Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,382
- 10,951
Chifu, umemaliza kila kitu...umeitendea haki avatar yako, kwa kuzungumza kwa busara kubwa.Tatizo lako wewe unapenda ligi badala ya mjadala.Ukijua maana ya mjadala kwa maana ya kuelewa mambo utajifunza mambo mengi sana si sports hata uchumi,biashara,siasa.........Lipo tatizo hasa vijana wengi wanafikiri habari za Edo Kumwembe ndio habari za kinaa za michezo katika anga la kimataifa,au ukisoma Champion,Mwanaspoti basi umemaliza kila kitu hakika hakuna magazet ya hovyo kama hayo habari zao nyingi wanazichomoa majarida ya ulaya "Gossip" .Ukiwa na access ya internet sidhani kama ni busara kusoma magazeti ya aina hiyo.
Ukisoma habari ya Edo baada ya Man United kufungwa unaweza kuiweka kapu moja na maneno aliyokuwa akisema Mchg Mtikila katika uwanja wa siasa.Vimaneno au misemo ya uswazi isikutishe wala usione aibu kutamka mimi mnazi wa Man kisa misemo ya mitaani tena mara nyingi haina maana sana.
Vijana wanakuwa wavivu na kutegemea kupewa habari za 'kiuchambuzi' na akina Edo, Saleh Ally, Shafii n.k. wakati wana access na internet, inayoweza kuwapa habari zote za uhakika na ukweli. Mtu nimemwambia alete vyanzo vinavyoonyesha kwamba wachezaji hao anaosema wameikataa United walikuwa kwenye mazungumzo rasmi na timu, kakimbia.
Tusichoke kuwapa elimu na busara hawa vijana.