Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

IMG_3134.JPG
 
Nakumbuka wakati timu imepoteana chini ya mou,kila idara ilionekana inahitaji marekebisho na hadi kufikia baadhi ya watu kutaka aina flan ya wachezaji wauzwe hawana hadhi ya kuichezea united. Lakini leo hii timu iko vizuri hao hao wachezaji wanaonekana mou alikuwa anawafuja kwa mbinu zake,sasa wanadeliver.
Herrera chini ya mou alionekana wa kawaida au mchezaji wa kumlinda mtu mmoja dakika zote 90,lakini leo hii anazurura uwanja mzima na maajabu yake sitaki kuyaongelea zaidi.
Kwa sasa timu inapata matokeo ya goli 3+ bila clean sheet tunajiaminisha kuwa defence yetu bado,lakini tungepata clean sheet walau 2 kati ya hizo game 3 usingeona ukosoaji humu. Ninachotaka kuwauliza mashabiki wenzangu humu,defence ya city,Chelsea na Liverpool inakipi cha ajabu kuliko united? Ederson,keppa na becker wanakutana na michomo mingi na kutokea pembe zote kama ilivyo kwa de gea,sema bahati yetu haijafika tu kupata clean sheet.
Nina imani kama ilivyo kwa safu yetu ya ushambuliaji kuwa kwenye wakati mzuri,itafikia zamu ya ulinzi pia kwa uimara zaidi ya huu aidha kwa mwalimu kuongeza mbinu au kujitoa kasoro ndogo walizo nazo wao wenyewe.
Tangu zama za mou,defence ilikuwa mbovu sababu tulikuwa tunaruhusu kushambuliwa zaidi tena karibu na lango letu.
Tumpe muda huyu jamaa aseme mwenyewe kama anataka striker,kiungo au beki. Siye tupate matokeo mazuri na burudani toka kwa solskjaer hayo mengine ni zaida tu
GGMU
Jana nilikuwa nacheki mechi na jamaa yangu mmoja hivi,akawa analalamika sana kuwa timu yetu bado inaruhusu wapinzani kushambulia,mimi nikamuuliza ni timu gani inacheza mechi zote bila kupata sekeseke kutoka kwa wapinzani??..analilia tu clean sheet..yaani akawa ananiboa kinoma..Man city,chelsea,spurs wote hawa gemu nyingi tu hawana clean sheet recently.


Mimi nachoweza kusema ni kuwa mabeki tulionao itafika time tutapata pair nzuri na watakuwa na hizo clean sheet,but for the mean time sisi tuendelee kufunga magoli kama mvua..

Replacement zinaweza kufanyika baadae kwenye baadhi ya maeneo lakini kwa sasa kikosi hiki bado tunaweza kudeliver vizuri tu..


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana nilikuwa nacheki mechi na jamaa yangu mmoja hivi,akawa analalamika sana kuwa timu yetu bado inaruhusu wapinzani kushambulia,mimi nikamuuliza ni timu gani inacheza mechi zote bila kupata sekeseke kutoka kwa wapinzani??..analilia tu clean sheet..yaani akawa ananiboa kinoma..Man city,chelsea,spurs wote hawa gemu nyingi tu hawana clean sheet recently.


Mimi nachoweza kusema ni kuwa mabeki tulionao itafika time tutapata pair nzuri na watakuwa na hizo clean sheet,but for the mean time sisi tuendelee kufunga magoli kama mvua..

Replacement zinaweza kufanyika baadae kwenye baadhi ya maeneo lakini kwa sasa kikosi hiki bado tunaweza kudeliver vizuri tu..


Sent using Jamii Forums mobile app

Sijui ubora wa defence yetu huwa tunaulinganisha na wa timu gani. City wanapunguza mashambulizi langoni mwao kwa kiungo chake kukaa na mpira muda mrefu,lakini nafasi chache wanazopata wapinzani ederson anakufa tu.
Kiungo kikikubali,automatically hata ulinzi utaboreka tu.
 
True that..hata uwe na beki wazuri duniani wote kwenye defence line,kama kiungo kinatetereka na lazima upigwe goli nyingi tu
Sijui ubora wa defence yetu huwa tunaulinganisha na wa timu gani. City wanapunguza mashambulizi langoni mwao kwa kiungo chake kukaa na mpira muda mrefu,lakini nafasi chache wanazopata wapinzani ederson anakufa tu.
Kiungo kikikubali,automatically hata ulinzi utaboreka tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi habari za man u kuwa na weak defense hazina mashiko wakati wa JM Man u ilikuwa ina defend na wachezaji 11, wote wanabanana na DEGEA kwenye 18 na tulikuwa tunafungwa.

leo tumepunguza idadi ya madefender wetu kwenye 18 yetu tunashinda mechi watu wanalalamika,
our philosophy ni attach attach attach attach attach no time for defending.
 
Jamani Nawasalimia.

GGMU...




Sent using Jamii Forums mobile app

Yani Mkuu navuta picha kipindi kile wewe peke yako unaendesha Kampeni ya Kufukuzwa Mourinho halafu watu wanakushambulia na kukuita Hujui mpira, Unaandika pumba, Mara kama humtaki Mourinho hama timu!!

Leo hii kila Mshabiki Wa Man United hapa anajifanya nayeye alishiriki katika kuendesha Kampeni za kumfukuza Mourinho kuliko Hata wewe 😀😀

Tena kuna wengine wanajifanya sasahivi kusema eti Mourinho anafaa kushtakiwa wakati walikuwa wakimtetea na kukushambulia wewe

Kuna mjinga mmoja anaingia kimyakimya humu anaona haya ata kupongeza ushindi Wa OGS kutokana na misifa aliyokuwa akimpa Mourinho na Kukushambulia wewe. 😀
Inaonesha anasubiri Man United iteleze game moja tu aibuke hapa! 😀😀

Hongera Mkuu Anti-Mourinho Campaign Manager wa JF.
 
Hatimaye kikokotoo kipya kilichokataliwa nchini Tanzania chaanza kutumika nchini Uingereza chini ya ukokotozi makini wa Manchester United.
 
Tuna tatizo Katika Beki yetu, hili lipo wazi, Hatuna right Beki Nzuri, Valencia na Young umri umeshawatupa, Dalot bado.

Tunahitaji fullback mmoja wa ziada tukiendelea kutafuta combination Nzuri ya waliopo, kuna improvement Nzuri kwa Lendlof.

Naamini bench letu la Ufundi litafanyia Kazi mapungufu yaliyoonekana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom