Hiyo ni kawaida miaka yote kwa premier leagueWakuu angalieni hizi mechi inakuwaje tunarudiana na leicester city round ya pili EPL na huku burnley hatujacheza nayo hata round ya kwanza au mm ndo sijaelewa..???
![]()
Aisee sidhani kama ni kweli watu wanataka Man U icheze kama City, watu wanataka Man U iende na ishambulie kwa sababu wachezaji wa kufanya hivyo pale wapo, na siyo Man U inayofunguka inapocheza na Bournamouth halafu ikicheza na top 6 teams inajifungia nyuma halafu tukitoka hapo tunalaumu LukakuShida ni Moja naona kama watu wanamchukia Jose kwa sababu zao binafs especialy kwa ile hulka yake ya Ujeur ila most of the time anaangalia matokeo na mafanikio yake,
Huwez kusema wewe ni kocha bora huku umeshida Kombe la FA wakat mwenzio msimu wake wa kwanza amechukua Europa Cup na League Cup.
LVG alijua kutuchezesha mpira wa mapasi meng bila kuwa na magoli ila kwa jose tuna direct footbal huku tukiwa na magoli meng ya Kufunga
Mfumo wa Pep ni huo attacking n possesing hawez kubadilika kamwe na hakuna wa kumbadilisha na Jose nae ana mfumo wake ambao hauwez kubadilika
Kama mnakumbuka Inter Milan anamtoa Barca kwenye Champion League kwa style ya kupak bus kila mtu alimsifu Jose kwa maana alijua nn anataka na mwisho wa siku alienda kuchukua Champions League Trophy
So Jose abakie na mfumo wake ambao umekuwa ukimpa mafanikio siku zote na Pep atabakia na mfumo wake ambao umekuwa unampa mafanikio hzi kelele za kutaka Man utd wacheze kama Man city zitabakia siku zote ila ni kitu ambacho hakitakuja kutokea kama hii team itabakia china ya Jose
Daaa ndugu umeongea kwa uchungu na ukweli mtupu, mimi sijui wanaomtetea Mou kwa hii staili ya uchezaji wanapata wapi uhalali huo. Nadhani hata utamaduni wa klabu yao ule ambao mashabiki pale OT wamekuwa wakifanyia chanting Attack! Attack! Attack! Hawaujui.Man utd hatutaki kucheza kama Man city, tunataka tucheze kama Man utd, ile ye Babu Fergie, Babu Fergie nae possession footbal sio style yake, yeye ni mashambulizi tu, ukipata mpira unatakiwa ufanye ufike mbele, Babu Fergie hataki kutia udi kabisa...... Na sio kwamba hawezi au hajui kuchezesha Possession anaweza vizuri sana tu, Ila shida yake ni mashambulizi. Na hata ukiikuta Man utd imecheza na Man city na kufungwa, lakini Under Fergie unajua kuwa ama timu ilizidiwa maarifa, au ilikuwa siku ya kufa nyani tu. Lakini under Jose, unapokutana na timu kubwa yoyote, basi tayari ameshaset mentality yake kuwa tuondoke na point 1 ishatosha, THIS IS NOT MAN UTD!!!
Chelsea iliyochukua ubingwa kabla Mou hajafukuzwa ilikuwa ina shambulia sana. Hata Real Madri ya Mou iliyoanza kuifunga barca ilikuwa inashambulia na kumiliki mpira kwa kiasi fulani.Kwaio Mourinho wa chelsea kipindi ndo anajoin hio team alikuwa ana paki basi na hakuna mashambulizi kabisa? Mourinho yule ilikuwa akikutana na timu kubwa alikuwa anatafuta droo tu hakua na attacking mind? Alikuwa akizi approach timu kubwa kwa woga? Ndivo alivokuwa vile?
Na wewe unapouhusudu huo mfumo wako na Mou ukumbuke kwamba ni kweli zama zimebadilika na huo mfumo unafeli pia. Kumbuka wakati Mou ameanzisha huo mfumo wenu alikuwa ana concede goals kirahisi? Alikuwa anapoteza game kirahisi? Alikuwa anakoswa koswa magoli mengi ya wazi ktk kila game alyocheza huo mfumo? Utagundua ni BIG NO! sasa mbona sasa anafungwa ktk huo huo mfumo wenu kirahisi na timu ya inakuwa exposed sana kwa maadui hasa hasa kwenye defence? Yani unaita cjui kupaki basi, sijui meli halafu wapinzani wanatengeneza nafasi nyingi za magoli ya wazi Mungu anaingilia kati tunakoswa? Refer back game ya liverpool tulitoka droo ila jamaa walikosa magoli ya wazi kabisa, Totten tukawafunga dk ya 85 na tuliruhusu pia walitengeneza nafasi za wazi, chelsea tukacheza nao hivyo tukafungwa, Arsenal tukacheza nao mfumo huo na De gea akafanya saving nyingi kwa game moja hadi kuwazidi makipa wengine wengi ktk game zote walizocheza msimu huu, na wengine bado hawajamfikia, hapo ni Mungu aliokoa jahazi. Tumecheza na City kwa mfumo huo huo tumefungwa tunasema wamebahatisha. Tusipoangalia hata kwa Sevilla tutapaki basi na tutatolewa Champions league.Hili ndio kosa ambalo masahabik weng wa manchester utd tunalifanya zama zimebadilika sio kila siku tutahtaj kile alichokifanya SAF bas makocha wengne nao wafanye hvyo hvyo hatutakuwa tunawatendea haki kabisa
Hata SAF alipkuja Man utd alikuta kuna kocha amabae alikuwa na falsafa yake what if nao wangetaka wacheze kama ilivyokuwa kwa kocha wa nyuma
Tuna bahat mbaya weng kizaz chetu kimeona zaid mafanikio ya SAF kuliko kocha mwengne ila ilfika kipind aliona kabisa utawala wake umefika kikomo amuachie mtu mwengne
SAF alwah kuhojiwa kama angekuwa kocha kipind hik man utd wangemvumila kwa misimu mitatu ya mwanzo bila kuwa na kombe kwa mdomo wake alisema hapana angeshafukuzwa kwa aina ya mfumo wa soka la sasa ulvyo
Wamiliki wa team mashabik wanaangalia mafanikio ya team kwa ujumla wake leo hii ucheze soka la kushambulia na bado huna kombe hata moja hakuna ambae ataoenda kuwa na kocha wa namna hyo
Mourinho ana mfumo wake na sio kwamba ulianzia man utd hapana alikuwa nao toka alipoanza kufundsha soka bas na yeye anataka kutengenza legacy yake kupitia huo mfumo kwa maana ndio ambao umekua ukimpa mafanikio siku zote
Asee Mou hasikilizagi mtu ngoja siku ampange Mata tukiwa tunacheza na Chelsea halafu amwambie huyo Mata acheze namba sita na marufuku kwenda mbele ndo utaposhangaa. Ile siku tumecheza na City nlivoiona lineup yetu nikasema leo ni mwendo wa viberenge tu na cty watahema leo duuu!!!Leo Mou kanisikiliza, badala ya kuwaweka Rashford na Martial kamuweka mmoja na Mata ambae atasaidia creativity all round.
Sifa na 6. Hawa mashabiki wanaishangilia timu yenye mashabiki wengi zaidi dunianiSifa za mashabiki wa man u;
1.Hawajui mpira,wengi wao hufuata mkumbo
2.Wanaongea sana kuliko uwezo halisi wa timu yao utawasikia leo tunashinda 4g halafu wanashinda 1g au wanapata kipigo kabisa
3.Ni mabingwa wa kuvamia thread za watu hata kama wao hawana mechi halafu mambo yakiwaendea kombo huingia mitini tafikir hawapo
4.Wakifungwa mechi husingizia mchezaji fulani hayupo eg PP
5.Timu yao haijui kucheza mpira ila wanalazimisha ionekane inajua utasikia man city tuliwabana walitubahatisha magoli tuliwapa pasi sisi,mara hatutaki kuposses mpira tunacheza mpira wa mashambulizi wa fergie halafu wanaambulia shots on target 4 mechi nzima
Ushauri:Hamuwezi kupambana na city na sasa mnatakiwa kupambana ili mshiriki uefa next season![]()
![]()
![]()
![]()
Umekataa hiyo ya kuvamia threadnani kavamia thread mwingine wewe dada???..
wewe ndo kila thread ya team zisozokuhusu upo
huenda na wao wanakuja huko kuwaponda kwa kuja kwenye thread zao...Umekataa hiyo ya kuvamia thread
Zingine umekubaliana nazo
Mi nakujaga humu kuwaponda kwa hayo matabia yenu
Hakuna wanaomtetea Mourinho tunaongea reality then dont try to compare SAF na makocha wengine kwenye EPL hakuna wa kumfananisha nae alishai-master EPL kuna mechi alipanga karibia timu nzima mabeki lakini alimfunga Arsenal goli 4Daaa ndugu umeongea kwa uchungu na ukweli mtupu, mimi sijui wanaomtetea Mou kwa hii staili ya uchezaji wanapata wapi uhalali huo. Nadhani hata utamaduni wa klabu yao ule ambao mashabiki pale OT wamekuwa wakifanyia chanting Attack! Attack! Attack! Hawaujui.
Ilikuwa inashambulia sana kwenye big match ?Chelsea iliyochukua ubingwa kabla Mou hajafukuzwa ilikuwa ina shambulia sana. Hata Real Madri ya Mou iliyoanza kuifunga barca ilikuwa inashambulia na kumiliki mpira kwa kiasi fulani.
Eeeh hata sisi wenyewe walitushambulia sana na ukipata kamuda cheki replays.Ilikuwa inashambulia sana kwenye big match ?