Ndiyo maana nimekwambia unaleta stori za Mwanaspoti. Unaweza kuleta sources zinazoonyesha kwamba United ilikuwa ina mazungumzo na hao wachezaji? Sources zinazoonyesha kwamba United officially iliwa-approach hao wachezaji?
Unatumia tetesi za usajili kuongea mambo yasiyo na msingi. Kama ukiweza kuonyesha kwamba kulikuwa na official engagements kati ya Manchester United na hao wachezaji, basi nitakuomba radhi.
Sielewi unaelewa vipi maana ya neno ujuaji? Kwa hiyo wewe unachokifanya siyo ujuaji ama? Unatumia vigezo vipi kusema nafanya ujuaji na wewe hufanyi ujuaji?
Sasa mbona wakali kama Di Maria, Mata, Falcao n.k. walisajiliwa baada ya SAF? Na bila kusahau jinsi LvG alivyofanya juhudi za kumbakiza DDG.
Licha ya hao, United hawana sana falsafa ya kusajili established players. Inatokea nadra sana, kama unavyotaka kusema hapa. Ndiyo maana nakuuliza kama kweli unaifahamu timu unayoshabikia.