokutuma..
Beki ya Chelsea itaundwa na Azi, Christensen, Emerson, Rudiger, Zouma, Alonso, Zapacosta pamoja na kijana mdgo James.. hapa kwa mfumo wa beki wanne namuona Rudiger na zouma katikati huku pembeni akicheza Azip na Emerson/ Alonso,, Hebu nambie yupo hata uzoefu hapo? au yupi ni beki dhaifu??

katikati hapa ndo pamenoga zaid,, kuna Kante nadhani hahitaji maneno mengi kumuelezea, yupo Joginho, Mateo, Barkery, Bakayoko na Monson mont.. hapa kwenye first eleven ni Kante, Joginho na barker/ Mateo sijui unataka combination gana zaid ya hii... wakati Kante anasaidia defence, Joginho anatulipa katikati huku Barkery akianzisha mashambulizi...

Hapa mbele yupo William, Pedro, tarented Culum Hudson Odoi (CHO), Roben loftus Cheek, yupo Pulisic ( Captain America) yupo Batman ( New Drogba ) na Olivier Giroud.. Sasa hebu nasiidie mwenyewe kuchagua mwenyewe watatu wa kuanza hapa... Ila kumbuka Captain America wanaweza cheza kama central striker..

Nimesahau kipa eeeh,,, hapa yupo Spain number one,, Keppa arrinini sijui,,, huyu mtoto anaenda kuchukua namba vya De gea pale Spain believe me...

Lampard hana uzoefu?? amecheza final ya play off unataka... hebu nikumbushe wakati zedane anaichukua Madrid alitokea timu gani iliyokua inashiliki LA liga au alitokea EPL ??

Wapinzani wajiandae na masuprise ya Mr Frankie na vijana wake...
Tukutane jumapili zidi ya Manjesta united pale OT...
 
Kwani academy ya United imeanzishwa Fergie alipoondoka?

Haya embu niambie kuna senior players wangapi wanaowika Ulaya pale Man City tangu timu iundwe (achilia mbali, tangu 2013 Fergie alipoondoka, maana hicho si ndio kipimo chako)

Vipi kuhusu Barcelona wapo wangapi wanaowika tangu 2013?

Nirudi kwenye swali lako, kwa uchache hao ndio wanaowika Ulaya tangu SAF aondoke United kutoka United Academy

Rashford Three Lions

Scot Tominay Scotland

Tuanzebe Three Lions

Henderson Goalkeeper - Shefield Wednesday - Three Lions

Pereira - kaitwa Selecao mara moja
Inaonekana hujaelewa. Man city wameanza kuweka serious investment lini kwenye academy? wana best facilties in England mpaka watoto wa former United players wanapelekwa pale. hapa nazungumzia Investment ya Mansour na tangu aingie ndio kwanza miaka 11 kama sikosei, na hio academy tangu aweke investment sina uhakika ni miaka mingapi, wait and see.

Shida ya Man city hawana kocha anaepend kuwapa gametime makinda.

Na hao uliowataja ni wachezaji wa kawaida tu perfomance yao ni average, hawana uwikaji mmoja ulaya. Hata lingard kuna kipindi alifananishwa na Messi. English medias bana!!
 
Tunacompare Man UTD na man city,

Hebu nitajie man city toka club ianzishwe mchezaji mmoja tu Kama Pogba au pique ama Rossi.

Pique Moja ya beki Bora duniani,

Pogba Moja ya midfield Bora duniani

Rossi Moja ya striker Bora duniani (top scorer Serie A na la Liga Mara kibao Kasumbuana na Kina Ronaldo na Messi). Sema Majeruhi tu yameharibu career yake.
Mkuu, tatizo la Man city wanawanyima makinda kucheza EPL na kuwabakisha chini, sasa wachezaji kama hawa ndio mwisho wa siku wanaamua kwenda kwengine na uko wanapokwenda ndio wanapokosa mafanikio mpaka wakawa ma star wa uhakika.

Hao kina Pogba, pique na Rossi, tunajisifia tu wametoka kwenye academy yetu ila wakati tulipokuwa nao hawakutisha wala nini na ndio maana wakaachiwe waende kwengine.

Usichukue credit kwa kila kitu, wengine wamekuwa ma star kwa kubadilisha njia
 
Naona kuna mashabiki humu ndani kisa stress zao za kuwakosa wachezaji waliokuwa wanategemea watasajiliwa, wanaanz kuwadogoisha waliopo, wanalazimisha kama rashford hakufunga goli 20+ msimu uliopita basi na msimu huu hatafunga


Tuache lamri jamani kikosi tulichonacho ndio hicho wanahitaji kuaminiwa,
Mimi bado nitazitazama mechi zetu kwa moyo mmoja kabisa
 
Mkuu, tatizo la Man city wanawanyima makinda kucheza EPL na kuwabakisha chini, sasa wachezaji kama hawa ndio mwisho wa siku wanaamua kwenda kwengine na uko wanapokwenda ndio wanapokosa mafanikio mpaka wakawa ma star wa uhakika.

Hao kina Pogba, pique na Rossi, tunajisifia tu wametoka kwenye academy yetu ila wakati tulipokuwa nao hawakutisha wala nini na ndio maana wakaachiwe waende kwengine.

Usichukue credit kwa kila kitu, wengine wamekuwa ma star kwa kubadilisha njia
Kwa hio wachezaji academy ya man U ambayo sio nzuri wakitoka wanacheza vizuri, na wachezaji academy nzuri ya man city wakitoka wanafeli, ndio logic yako?

Last Time naangalia Pogba anachezea Man U, japo alitoka lakini mapenzi yake kwa club yamemfanya arudi, Alikataa interest za madrid na Barca 2016 na kurudi Man U. Hilo lisingewezekana Kama angekuwa hajakulia Manchester.
 
Kwa hio wachezaji academy ya man U ambayo sio nzuri wakitoka wanacheza vizuri, na wachezaji academy nzuri ya man city wakitoka wanafeli, ndio logic yako?
Hio Ni logic yako ambayo imekufanya uelewe ivo. Nnachokwambia ni kuwa wachezaji wa Man city from Academy hawapit game time kama wanavopata MUFC na ndio maana mnawasikia sikia kwenye media.

Kumbuka kuwa mfumo wa kocha unachangia sana kwenye kukuza au kubomoa kiwango cha mchezaji haijaalishi academy ulotoka ni ipi.

Halafu kitu kingine ujue, now Only the media na fans ndio inaibeba MUFC over MCFC, siku Medias zikiacha kuzungumzia MUFC na kuwa fair, hii timu itasubiri sana kurudisha heshima yake.

Last Time naangalia Pogba anachezea Man U, japo alitoka lakini mapenzi yake kwa club yamemfanya arudi, Alikataa interest za madrid na Barca 2016 na kurudi Man U. Hilo lisingewezekana Kama angekuwa hajakulia Manchester.
Huyu ndo mchezaji ambae ameweka wazi wazi kuwa anataka kuondoka? 😀 Be serious! Fergie alimjua mapema na ndio maana akamuacha asepe zake. Eti mapenzi yake ya MUFC ndio yamemfanya arudi. Duh! Haya basi

Naiombea timu mafanikio!
 
Eti usajili ulikua mgumu kweli kweli mbona madrid anasajili bila tabu
Mimi nadhani tuwape nafasi makinda wanaweza kutusogeza mbele kidogo kuliko kutegemea wachezaji kama Dyabala ambao hawako tayari kupigania team.

Ole kajitahidi kusajili sehemu zenye mapungufu hasa eneo la ulinzi,bado kiungo na mshambuliaji wa kulia.Pia tukumbuke usajili ulikuwa mgumu kweli kweli hasa bei za wachezaji zipo juu sana.

Tumefanikiwa kuziba pengo mlinzi wa pembeni kulia na baki wa kati,naamini Fred,Pereira,Fosu Mensah na McTominary wana uwezo wa kuziba pengo la Hereira na Manywele.Sehemu pekee bado tutaumiza kichwa ni mshambuliaji wa kulia.

Lukaku sidhani kama kaacha pengo kubwa kinda Mason ana uwezo mkubwa kuliko kubwajinga Lukaku.Sijui kwanini mpaka sasa naamini Sanchez anaweza kutusaidia msimu huu.

Tupe team yetu moyo badala ya kulalama.
 
Hio Ni logic yako ambayo imekufanya uelewe ivo. Nnachokwambia ni kuwa wachezaji wa Man city from Academy hawapit game time kama wanavopata MUFC na ndio maana mnawasikia sikia kwenye media.

Kumbuka kuwa mfumo wa kocha unachangia sana kwenye kukuza au kubomoa kiwango cha mchezaji haijaalishi academy ulotoka ni ipi.

Halafu kitu kingine ujue, now Only the media na fans ndio inaibeba MUFC over MCFC, siku Medias zikiacha kuzungumzia MUFC na kuwa fair, hii timu itasubiri sana kurudisha heshima yake.


Huyu ndo mchezaji ambae ameweka wazi wazi kuwa anataka kuondoka? 😀 Be serious! Fergie alimjua mapema na ndio maana akamuacha asepe zake. Eti mapenzi yake ya MUFC ndio yamemfanya arudi. Duh! Haya basi

Naiombea timu mafanikio!
1. Fergie hakumuacha asepe, mwenyewe kwenye kitabu chake anasema alimfuata Evra akambembeleze pogba asiondoke, na Evra Kama rafiki wa karibu wa Pogba pia amethibitisha hili ukitaka ushahidi nitatoa mpaka page za kitabu.

2. Kuna Kauli za Raiola na Kauli za Pogba usichanganye, Pogba Ni mchezaji wa man U na ana mkataba pale, na Ni mmoja Kati ya wachezaji ambao walikuwa na raha pre season, na hata Attitude aliyoonyesha Ime impress wachezaji wenzake, sio maneno yangu Ni stone anaongea



3. Halafu we Jamaa wa ajabu Sana, nimekutajia wachezaji zaidi ya 20 wa academy ya man U wanaocheza Timu mbali mbali ligi ya Uingereza, wewe umeshindwa kutaja hata mmoja halafu unakazania Man U wanabebwa na Media,

Na kazi ya Academy Ni kukuza vipaji, Kama unajua unajua tu utakapoenda utaperform vizuri, Michael Kean aliondolewa na LVG kaenda Burnley kacheza vizuri mpaka kasajiliwa Everton, hao kina Simpson, drinkwater, Heaton etc sio kwamba walikuwa na namba man U, walivyomaliza academy wakatafuta Timu wacheze.
 
Back
Top Bottom