Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu Damushin una IQ kubwa kusoma matukio ya club pia unatoa ufafanuzi mzuri mno kwa kugusa historia na current situation.... Kuna uongo tunalishwa hapa bila sisi kujua..... Alafu alisema Valencia mgonjwa juzi Valencia kasema yupo fiti na ni technical reason zinamuweka nje.... Kwanini kocha asiwe muwazi?... Mwisho shikamoo Damushin najua hutulazimishi kukubali hali ya club ila muda mwingine board yetu inaonewa kwa sababu haiwezi kutoka nje kumpinga kocha direct
bingo
hii heshima uliyonipa ni kubwa mnoo lakini nitaipokea kwa mikono yangu miwili isiokuwa na uzito wowote kwa wengine.
ahsante sana
 
Mimi sio fan wa Jose' Mourihno lakini naamini kama angepewa mahitaji yake yote kama pep anavyopewa kwa kipindi hiki cha miaka mitatu,kuna mwaka Jamaa angetupa mafanikio na kuacha timu yenye backup nzuri..

Tunadanganyana tu kuwa pep akipewa hii timu itasumbua pale uingereza..No,sidhani hivyo..lakini naimani itaimprove at some point..

Fagia Fagia inabidi ifanyike,tunawachezaji ambao washachoka na wengine ni bang average..Young,,Smalling,,Valencia,,Mc Tominay,,Jones,,Matic,,Lingard,,Raahford,,Darmian

Inabidi tujitafakari jinsi ambavyo tunafanya sajili zetu aisee..tumekuwa ovyo sana..leo unamsajili Fred then benched,,Dalot then benched..city angalia wanavyosajili..kila sajili inaingizwa kwenye timu,,angalia Laporte,Mahrez na wengine
inawezekana tunayo yazungumza yana ukweli ndani yake au ni kinyume chake,ngoja tusubiri siku atakayoondoka jose mourinho huenda atazungumza yote yaliopo ndani ya klabu kama alivyofanya LVG baada ya kudai ya kwamba viongozi wa manchester united hawana uelewa mkubwa wa mpira isipokuwa uelewa wao mkubwa upo kwenye biashara ukilinganisha na viongozi wa bayern munich.
mambo ya ndani hatuwezi kuyaelewa makapuku kama sisi tusiotimiza hata mlo mmoja uliotimia kwa siku na tutabaki kuwa watabiri uchwara.
kwa maoni yangu finyu kwa sababu sijakamilika inawezekana kwa nyakati hizi:
  • inawezekana jose mourinho lile jicho lake la tatu limepoteza nuru kwa kiasi kikubwa sana jambo linalompelekea kupoteza umakini kwenye swala zima la ufundishaji wake wa soka, kwa mfano jaribu kuangalia usajili anaoufanya ndani ya klabu wachezaji wote aliowasajili inawachukua muda sana kuendana na matumaini aliyoyaweka ndani ya muda mfupi mfano fred, dalot, lindelof imemchukua msimu mzima kuendana na matumizi yake na wengine ndio wamepoteza muelekeo kati kati ya mapambano kwa mfano nemanja matic,eric bailly, henrick mkhitaryan na hata lukaku.
  • pia inawezekana labda vifungu vya mkataba dhidi ya manchester united vinamzuia kuwa mbwatukaji kwenye ishu zote za ndani ya klabu ndio maana amepoa sana tofauti na kipindi kile alipogombana hadharani na viongozi wa juu wa chelsea kwenye ishu kama ile ya usajili wa shevchenko,kupewa nafasi mzee avram grant kuwa mkurugenzi wa ufundi wa chelsea kipindi kile.
  • binafsi nashangaa inakuwaje jose mourinho huyu aliyewahi kumuondoa william gallas ndani ya chelsea kwa uhuni na fedha juu kwa ajili ya ashley cole kiurahisi rahisi tu leo hii anakubali kuwa na wachezaji watatu wenye uwezo unaolingana kwenye klabu, mfano valencia, ashley young, matteo darmian. mourinho hakuwa hivi sasa sijui ni kipi kimemkuta yule mzee mtafsiri lugha wa zamani.
je macho yake yamepoteza nuru au amepoteza mamlaka makubwa kwenye ishu nzima ya kuwasimamia wachezaji?
kiurahisi rahisi mourinho anakubali jesse lingard kupewa mkataba mpya wenye thamani ndani ya klabu?
au wewe kiupande wako unaonaje?
Chelsea na United ni timu tofauti zinavyoendeshwa na wakati anaenda Chelsea kwa mara ya kwanza Roman alikuwa anataka kutengeneza empire ndio maana alimpa wachezaji wote ambao Mourinho aliwataka na walifanikiwa Mourinho ndio ametengeneza foundation ya mafanikio ya Chelsea na hii ndio faida anayoipata Pep kwa wale waarabu wanaamini Pep atawapeleka next step ndio maana wanamsikiliza pia kumbuka alivyoenda Chelsea mara ya pili aliwasajili Willian,Costa,Fabregas,Matic ambao hawa pia walikuwa na impact kubwa Chelsea

Kocha yeyote akija Manchester United baada ya SAF lazima ata-struggle lazima tukubaliane na hili the problem most of us tumeishangilia United kipindi cha mafanikio so ni ngumu sana kuona timu ikiwa inafanya vibaya

Kocha hawezi ku-aprove mchezaji auzwe kama hajapata replacement yake (Darmian ilikuwa auzwe) lakini wakati tunaanza msimu most of senior defenders walikuwa majeruhi au hawakwenda pre-season sababu walitoka WC (Young,Dalot,Rojo,Valencia).
 
inawezekana tunayo yazungumza yana ukweli ndani yake au ni kinyume chake,ngoja tusubiri siku atakayoondoka jose mourinho huenda atazungumza yote yaliopo ndani ya klabu kama alivyofanya LVG baada ya kudai ya kwamba viongozi wa manchester united hawana uelewa mkubwa wa mpira isipokuwa uelewa wao mkubwa upo kwenye biashara ukilinganisha na viongozi wa bayern munich.
mambo ya ndani hatuwezi kuyaelewa makapuku kama sisi tusiotimiza hata mlo mmoja uliotimia kwa siku na tutabaki kuwa watabiri uchwara.
kwa maoni yangu finyu kwa sababu sijakamilika inawezekana kwa nyakati hizi:
  • inawezekana jose mourinho lile jicho lake la tatu limepoteza nuru kwa kiasi kikubwa sana jambo linalompelekea kupoteza umakini kwenye swala zima la ufundishaji wake wa soka, kwa mfano jaribu kuangalia usajili anaoufanya ndani ya klabu wachezaji wote aliowasajili inawachukua muda sana kuendana na matumaini aliyoyaweka ndani ya muda mfupi mfano fred, dalot, lindelof imemchukua msimu mzima kuendana na matumizi yake na wengine ndio wamepoteza muelekeo kati kati ya mapambano kwa mfano nemanja matic,eric bailly, henrick mkhitaryan na hata lukaku.
  • pia inawezekana labda vifungu vya mkataba dhidi ya manchester united vinamzuia kuwa mbwatukaji kwenye ishu zote za ndani ya klabu ndio maana amepoa sana tofauti na kipindi kile alipogombana hadharani na viongozi wa juu wa chelsea kwenye ishu kama ile ya usajili wa shevchenko,kupewa nafasi mzee avram grant kuwa mkurugenzi wa ufundi wa chelsea kipindi kile.
  • binafsi nashangaa inakuwaje jose mourinho huyu aliyewahi kumuondoa william gallas ndani ya chelsea kwa uhuni na fedha juu kwa ajili ya ashley cole kiurahisi rahisi tu leo hii anakubali kuwa na wachezaji watatu wenye uwezo unaolingana kwenye klabu, mfano valencia, ashley young, matteo darmian. mourinho hakuwa hivi sasa sijui ni kipi kimemkuta yule mzee mtafsiri lugha wa zamani.
je macho yake yamepoteza nuru au amepoteza mamlaka makubwa kwenye ishu nzima ya kuwasimamia wachezaji?
kiurahisi rahisi mourinho anakubali jesse lingard kupewa mkataba mpya wenye thamani ndani ya klabu?
au wewe kiupande wako unaonaje?
Heshima kwako Mkuu. Mimi nitoe mtazamo wangu kidogo. Kinacho sababisha Mou awe mpole nadhani inachangiwa Na mambo mawili. 1) Mou alikuwa anaipenda kazi ya kufundisha Man utd pengine kuliko timu zote/nyingi alizo pitia. Ilikuwa ni ndoto yake kuifundisha man utd. Hii imepelekea kuwa mstaarabu kiasi maana hatak kuipoteza kazi yake. Sio sababu anataka hela tu ila ni Kwa sababu anaipenda timu. Mou tunaye mjua sio MTU Wa kumkumbatia Darmian,Young,Jones na wengineo eti Kwa kisingizio cha kuwapa nafasi ya kumshawishi. Kinacho
2) mfumo Wa uendeshwaji wa timu uko tofauti na kote aliko pita. First time alipo Kuwa Chelsea yeye ndio alikuwa anaamua anamtaka nani bila kujali gharama na Abramovic alikuwa anatoa hela. Abramovic alipo anza kumpanda kichwani wakagombana akaondoka. Inter walimuachia kila kitu yeye. Madrid hakuwa na sauti kubwa ila Kwa hali waliyo kuwa nayo ilibidi wamvumilie. Ndio maana aliweza kusajili kina Ozil wakati Kaka yupo Kwenye hiyo nafasi.
 
Chelsea na United ni timu tofauti zinavyoendeshwa na wakati anaenda Chelsea kwa mara ya kwanza Roman alikuwa anataka kutengeneza empire ndio maana alimpa wachezaji wote ambao Mourinho aliwataka na walifanikiwa Mourinho ndio ametengeneza foundation ya mafanikio ya Chelsea na hii ndio faida anayoipata Pep kwa wale waarabu wanaamini Pep atawapeleka next step ndio maana wanamsikiliza pia kumbuka alivyoenda Chelsea mara ya pili aliwasajili Willian,Costa,Fabregas,Matic ambao hawa pia walikuwa na impact kubwa Chelsea
je kwa maoni yako kwa jinsi soka lilivyozidi ushindani nchini uingereza unadhani bado ni sahihi kwa klabu kuendeshwa kwa mfumo huu uliopo ya kwamba kauli ya kocha haina nguvu sana ukilinganisha na kauli ya CEO na mabwana zake kwenye soko la usajili?

kama kila kocha anayekuja manchester city anapewa kila kitu lakini kiupande wetu kocha anapangiwa cha kufanya kwenye soko la usajili huoni kama itatuchukua tena miaka 6 kuwafikia manchester city?

je kwa sasa hivi ndani ya uwanja tuna empire au dynasty mbele ya wapinzani wetu manchester city?
hili la mwisho naomba uwe mkweli fundi wangu Belo
 
Kocha hawezi ku-aprove mchezaji auzwe kama hajapata replacement yake (Darmian ilikuwa auzwe) lakini wakati tunaanza msimu most of senior defenders walikuwa majeruhi au hawakwenda pre-season sababu walitoka WC (Young,Dalot,Rojo,Valencia).
  • kwa mawazo yako unadhani ni sahihi kwa klabu au kwa kocha kuendelea kuwashikilia wachezaji watatu hawa wanaofanana kimpira kuendelea kutoa huduma ndani ya klabu (valencia, young, darmian matteo) kwa pamoja?
  • kwa nini kocha au klabu wanashindwa kufanya maamuzi ya kubaki na mmoja kati ya hao watatu, kama ni mimi nitamchagua ashley young kwa sababu ana uwezo wa kunipa faida mbili kwa wakati mmoja, ana uwezo wa kucheza upande wa kulia na kushoto japokuwa kiwango chake hakiridhishi.
  • je kwa uoni wako una amini ni kocha ndiye anayeshikilia wachezaji hao watatu kuendelea kuwepo kwenye timu kwa pamoja au ni bodi ya klabu ndio inamlazimisha mourinho aendelee kuwatumia wachezaji hao kwa sababu wanaamini bado wana uwezo wa kucheza ndani ya klabu hivyo basi hakuna ulazima wa kutumia fedha kwa dhumuni la kuleta damu mpya zitakazoendeleza ushindani? au ni wote kwa pamoja wana imani hao wote watatu wanastahili kuendelea kuwepo ndani ya klabu?
  • kuhusu replacement ninavyofahamu mimi hawashuki mbinguni kama mvua au samaki aina ya kambare bali replacement hutafutwa, njia ya kwanza ni kutumia academy kama klabu ilivyowapa nafasi vijana kama gary neville, phil neville, wes brown, oshea n.k .njia ya pili ni kununua wachezaji aliokwisha kutengenezwa kama wanavyofanya manchester city.
  • kiupande wangu ninajenga imani ya kwamba matteo darmian hata kama angeliondolewa asingeleta athari kubwa yoyote kama ilivyokuwa kwa darley blind kuondoka kwake.
 
je kwa maoni yako kwa jinsi soka lilivyozidi ushindani nchini uingereza unadhani bado ni sahihi kwa klabu kuendeshwa kwa mfumo huu uliopo ya kwamba kauli ya kocha haina nguvu sana ukilinganisha na kauli ya CEO na mabwana zake kwenye soko la usajili?

kama kila kocha anayekuja manchester city anapewa kila kitu lakini kiupande wetu kocha anapangiwa cha kufanya kwenye soko la usajili huoni kama itatuchukua tena miaka 6 kuwafikia manchester city?

je kwa sasa hivi ndani ya uwanja tuna empire au dynasty mbele ya wapinzani wetu manchester city?
hili la mwisho naomba uwe mkweli fundi wangu Belo

I think kinachoiponza United ni mafanikio waliyopata huko nyuma ambayo kwa kiasi kikubwa yalichangiwa na SAF ambaye alikuwa anaweza kupata mafanikio hata akiwa na average players +(Scouting ya klabu ilikuwa inafanya kazi nzuri sana) .Evra alisajiliwa kwa £5m,Vidic £12m,Van der Sar £2m so Glazers waliridhika as long wao wanaendelea kutengeneza faida kubwa nje ya uwanja.United ilimuuza CR7 kwa £80m replacement yake walikuwa Owen/Valencia / Obertan but kwakuwa alikuwa SAF still aliendelea kuchukua vizuri

Klabu nyingi sasa zina Director of Football ambaye anakuwa link kati ya top management(CEO,Owner) na technical bench na kuendelea kuhakikisha philosophy ya club inaendelea hii inasaidia hata makocha watakaopewa kazi wanakuwa hawatofautiani,
Juventus -Giuseppe Marota,Dortmund-Marc Zorc,Man City-Txiki Begiristain,Bayern-Matias Sammer/Hassan Salihamidzic,Liverpool-Michael Edward,Ajax-Overmars ,Atletico-Andrea Berta angalia hizo timu zinavyoendeshwa recently kuanzia kusajili wachezaji na makocha .Juventus miaka yote wanasajili wachezaji wazuri cheap hata wazee lakini wanakuwa na mchango mkubwa sana.Ukiangalia kuanzia Mancini,Pellegrini ,Pep hawa wote wanacheza soka la kushambulia ndio maana Kompany,Aguero,Silva,De Bruyne,Sterling,Fernandinho hawa hawakusajiliwa na Pep lakini ni wachezaji anaowategemea

Ferguson,Moyes,LVG,Mourinho (hatujui anayekuja) wote ni makocha wenye philosophy tofauti kabisa na kila kocha amenunua wachezaji wake kuna wachezaji hawawezi ku-improve kiwango zaidi ya walichonacho wameshakaa kwenye klabu zaidi ya miaka 4 Valencia,Jones,Young,Rojo,Lingard,Fellaini,Darmian,Smalling ) hata kwenye klabu walizokuwa mwanzo hawajawahi kucheza vizuri zaidi ya wanavyocheza sasa

Since miaka ya mwisho ya SAF Man City walishaanza kuwa tishio kwetu (nakumbuka wanatufunga 6-1,na tulivyowafunga 4-3 Owen anafunga goli la ushindi) tangia hapo sisi tunarudi nyuma wao wanazidi kuimarika na kama management hawataamka very soon wataanza kutuacha
 
Since miaka ya mwisho ya SAF Man City walishaanza kuwa tishio kwetu (nakumbuka wanatufunga 6-1,na tulivyowafunga 4-3 Owen anafunga goli la ushindi) tangia hapo sisi tunarudi nyuma wao wanazidi kuimarika na kama management hawataamka very soon wataanza kutuacha
ahsante sana brother, sijawahi kuchoshwa kusoma comment yako humu ndani kwa sababu una utofauti mkubwa sana na sisi wengineo.

hii paragraph niliyoinukuu huwezi amini nilitaka niiwasilishe humu ndani kesho kama nikiamka na afya njema lakini ndio umeniwahi.
kuna watu wanafikiri utofauti wetu na manchester city ulianza baada ya kuondoka alex ferguson kumbe tokea nyakati za mzee majirani zetu walishaonyesha kila dalili za kutaka kutupindua kupitia mafanikio ya uwanjani.
unalikumbuka lile dili la dimitar berbatov kuja manchester united lilivyokuwa?
lile dili la berbatov na robinho lilikuwa ni fundisho tosha kwa viongozi,mashabiki na hata sisi wapiga kelele wa manchester united kutuonyesha jinsi gani majirani etu walivyodhamiria kutuvua nguo hadharani lakini bahati mbaya hakuna aliyejali kipindi kile.
sasa tumebaki kuugulia maumivu ya nje na ndani.
 
Since miaka ya mwisho ya SAF Man City walishaanza kuwa tishio kwetu (nakumbuka wanatufunga 6-1,na tulivyowafunga 4-3 Owen anafunga goli la ushindi) tangia hapo sisi tunarudi nyuma wao wanazidi kuimarika na kama management hawataamka very soon wataanza kutuacha[/QUOTE]

Wakuu Belo na Damushin heshima kwenu kwa michango yenu iliyoshiba kuhusu klabu yetu pendwa hasa kipindi hiki tunapo batizwa kwa moto kila uchwao.
Kuhusu mstari wa mwisho naomba nitofautiane na ninyi ifuatavyo: Manchester ya Fergie haikuwekeza kuifunga city wala top clubs za wakati huo kama arsenal,chelsea na liverpool kama kipaumbele chake. Fergie alikuwa anahakikisha timu zilizo nje ya top 4 anakusanya point nyingi kadri iwezekanavyo kuliko kukomaa na game 1 ngumu halafu ukikutana na blackburn,portsmouth,astonvila,etc unapigwa au kudroo.
Hata sasa kama united hii ingekuwa inafungwa na big 4 zote lakini ikachukua ubingwa tusingejali kama city amesajili wachezaji wazuri au la.
 
Since miaka ya mwisho ya SAF Man City walishaanza kuwa tishio kwetu (nakumbuka wanatufunga 6-1,na tulivyowafunga 4-3 Owen anafunga goli la ushindi) tangia hapo sisi tunarudi nyuma wao wanazidi kuimarika na kama management hawataamka very soon wataanza kutuacha

Wakuu Belo na Damushin heshima kwenu kwa michango yenu iliyoshiba kuhusu klabu yetu pendwa hasa kipindi hiki tunapo batizwa kwa moto kila uchwao.
Kuhusu mstari wa mwisho naomba nitofautiane na ninyi ifuatavyo: Manchester ya Fergie haikuwekeza kuifunga city wala top clubs za wakati huo kama arsenal,chelsea na liverpool kama kipaumbele chake. Fergie alikuwa anahakikisha timu zilizo nje ya top 4 anakusanya point nyingi kadri iwezekanavyo kuliko kukomaa na game 1 ngumu halafu ukikutana na blackburn,portsmouth,astonvila,etc unapigwa au kudroo.
Hata sasa kama united hii ingekuwa inafungwa na big 4 zote lakini ikachukua ubingwa tusingejali kama city amesajili wachezaji wazuri au la.[/QUOTE]Arsenal haijawahi kumsumbua Ferguson kabisa alikuwa anaifunga anavyotaka

Timu ambayo ilikuwa ngumu kwake ni Chelsea ndio timu ambayo imeifunga Sana United tangu enzi hizo

Miaka ya nyuma Man City hawakuwa tishio Kwa United na walianza kuimarika baada ya kunuliwa na Waarabu na moja ya vitu vilivyomuumiza Ferguson ni ule msimu ambao Man City anachukua ubingwa siku ya mwisho ukisoma kitabu chake amezungumzia hilo.
 
Nimekusoma mkuu..Maybe anakutana na vizingiti ambavyo hakukutana navyo before..Mkuu Damushin wewe unahisi ubabe wake umepotelea wapi??,unaweza kutupa mwanga kidogo..
Japo Mimi siyo damushin ila naona ubabe wake umepotelea kwenye signings zake. Signings alizofanya yeye mwenyewe kwa utashi wake baada ya kupewa kitita karibia £ 300 mil karibia zote hazifanyi kilichotarajiwa na mbaya zaidi zinafanya vibaya, kwa hiyo hapo lazima na yeye akose sauti kuu ya kuwatemea kibesi wenye timu.
 
Since miaka ya mwisho ya SAF Man City walishaanza kuwa tishio kwetu (nakumbuka wanatufunga 6-1,na tulivyowafunga 4-3 Owen anafunga goli la ushindi) tangia hapo sisi tunarudi nyuma wao wanazidi kuimarika na kama management hawataamka very soon wataanza kutuacha

Wakuu Belo na Damushin heshima kwenu kwa michango yenu iliyoshiba kuhusu klabu yetu pendwa hasa kipindi hiki tunapo batizwa kwa moto kila uchwao.
Kuhusu mstari wa mwisho naomba nitofautiane na ninyi ifuatavyo: Manchester ya Fergie haikuwekeza kuifunga city wala top clubs za wakati huo kama arsenal,chelsea na liverpool kama kipaumbele chake. Fergie alikuwa anahakikisha timu zilizo nje ya top 4 anakusanya point nyingi kadri iwezekanavyo kuliko kukomaa na game 1 ngumu halafu ukikutana na blackburn,portsmouth,astonvila,etc unapigwa au kudroo.
Hata sasa kama united hii ingekuwa inafungwa na big 4 zote lakini ikachukua ubingwa tusingejali kama city amesajili wachezaji wazuri au la.[/QUOTE]Ofcourse kadri unavyopiga timu za nje ya top 4 ndivyo unavyopata ujasiri wa kuzipga top 4 pia maana hali ya ushindi unakuwa umeizoea.
Leo hii hata tukimfunga leceister ni habari kubwa sana
 
Toka Man u aondoke Ferguson haikujiandaa namna ya kukabiliana na changamoto za kuondoka kwake, na baada ya plan A yao kushindwa it seems Man u imekuwa frustrated na inafanya mambo kwa hisia zinazojengwa na media pamoja na tahadhari ya kuiporomosha brand.

Kuna makosa kadhaa ya wazi kabisa kwa mpenda mpira yeyote anaweza kuyaona kwa wazi.

1 Board imepoteza mwelekeo na kupungukiwa mbinu za ushindani katika soka la kisasa linalohitaji uwekezaji mkubwa sana kupata mafanikio uwanjani.

2 Board imeshindwa kupata mbadala wa Ferguson na badala yake inafanya kazi ya kutapatapa kujaribu kujinasua bila kujua chanzo cha tatizo ni kipi hasa kimpira man u inaelekea kupotea ndani ya uingereza na nje ya uingereza hili litakuwa ni janga kubwa sana. Liverpool walipotea katika internal competition lakini nje walikuwa wa moto sana.

3 sajili zisizoeleweka toka Ferguson sajili nyingi za wachezaji siyo manchester united materials mfano Darmian, lukaku, Romero, Bailly ,Bastian , Dimaria etc

4 kuna jambo moja sijui labda naliona Mimi tu wachezaji wengi wa Latin America hawafanyi vizuri sana kwenye ligi ya uingereza na hasa Man u wamebahatika wachache sana hili nalo sasa linatatiza pale kikosini.

5 kuna wachezaji wameuzwa wakati walikuwa na mchango mkubwa sana man u na wangekuwa backup nzuri ya team Moja ni Daley Blind, etc

6 makocha kwa sasa mwenye mafanikio badala ya kocha wa kuipa mafanikio man u ingefaa sana wakapata insider wa pale pale man u wakampa kazi badala ya kuokoteza okoteza wapita njia au waokoteze lakini wampe muda wa kutosha.

7 Wachezaji wengi bora wa kiingereza hawaitamani Man u tofauti na zamani half ya squad ya uingereza ilikuwa inatoka man u.
 
Since miaka ya mwisho ya SAF Man City walishaanza kuwa tishio kwetu (nakumbuka wanatufunga 6-1,na tulivyowafunga 4-3 Owen anafunga goli la ushindi) tangia hapo sisi tunarudi nyuma wao wanazidi kuimarika na kama management hawataamka very soon wataanza kutuacha

Wakuu Belo na Damushin heshima kwenu kwa michango yenu iliyoshiba kuhusu klabu yetu pendwa hasa kipindi hiki tunapo batizwa kwa moto kila uchwao.
Kuhusu mstari wa mwisho naomba nitofautiane na ninyi ifuatavyo: Manchester ya Fergie haikuwekeza kuifunga city wala top clubs za wakati huo kama arsenal,chelsea na liverpool kama kipaumbele chake. Fergie alikuwa anahakikisha timu zilizo nje ya top 4 anakusanya point nyingi kadri iwezekanavyo kuliko kukomaa na game 1 ngumu halafu ukikutana na blackburn,portsmouth,astonvila,etc unapigwa au kudroo.
Hata sasa kama united hii ingekuwa inafungwa na big 4 zote lakini ikachukua ubingwa tusingejali kama city amesajili wachezaji wazuri au la.[/QUOTE]
maelezo yako yenye madai ya kuwa sir alex ferguson alijenga timu kwa dhumuni la kupambana na timu zote zinazoshiriki ligi kuu ya uingereza yana ukweli kwa asilimia kubwa sana muheshimiwa fuentte na sababu kubwa ni kuwa timu kubwa zitakupa jumla ya pointi 18 kwa msimu mzima lakini unapozifunga timu za wastani zitakupa pointi 96 kwa msimu mmoja, tokea nianze kufuatilia mpira wa miguu na umri wangu huu unaokaribia robo karne tokea nizaliwe ni Tanzania pekee ndio nimeshuhudia klabu kubwa za simba na yanga ndio zinazotengeneza timu kwa ajili ya kuhakikisha pindi watakapokutana mmoja wapo asifungwe na mwenzake, namaanisha ya kwamba simba au yanga yupo radhi afungwe na Pamba FC au ashanti united mechi zote mbili kuliko kufungwa mechi moja tu na mtani mwenzake asiyekuwa na uwanja hata wa mazoezi.

takribani miezi minne tokea msimu wa ligi umeanza nchini uingereza kwa kiasi kikubwa humu ndani tumekuwa tukijitahidi wachangiaji tofauti kuzungumzia mwenendo wa manchester united, yameshazungumzwa mengi sana lakini kwa kiasi kikubwa michango mingi utakayokutana nayo humu ndani yanakupa mambo mawili makubwa ambayo ndio yanayoisumbua manchester united kwa miaka hii.
  1. kupoteza nguvu na ushawishi wa kupambana na timu pinzani zote 19 zinazoshiriki ligi kuu ndani ya uwanja.
  2. kupoteza nguvu na uwezo wa kupambana na uwekezaji wa manchester city kadri miaka inavyosogea mbele ndani ya uwanja na nje ya uwanja ijapokuwa hizi athari za nje ya uwanja hazijajidhihirisha waziwazi kwa kiasi kikubwa.
Tatizo la kwanza lilianza baada ya kuondoka mwanadamu mgumu, muelewa na mwenye kwenda na wakati anayeitwa sir alex ferguson ndani ya klabu ya manchester united lakini tatizo la pili lilianza kuota mizizi mirefu na migumu kuing'oa tokea nyakati za sir alex ferguson akiwa madarakani. Tuachane na tatizo la kwanza ambalo linazungumzwa kila siku humu ndani turudi kwenye tatizo la pili ambalo amelizungumza Belo kupitia comment yake hapo juzi.
baada ya msimu wa 2007/2008 kumalizika ambapo manchester united walibeba ubingwa wa ligi kuu na ligi ya mabingwa kwa kuifunga chelsea vugu vugu la maandalizi ya msimu mpya wa 2008/2009 lilianza rasmi barani ulaya, nchini uingereza kwa kiasi kikubwa habari zilizokuwa zinazungumzwa zaidi kwa miezi miwili ya usajili ni :
  • habari ya dimitar berbatov kutakiwa na manchester united
  • habari ya robinho kutakiwa na chelsea.
  • mwishoni ni habari ya waarabu kutaka kuinunua newcastle united baadae man city.
September 1- 2008 ambayo ilikuwa ni siku ya kwanza kwa matajiri wa kiarabu kuanza rasmi kuimiliki manchester city ambayo mwanzoni ilikuwa inamilikiwa na tajiri fisadi thaksin shinawatra ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu wa Thailand ndipo balaa lilianzia . Jambo la kwanza walilolifanya hawa waarabu walituma ofa ya paundi millioni 32.5 kwa muhuni daniel levy ambaye ndiye mwenyekiti wa tottenham hotspurs kwa ajili ya dimitar berbatov kumbuka upande wetu kwa miezi 2 tulikuwa tunampigania kwa ofa ya paundi millioni 27- 30.

Unapodhamiria kutanua himaya yako ya utawala jambo muhimu la kwanza unalotakiwa kulifanya ni kuanza kuwatawala majirani zako kwanza ndipo ufanye maandalizi ya kuwatawala maadui wako wa mbali, kitendo cha waarabu wa etihad kutuma ofa kwanza kwa berbatov ambaye tulikuwa tunampigania kwa miezi miwili ilikuwa ni ujumbe tosha kwetu sisi wenye kuonyesha dalili za wazi za majirani kudhamiria kututawala sisi kwanza ndipo waelekeze nguvu kwa wengineo. Bahati nzuri siku hiyo mzee fergie akafanikiwa kuvunja dili la berbatov la kuelekea manchester city baada ya kuongeza dau na pia kumtoa Fraizer Campbell kwa mkopo. balaa likawageukia chelsea ambao na wao pia miezi 2 walikuwa wanahangaika na robinho kutoka real madrid na hatimaye chelsea wakapokonywa tonge mdomoni baada ya manchester city kukubali kulipa paundi millioni 32 na mshahara unaofikia million 270 kwa wiki.
maumivu haya tunayoyapata kipindi hiki yasingelikuwa makali sana laiti kama waarabu wa etihad wangelifanikiwa kuinunua klabu yoyote kama newcastle united kwa sababu sisi ni wababe wa mji wa manchester na pia ni wababe wa nchi nzima ya uingereza kisoka na wanachokihitaji man city ni kutuondolea heshima ya ubabe wa uingereza na ubabe wa mji wa manchester na dalili zinaanza kuonyesha man city wanaelekea kwanza kufanikiwa kuondoa ubabe wa man utd ndani ya jiji endapo tusipokuwa makini.

  • mwanzoni ukiangalia upande wetu sisi kwa kiasi kikubwa sana tulikuwa tunajenga timu kupitia mfumo wa kununua wachezaji ambao walikwisha tengenezwa na timu nyengine mfano nistelrooy, veron, andy cole, yorke, berbatov, ferdinand n.k
  • kuwapa nafasi vijana waliofaulu kupitia mfumo wa academy mfano cleverley, welbeck, brown, chadwick, oshea, scholes, gibson, fletcher n.k
  • kununua wachezaji ambao wanakuja kutengenezwa kwa asilimia fulani ndani ya klabu mfano ronaldo, rafael, fabio, chicharito, vidic, smith, marehemu liam miller kutoka celtic n.k
kwa hivyo ulikuwa unakuta kwa muda mrefu ndani ya manchester united ulikuwa unakutana na timu yenye muunganiko wa wachezaji wa aina kuu mbili kwenye kikosi cha kwanza.
  • wale wenye viwango vikubwa sana tokea mwanzoni mfano ferdinand, roy keane,van persie, giggs, berbatov, tevez, scholes n.k
  • wale wenye viwango vya wastani ambao wanahitaji kwa kiasi kikubwa uwepo wa wachezaji wenye viwango vikubwa ili wapate kujijenga zaidi kiuwezo kwa mfano ujio wa chicharito, ujio wa smalling oshea, evans n.k.
ukija upande wa majirani zetu wanapoingia sokoni wanatafuta wachezaji watakaowapa faida ya hapo kwa hapo, aina hii ya ujengaji wa timu unapobahatika kupata wachezaji wenye viwango vikubwa sokoni basi huchelewi kupata mafanikio tofauti na yule anayejenga timu kwa kutumia aina tatu nilizozieleza hapo juu ambazo kwa kiasi kikubwa ndio tunazozitumia mwanzoni. Kwa mfano angalia chelsea walivyopata mafanikio ndani ya muda mfupi baada ya kufanya uwekezaji wa wachezaji waliokwishaiva kwa ajili ya mapambano iliwachukua miaka miwili tu kujitangaza kwenye ulimwengu wa soka.
wakati wewe unamsubiri welbeck, gibson, cleverley apandishe kiwango chake ili awe mrithi wa paul scholes, rooney na michael carrick pindi watakapochoka mwenzako anakwenda spain kumng'oa yaya toure, sergio aguero na david silva ili wampe mafanikio ya haraka.

mwanzoni kabla ya mabepari hawajavamia mchezo wa soka tulikuwa hatupati tabu sana kwa sababu wapinzani wetu wakiwemo arsenal, walikuwa na mfumo huu tunaoutumia sisi ila tofauti mzee wenger alikuwa haendi na wakati ukimlinganisha na alex ferguson, mzee wenger alikuwa na tabia za kuwa tayari kuvumilia miaka mitatu akimsubiri fabregas au henry ili azibe tatizo lakini fergie alikuwa hana tabia hiyo ndio maana ilifika baadhi ya nyakati hakuona tabu kufungua pochi lake kwa dhumuni la kufanya malipo ya gharama kubwa kwa ajili ya kutatua tatizo la timu yake, kwa mfano jaribu kurejea usajili wa michael carrick, van persie, rio ferdinand, dwight yorke, nistelrooy n.k.
ukiachana na mbinu, ubora na uzoefu wa kocha kwenye mashindano timu yenye muunganiko wa aina mbili nilizozieleza inapokutana na timu inayojengwa kwa mfumo wa kukusanya wachezaji nyota watupu ndani ya kikosi lazima timu A itapata tabu kuliko timu B itakavyopata tabu. Bahati mbaya sana nakiri hadharani nyakati za mwisho za alex fergie timu yetu tayari ilishajaza zaidi group hili la wachezaji wenye viwango vya wastani kuliko group la wachezaji wenye viwango vikubwa ila ubora wa kocha ndio ulitufanya tutembee kifua mbele kwa miaka ya mwishoni.

jaribu kufikiria hizi baadhi ya biashara tulizozifanya kwa nyakati tofauti.​
  1. tulimuondoa mchezaji bora ronaldo ambaye ana uwezo wa kukupa magoli 40 kwa msimu tukaleta wachezaji wa wastani akiwemo valencia, obertan, michael owen. Dili la ronaldo lilipaswa kuzibwa na watu kama frank ribery kipindi kile, tatizo la kuwa na wachezaji wenye viwango vya wastani ndani ya timu ndio hili hawakupi uhakika wa kupandisha viwango vyao kwa haraka kama alivyozungumza Belo.
  2. tulikataa kumsajili carlos tevez ambaye majirani zetu walimchukua kwa paundi 27 millioni, huyu tevez aliondoka msimu mmoja na ronaldo. inamaana tuliwaondoa watu wawili wenye uwezo wa kukupa magoli 60 kwa msimu mmoja na nafasi ya tevez ilizibwa na msenegal mame biram diouf ambaye alishindwa kufikia matarajio yetu. carlos Tevez alipokwenda etihad alifunga magoli 29 msimu wake wa kwanza na kuifanya city ishike nafasi ya 5 wakati msimu wa nyuma yake man city walishika nafasi ya 10. Hivyo tuliendelea kumtegemea rooney huku tukisubiri dimitar berbatov aweze kuendana na falsafa ya timu. Msimu wa 2010/2011 carlos tevez aliwasaidia man city kushika nafasi ya 3 baada ya kufunga magoli 23 wakati man utd tulibeba ubingwa na kufungwa na barcelona. msimu huu kiupande wetu dimitar berbatov anafunga magoli 21 kwa msimu mzima. Msimu huu balaa la kuwafunga man city kwa tabu likajiendeleza tena, unakumbuka tik tak la wayne rooney?
kwa ufupi ukianzia mwaka ambao man city wanafanya sajili za wachezaji waliokwisha tengenezwa na timu nyengine kiupande wetu sisi wale wachezaji wenye viwango vikubwa walikuwa wapo katika nyakati zao za mwisho na wale wanaopaswa kuziba nafasi za mafundi kama giggss (umri 37), scholes (umri 34), evra (32), vidic (31), ferdinand (33) ,carrick (32), rooney (30) kupitia mfumo wa academy au kuwanunua kupitia timu nyengine viwango vyao wengi wao vilibaki vile vile bila ya kufikia viwango vya mafundi wetu, ni David De gea peke yake ndiye anatupa faida ile tunayoihitaji kwa kuweza kuziba nafasi ya edwin van der sar.

ndio tukasema tishio la man city lilianza tokea nyakati za mwisho za alex ferguson akiwa madarakani bila ya kusahau kipigo cha magoli 6, tuacheni na habari za mzee wetu sir alex ferguson ambaye alijenga emperor kubwa kwa miaka 26 ya utawala wake pale old trafford.

hivi labda tujaribu kujiuliza​
  1. jee smalling na phil jones kabla na hata baada ya kuondoka fergie wamefikia angalau viwango vya ottamendi na vicent kompany ambao hawana nafasi kwa majirani zetu? cha ajabu hawa wote wawili walicheza pamoja na walinzi bora kwa zaidi ya miaka 10 ambao ni vidic na ferdinand, lile dhumuni la kuwanunua wakiwa na viwango vya kawaida na kuwatengeneza ili kuziba nafasi za magwiji wa ulinzi halijazaa matunda kwa asilimia 40 kwa maoni yangu lakini.

lakini upande wa pili wa shilingi tokea aondoke ferguson cha ajabu tumeachana kabisa na mpango wa kununua wachezaji wenye viwango vya kawaida na tumeiga tabia za majirani zetu za kufanya uwekezaji wa wachezaji waliokwisha tengenezwa moja kwa moja na timu nyengine lakini cha kushangaza sana matokeo tunayoyapata afadhali ya ferguson na gurupu lake la wachezaji kama vile obertan, buttner, fabio, bebe, macheda aliweza kupambana dhidi ya manchester city na timu nyengine japokuwa presha ilikuwa kubwa kuliko hawa wazee wa kutumia hela waliorithi nafasi ya fergie
mambo yanayoendelea kutuumiza vichwa na kutufanya tugawanyike kimtazamo​
  • je turudi tena zama za ferguson za kusajili wachezaji wenye viwango vya wastani na wale wenye viwango vikubwa huku tukiendelea kuwavumilia kwa miaka angalau 3 tukiwa chini ya mwalimu asiyekuwa na presha yoyote, nyakati za ferguson tuliwahi kukaa miaka 3 bila ya ubingwa na miaka 3 baadae tukachukua makombe kwa miaka 3 mfululizo (rejea misimu ya 2003, 004, 005, 006,007 na 2008).
  • kama leo hii tunasajili wachezaji bora tunaishia nafasi ya 2 hadi ya 7, vipi kuhusiana na hawa average kama walivyokuwa akina vidic, heinze, alan smith, ronaldo kutoka sporting si tutaishia nafasi ya 10? kwa sababu majirani zetu hawatoacha mfumo wa kununua wachezaji bora labda makocha wa timu pinzani wawe na akili za arsene wenger
  • je tunasajili wachezaji bora au tunauziwa wachezaji wenye majina bora?
  • tatizo letu ni mwalimu na uongozi wa manchester united?
  • kama tatizo ni uongozi mbona nyakati za fergie alifanya kazi na watu hawa waliopo madarakani lakini matokeo mazuri yalionekana?
  • kama tatizo ni walimu mbona jose na van gaal wana cv nzuri?
  • mbona david moyes alisifika kwa kuwapa nafasi vijana alipokuwa everton lakini kwetu kashindwa, rejea ubora wa wachezaji kama vile rodwell, jagielka, baines, pienaar steven, osman leon, arteta n.k?
  • mbona majirani zetu wachezaji wao waliofeli wanahesabika?
  • je laana ya liverpool tumeirithi sisi hivyo basi hata kama tutamsajili messi na guardiola ndio yale yale? (mhhhh ila mimi siamini ujinga huu)
miaka 6 tumefanya usajili wa wachezaji wafuatao lakini hatujawahi kuvuka hata robo fainali ya UEFA wakati majirani zetu wamefika nusu fainal zaidi ya mara mbili, huu usajili tulioufanya kwa kuangalia majina yao ni wachezaji wanaopaswa kukupa ubingwa tena mbele ya timu ngumu kama ya real madrid na barcelona.
sir alex baada ya kufungwa nusu fainal na AC milan msimu uliofuata alimuongeza tevez, owen hargreavez, anderson na luis nani tukabeba ubingwa lakini nyakati hizi balaa liko palepale licha ya usajili tunaoendelea kufanya
paul pogba = 95 million
mkhitaryan = 25 million
lindeloff victor = 30 million
marcos rojo = 15 million
luke shaw = 27 million
eric bailly = 25 million
lukaku = 75 million
nemanja matic = 30 million
fred = 55 million
diogo dalot = 20 million
antony martial = 55 million
juan mata = 27 million
maroaunne fellaini = 27 millioni
herrera ander = 27 million
depay memphis 17 million
schneiderlin = 26 million
angel dimaria = 54 million
daley blind = 15 million
matteo darmian = 14 million
bastian schweinsteiger = 3 million
radamel falcao = mkopo.
ibrahimovic = free​

  • ndani ya miaka 10 hii manchester united wamebeba makombe 3 ya ligi kuu ya uingereza
  • ndani ya miaka 10 hii chini ya utawala wa sheikh mansour man city. wameshinda makombe 3 ya ligi kuu ya uingereza.
  • ndani ya miaka 10 hii chelsea wamebeba makombe 3 ya ligi kuu ya uingereza.
  • ndani ya miaka 10 hii leicester city wamebeba kombe 1 la ligi kuu.
  • bila ya kusahau ndani ya miaka 10 arsenal, liverpool kwa pamoja wameendelea kuwa washiriki wa ligi kuu.
mpaka muda huu manchester city yupo juu ya man utd kwenye msimamo wa ligi kuu, tukisema manchester city anamzidi manchester united kwa miaka 10 hii ninakosea?

1542716814798.png
 
Back
Top Bottom