Sija li discredit goli, ninacho sema lilikuwa ni kosa la kipa na si ufundi wa Ibra ulio sababisha goli. Tuna option mbili tuu
1.Mourinho afukuzwe.
Yeah najua mtasema mapema mnoo lakini mapema ndio vizuri, mou mpaka sasa hana kikosi cha kwanza, haja weza kufanya sub za maana, kashinda mechi chache sana, pia kumbuka chelsea walichelewa kumfukuza lakini haku improve, nadhan Mou wa kuanzia mwaka 2013, mpira ulisha anza kumpotea.
Mechi 11 za mwisho za Mou hizi
1-1, 1-1, 1-1 3-1, 0-0, 0-4, 0-0, 1-1, 4-1, 1-3 na1-2.
9 points out of a possible 33 ..... 27.3%
For now yeye ndio kocha mbovu kuliko wote tangu babu Alex astaafu.
.Au
2.Mou abaki lakin afanye yafuatayo.
-Pogba haja fiti kwenye timu atafute namna ya kumfanya afit ambayo ni kutafuta mfumo utakao muwezesha Pogba acheze na ma mido wa 2, ambao kati ya hao lazima mmoja awe na kasi mfano angalia alipo kuwa akicheza yeye, vidal na pirlo, mechi nyingi anazo cheza yuko slow si lazima acheze kama hafit kwenye mfumo au badilisha mfumo
-awatumie Basti na Schneiderlin, mechi nyingi tuu zimeonesha umuhim wao. Pia kuna madogo kama kina Tuanzebe na TFM awatumie, uzuri wa LvG tulikuwa tunafeli lakin at least unaona anatumia vijana. Huyu wa sasa hawatumii hao madogo na ana zidi kuboronga kuloko Sir LvG
-timu haina discpline na morali, ni kazi yake hiyo kufanya morali na nidhamu viwepo mfano. Angalia jinsi tulivyo fungwa magoli msimu huu kwa dakika.
Watford (83'+90'), Arsenal (89'), Everton (89'), Fenerbache (83'), Stoke (82') and Feyenoord (79').
Chelsea (1'), Fenerbache (2') and West Ham (2').
Timu ina onesha hapo ni no self-control, no discipline, no awareness, hili ni kosa lake awaande wachezaji wakabiliane nalo yeye ndio kiongozi.
-aache kuwapendelea Pogba na Ibra, anaweka matabaka, hasa Ibra hata leo ilitakiwa ibra apigwe sub, pia asiwa treat hao kama ndio wana stahili kupata game time kuliko wengine, kama ameweza kumuacha Blind na kuanza na Darmian alishindweje ku msub Ibra ambaye kuna Tym alichoka kabsa!? Matabaka yanavunja umoja.
-Mikhi ni mchezaj muhim amtumie vzuri kwa sasa hafanyi hivo bado.
Yako Mengi sana lakin hayo ni baadhi ya mambo ya kufanya la si hivo tutakuwa tunafungwa mpaka tuzoee.