KOCHA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amesisitiza kuwa ubingwaupo wazi kwao au Chelsea licha ya timu yake kuadhibiwa na maamuzi duni ya mwamuzi wa mchezo dhidi ya Arsenal juzi.
Alisema makosa ya mwamuzi Chris Foy katika mchezo huo yaliikosesha penalti Man United kipindi cha pili baada ya Gael Clichy kumkwatua Michael Owen.Ferguson alieleza imani yake kwamba Foy alikosea kwa kushindwa kuwapa penalti ya dakika ya 88 baada ya Clichy kumchezea vibaya Owen.
Pia, alieleza kuwa wapinzani wao (Arsenal) pia walinyimwa penalti kipindi cha kwanza baada ya Nemanja Vidic kucheza kwa mkono krosi yaTheo Walcott.Kwa matokeo hayo, Chelsea ina pengo la pointi tatu nyuma ya Man United baada ya Jumamosi kuishinda Tottenham kwa mabao 2-1 na timu hizo zinakutana Old Trafford , Mei 8.
Miezi 11 iliyopita, Didier Drogba alifunga bao la ushindi na kuipa ushindi Chelsea na ubingwa dhidi ya Man United, lakini Ferguson ana matarajio ya kutorudia kosa."Utakuwa mchezo mgumu, una umuhimu mkubwa, lakini unahitaji maamuzi sahihi," alieleza Ferguson. "Ninajua utakuwa mgumu kwa kila mmoja wetu.
"Sina shaka kwamba uamuzi wa kutunyima penalti na nafasi ya kusawazisha umewasaidia Chelsea ambao tunakutana nao wiki moja ijayo. Wao (Chelsea) walipata ushindi na ubingwa pale Old Trafford , hiki kinanipa wasiwasi.
"Lakini, kuhusu uwezo - mchezo pale Old Trafford, mbele ya mashabiki, tupo tayari kwa vita, nimewaambia pia wachezaji wangu."
Katika mchezo wa Jumapili, Aaron Ramsey alifunga bao la sakika ya 56 na kuipa ushindi Arsenal ambayo ilitawala mchezo huo huku Ferguson akikiri kwamba walishindwa kuhimili vishindo licha ya mwanzo wa mchezo kutawala wao.Kwa matokeo hayo, Arsenal ipo nyuma ya vinara hao kwa pointi sita zikiwa zimebakia mechi tatu msimu huu na kocha Arsene Wenger amekata kusema kuwa amekata tamaa.
Nafasi yao ya ubingwa itaimarika endapo Chelsea itailaa United na Wenger ameeleza kuiunga mkono Chelsea chini ya Carlo Ancelotti Jumapili
Wenger anajifariji kuwa nao Samir Nasri na Cesc Fabregas katika mchezo ujao dhidi ya Stoke City. Nasri aliumia juzi huku Fabregas akiuguza paja.