Wakuu Mou ni kocha mzuri kulingana na historia yake ila anamapungufu mengi..Nakumbuka siku tumetangaza kumpata huyu Mou sikuwa na furaha kihivo maana nilijua kuna ladha tutaikosa sidhani kama kulikuwa na ulazima wa kupaki basi kwa city ambao walionesha kuwa na tahadhari mda mwingi....mpaka tufungwe ndo tuanze kushambulia,mimi binafsi nilipendelea zaidi aje Diego simeone wa Athletic wengi wakapinga kuwa anafika fainal ila hajawahi chukua kitu,jamaa anatengeneza sana wachezaji mentally na anacheza mchezo wa kuvutia sana tena sana...mou yeye anapandikiza wazimu wachezaji wanaenda kujitoa muhanga tukifungwa lawama tu...sikumbuki ni member gani alisema hadhani kama mou anastahili saaaana kuongezewa mkataba Man u maana inaumiza sana wakuu tumepoteza aina ya mchezo wetu na confidence yetu kabisa,,,man u sio ya kupaki bus man u ya kushambulia,man u sio wa kutegemea bahati...Mou anazingua sana man u kwa fujo za city tunaonekana sisi ni genge la wahuni fergie asingeweza kuja kufanya haya daima..
Sure mkuu...man city walitufunga ila hawakuwa strong kama walivyocheza na liverpool au chelsea,hawakutengeneza chance nyingi kama kawaida yao..nachotaka kusema ni kuwa city tulikuwa na uwezo wa kuwafunga,beki zao zilikuwa za kawaida sana.
Inaonekana Mourinho aliwaambia wachezaji wajihami tu,wasifunguke,angalia alivyompanga Martial kabla ya kufungwa alikuwa anacheza kulia,kitu ambacho kilikuwa kigumu kwa martial,na baada ya kufungwa Martial alihamia kushoto na mpira ukaanza kuchezwa hadi tukaequalize goli.
Mourinho approach zake hasa big match ni mbovu sana hata matokeo yanareflect ubovu wake..refer gemu ya liverpool,recently liver ndo timu iliyokuwa na beki mbovu,sasa kwa nini upaki basi?..
Una wachezaji kama rashford,martial,lingard,mata,mhkitaryan na bado approach ni za ajabu ajabu..naungana na kauli aliyoitoa Van gaal,kuwa united ya Mourinho inacheza mpira ambao hauvutii kabisa,hasa kwenye mechi ambazo tunataka tuonyeshe kuwa sisi ni united na tunajua soka.
Mkhitaryan anaongoza kwa assist so far msimu,ila hapa katikati alifllop,na amemdrop kwenye kikosi cha kwanza,Lukaku mechi nane kufunga goli moja,kwa nini na yeye asipewe treatment kama hii?,haiwezekani mshambuliaji uwe unachezea nafasi chache unazozipata ambazo zingeipa timu matokeo,refer kina Rvp,Rooney walivyokuwa wanatupia magoli kwenye mechi muhimu..huyu lukaku anahitaji kuwa benchi ili ajue kuwa hapa ni united na sio Everton...fecking pathetic.
Tutaendelea kupata mafanikio ya kuungaunga na tutacheza Mpira usiovutia under Jose's mourinho kama hatabadili mfumo wake..
Mimi ni Ferrenga,
Shabiki mkereketwa.