Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Wadau usajil wa msimu huu tumejtahd ila bado kuna changamoto kwenye midfield replacement y pogba incase kauzwa au injury. Pia hatuna winger y kulia n no.10 ya kueleweka tungempata bruno attacking side y2 ingekuwa nzur zaid kwa upande wa defensive sina mashaka nna iman n vijana w2 but tusubir lig ianze ndo tujue wap bado tunachangamoto ila wood anazngua kwa kwel
 
Dirisha la usajili ndio hilo limefungwa

Sasa club iangalie kupata Sporting/Technical Director na si lingine

Shabiki yoyote angependa kuona sura mpya kikosini, hiyo ndiyo hulka yetu.... Yaani hata Rojo angekuwa yupo Benfica juzi tungetamani sana jana atangazwe kuwa mchezaji wetu mpya. All fans are desperate for new faces

Kuna baadhi yetu Nimeona wanawatamani Arsenal kwenye usajili wao na wanauponda usajili wetu. Amin Amin nakwambia, hata Man Utd wasingesajili mwanzo wa dirisha (kama ilivyokuwa kwa Arsenal) halafu mwishoni tuje tusajili Daniel James, Wan Bissaka na Maquire na Arsenal wange fanya usajili huu walioufanya, mapema dirisha lilipofunguliwa, tungeona sisi tumesajili vizuri zaidi

Kiujumla kwa mujibu wa mahitaji yetu na mahitaji ya Arsenal, naona sisi tuna afadhali kuliko wao. NIMESEMA TUNA AFADHALI, SIJASEMA NIMEREDHIKA. Bado naamini tulimuhitaji sana BF asaidiane na Pogba, tulihitaji sana CDM na winger wa kulia, japo hizo nafasi mbili za mwanzo nilizozitaja ndio zilikuwa muhimu sana.

Ukiniambia mimi ni rank timu zipi zilizosajili vizuri (kwa top six) kulingana na mahitaji yao, wa kwanza nitampa Man City, wa pili Spurs na wa tatu atakuwa United kisha Arsenal na Liverpool. Chelsea wao hawakusajili kabisa

Kiukweli tulihitaji sana, beki wa kati na wa pembeni kulia, pia tulihitaji winger ambao watatoa nafasi kwa Martial na Rashford kucheza zaidi kwenye nafasi wanazozipendelea, na hilo ndilo lilifanyika. Huu usajili wa kuzingatia mahitaji ndio unanifanya niseme tumesajili afadhali. Lakini kiujumla usajili wetu msimu huu hauridhishi lakini utaifanya timu kuwa imara kuliko ilivyokuwa msimu ujao

City wameimarika zaidi. Liverpool wataendelea kuwa na changamoto ya depth ya kikosi, Arsenal pia wata improve beki yao ya kushoto na winger yao ya kulia na Spurs watatisha zaidi.

Kiujumla dirisha hili lilipita halitakumbukika sana vichwani mwetu washabiki wa United.

Ngoja tuwaangalie pia mazao kutoka academy akina Mc Tominay, Pereira, Tuanzebe, Greenwood, Gomes, Chong kama wataweza kutuongezea nguvu pale palipopungua.

EPL IS BACK
 
Mm kinachonishangaza ni kuwa watu wanakata tamaa ligi haijaanza. Nyie mashabiki vip.. mlitaka man u wamsajili yesu
Mtu mmoja aje baada ya ligi aseme aone man utd itakavyoshuka mapato...binafsi hamu ya kutazama mechi zake kwisha...


Jana kuna shabiki alichoma jezi Ugenini akimaanisha hatakuja asafiri kutazama timu
 
IMG_0115.JPG


Hamna timu hapa
IMG_0116.JPG

Pogba anafanyaje?
 
Ole sio kocha unauza striker ukiwa huna mbadala?

Unauza kiungo ukiwa huna mbadala?

Mourinho aligoma kumuuza fellain hakuwa na mbadala hapa alilazimisha kuongeza mkataba ulikuwa unakwisha

Ole angemuuza sanchez wala nisingepiga kelele herrera wakumuacha????

Lampard kamuuza luiz akiwa hana mbadala kichekesho

Pep na klopp + pochetino watatunyoosha sana

Kwa sasa hii timu haiwez hata kusimama na arsenal bado west ham, everton, wolves timu imejengwa miaka 26 wafanyabiashara wanaivunja ndani ya miaka 6
 
Wenzetu wanachukulia msimu wa ligi kama mashindano ya ICC pengine.

Kuna michezo mingi sana, hapo Pogba hajavunjwa, Scott hajaumia misuli ya paja.

Sijui, pengine kuna miujiza Ole atafanya. Labda Jones anaanza kucheza kama kiungo.
Ngoja tuone mkuu

Ila kwa viungo tulionao on paper tu ni kama hatuna watu..utakuwa ni unafki tu tukisema kuwa tuko sawa wakati ukiacha Pogba hatuna mtu mwingine pale middle..tulihitaji kiungo wa level za juu kabisa hilo halina ubishi..
 
Jones huwa anacheza kama kiungo pia. Ukimweka hapo DM huwa anakichafua balaa
Wenzetu wanachukulia msimu wa ligi kama mashindano ya ICC pengine.

Kuna michezo mingi sana, hapo Pogba hajavunjwa, Scott hajaumia misuli ya paja.

Sijui, pengine kuna miujiza Ole atafanya. Labda Jones anaanza kucheza kama kiungo.
 
Back
Top Bottom