Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Inatisha sana ukipita asubuhi eneo la Kawe Stand na kukuta makundi ya vijana wakivuta bangi na kujidunga sindano za dawa za kulevya huku wakisindikiza na pombe na energy.
Inashangaza sana kwasababu kituo cha Polisi Kawe hakipo mbali na eneo lile, ni kama mita 250 hivi lakini vijana wale wanatumia dawa za kulevya bila kujificha.
Usiku hujibanza kwenye mabanda ya mama lishe na mabanda mengine yaliyo eneo hilo, kukikucha wakati hayo mabanda yakitumika kwa kazi za uzalishaji basi vijana wale husambaa mpaka kwenye uzio wa mabati ambako kuna mradi wa ujenzi wa nyumba za NHC na kutumia hizo dawa, japokuwa hawana shida na mtu lakini si salama maana vijana wetu hupita pale na kuwakuta hivyo inaweza kupelekea nao kutamani kugeza tabia hizo.
Nashauri tu mamlaka ziweze kuingilia kati suala hili ili kuokoa hicho kizazi kinachopotea.
Inashangaza sana kwasababu kituo cha Polisi Kawe hakipo mbali na eneo lile, ni kama mita 250 hivi lakini vijana wale wanatumia dawa za kulevya bila kujificha.
Usiku hujibanza kwenye mabanda ya mama lishe na mabanda mengine yaliyo eneo hilo, kukikucha wakati hayo mabanda yakitumika kwa kazi za uzalishaji basi vijana wale husambaa mpaka kwenye uzio wa mabati ambako kuna mradi wa ujenzi wa nyumba za NHC na kutumia hizo dawa, japokuwa hawana shida na mtu lakini si salama maana vijana wetu hupita pale na kuwakuta hivyo inaweza kupelekea nao kutamani kugeza tabia hizo.
Nashauri tu mamlaka ziweze kuingilia kati suala hili ili kuokoa hicho kizazi kinachopotea.