Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Nimependa mjadala wa leo wazawa vs haters. Nawakumbusha tu “haters" wakubwa tunajenga nyumba hatutaki kelele au mnataka tununue magarasa kama Perez au Mkorea mwenye jina la tusi yule? Pambaneni kupeleka news jukwaani kwetu huku tuacheni tumchambue Pogba kama tumuonavyo kwetu ni mtu muhimu na limethibishwa na game ambazo alikua hayupo dah timu ilikua inacheza kiwango cha kawaida ila akiwepo kati pale akichezea mpira burudani sana kwetu [HASHTAG]#GGMU[/HASHTAG]
 
Giroud alikuwa mfungaji bora France. Ila alivyokuja England amekuwa kituko.
Kuwa mfungaji bora kwenye nchi moja hakukufanyi uwike nchi nyingine.
 
Giroud alikuwa mfungaji bora France. Ila alivyokuja England amekuwa kituko.
Kuwa mfungaji bora kwenye nchi moja hakukufanyi uwike nchi nyingine.
Kwa hiyo? Manutd walimsajili Bebatov na Louis Saha wenye uzoefu wa kufunga magoli ndani ya EPL lakini matokeo yake hawakuwahi kushinda golden boot!

Akaja Ruud Van Nisteroy kutoka ligi ya Everstite rekodi yake ya kufunga bado inakumbukwa iwe EPL au Champions ligi

My point treat each case as unique because the past experiences of other players irrelevant
 
Sizani kama greizmann ni completely no. 9 striker! Kwangu nadhan belloti atafaa zaidi kama namba tisa...may be greizmann kama namba kumi au 11 au 7!! Pogba aendelee kama namba 8!
Upo sahihi Griezman sio completely namba 9 ye ni namba kumi Zaidi, lakini faida yake anacheza namba,9,10,11,7 na mara chache namba 8 lakini kwenye hii hayupo vizuri sana.

Ila kama akisijiliwa sio mbaya itategemea na mifumo ya Kocha,tunaweza mtumia kama False striker kama Kocha atatumia washambuliaji wawili.

Na vilevile anaweza kutumika kama kiungo mshambuliaji kama Kocha ataamua kuua namba tisa na kuwa na Viungo Zaidi ya watatu mfumo ambao Mourihno ameutumia sana msimu huu kwa kuuwa wing moja hasa no.7.
 
Umesema vema mkuu,ni sahihi Herera ni mmoja ya wachezaji waliofiti kwenye mifumo ya Mou pale Old T kwa haraka na sasa ni tegemeo kubwa sana la Mou hasa katika match anazohitajika kushinda,lakini uchezaji wa Herera toka ajiunge na Man U umekuwa wa kuridhisha na haikutegemewa kama angelimud soka la England kwa haraka Zaidi,mashabiki wa Man U wanamuona Herera kama Muingereza Zaidi kutoka na shughuli yake nyumbani.
 
Kwenye ukweli tuwe wakweli,nakubaliana na uchambuzi wako,pamoja na kuwa shabiki wa Man U toka nianze kushangilia mpira lakini kwa msimu huu bado hatujaona yale makali ya Pogba tuliyotarajia,naweza kumtetea inawezekana kutoka na mifumo ya kocha,Pogba ni mzuri akicheza kama kiungo mshambuliaji na huru akilindwa na Viungo Wengine wasaidizi.

Tumpe mda lakini bado kumpa sifa hizi tunazompa,game chache hasa ya Fainal Europa ligue ndio ameweza kucheza nusu ya uwezo wake.

Ila nina matumaini makubwa Pogba atarudi katika ubora wake.
 
Nasikia Jose Mourinho anataka kumuuza Martial
Maamuzi ya Jose Mou kumuuza A. Martial ni katika kumsaidia Martial ,Mou hamuhitaji Martial na hana mipango naye msimu ujao ni bora kumpa nafasi katika timu nyingine,ila nadhani Mou angeendelea kumuamini Martial,ni mchezaji mzuri lakini ameshindwa kuperforme msimu huu katika aina ya soka la Mou.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…