Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Bolingo alizidi uzito,aliongezeka uzito sana. Binafsi nitafurahi sana kama Martial akirudishiwa No.9 yake na akacheza kati.

Pia hata Sanchez anaweza kucheza hapo. Mtu nisiyemuamini hapo ni Rashford, ana utoto mwingi sana na Ole amemjaza ujinga, anavimba hata akiwa na kipa.

Balaa lipo hapo kwenye viungo. Fred bado hajaonyesha kama anafaa kutegemewa, Matic ndio huyo anakaba kwa macho. Hapo ninao uhakika sana na Scott.
Lets wait n see
 
Mimi naamini msimu huu Spurs na Arsenal ndo wamepiga usajili mkali sana. Hii Man u isiyo na Lukaku wala Herrera nitaibamiza nyingi sana.

Magwaya na Bissaka watacheza kwa presha kubwa ivyo ligi itawashinda mapema.
Harry na Bissaka ni wachezaji wasio na makuu wao ni kazi tu ndugu Ollachuga. Usitegemee kabisa kuona wakicheza kwa presha.

pamoja na kwamba sijaridhika na usajili wa MUFC lakini sijui ni kitu gani kinakufanya uamini una timu ya kuifunga MUFC msimu huu.

Unasahau mwenye timu yake yupo Madrid huko? Luiz ametambua hatari iliyopo ndio maana ameamua kukimbia mapema ili yeye pia aonekane ni pengo 'changifu' katika kumaliza kwenu ligi mkiwa nafasi ya 11.
 
Unajua unashindania makombe mangapi??? Hao watoto na viugoko vyao wataweza pambana na akina ngolo kante au fernandinho....
Wakuu wengi Sana tunamkosoa Ed peke yake juu ya kukosa usajili wa midfielder 1 na striker mbadala wa lukaku....

ila uhalisia ninaoona mimi Ole amechangia kwa hili suala.... issue inakuja solskjaer anaamini sana katika tabia ya kutumia makinda na kuwapa nafasi na kuwa na kikosi kidogo anachoweza kukimanage..... Katika press kadhaa alizungumzia hawa madogo na ameonesha anatamani Sana kuwatumia kwenye first team swali linalokuja hapa je wataderiver?, Nikweli wanatalent ila je wataweza kuishi na pressure ya kusemwa na media pindi wanapocheza chini ya kiwango?....

Greenwood, Angel gomez, Chong na Garner wote wananafasi msimu huu... hapo Greenwood na Gomez wakiwa wamepewa namba ndogo mgongoni ambazo huwa zinatumiwa na wachezaji wale key 23 wa timu..... Kitu kisichopingika kabisa Licha ya talent kubwa waliyonayo Greenwood, Gomez, chong hawana nguvu za kuweza kusema wataweza pambana kuwin baadhi ya mipira...kidogo Garner yupo vizuri ila sio kihivo.......

Msimu huu unaweza kuwa na matokeo mawili tu....either tufanye vizuri sana or tufanye vibaya sana... maana wachezaji wanaweza kuderiver vizuri au wakaharibu kabisa na mbinu ya solskjaer inaweza leta positive impact au ndo inaweza fanya kocha mwingine ake aanze upya hii project inayowapendelea #classof2019.....
 
Tutakuwa wapuuzi sana kufanya usajili eti kwasababu timu nyingine zimesajili....tutasajili kutokana na mahitaji yetu
Manchester United haina winga wa kulia inakaribia miaka 10,one of the strength za United huko nyuma ni kuwa na winga wazuri (Beckham,Giggs,CR7,Best) goal contribution upande wa kulia imekuwa ni ndogo sana kwa sasa.Option zilizopo ni Mata(ambaye ni no 10) na mchango wake kwa sasa ni mdogo na Lingard.We have only one creative midfielder (Pogba) akikabwa/akiumia hatuna timu .Our competitors wamesajili kuimarisha matatizo waliyokuwa nayo
 
Habarini za usiku wakuu..
Dirisha la usajiri limefungwa..kikosi chetu ndo hicho..binafsi nilipenda waje wachezaji wengi zaidi lkn naona kocha na bodi wameamua kubaki na hao..

Tufunge mikanda maana tunaingia kwenye msimu mmoja mgumu sana..na sitashangaa tukiretain nafasi yetu pendwa ya 6..pia tukamaliza msimu bila kushinda hata CARABAO CUP.

Mwisho wa siku hii timu ni yetu..tuiombee mema..tuwe positive..GGMU GGMU.
 
Man u anashinda safi kabisa,wazee wa kubet Man u apewe handicap hiyo game
 
Wapiga ramli mumeshaanza mambo yenu. Karibuni sana
Si kupiga ramli kiongozi hii ipo wazi
Hazard, Luiz, Loftus nani mbadala wao? Japo mna ban ila kungetakiwa kuwe na mkakati wa kutouza key players huku hamruhusiwi kuspend big..... Same applies utd wametoa essential players bila replacement.
 
Ole ndo ana mpango kazi wa timu kwa msimu mzima..sio dhambi kutumia vijana ..sisi tungesubiri ligi ianze tuone timu inafanya nini...timu haijengwi kwa dirisha moja la usajiri...mimi simwamini rashford ila naiamin timu nzima kwa ujumla wake
 
Manchester United haina winga wa kulia inakaribia miaka 10,one of the strength za United huko nyuma ni kuwa na winga wazuri (Beckham,Giggs,CR7,Best) goal contribution upande wa kulia imekuwa ni ndogo sana kwa sasa.Option zilizopo ni Mata(ambaye ni no 10) na mchango wake kwa sasa ni mdogo na Lingard.We have only one creative midfielder (Pogba) akikabwa/akiumia hatuna timu .Our competitors wamesajili kuimarisha matatizo waliyokuwa nayo
True
 
Back
Top Bottom