DOKEZO Tope kituo cha daladala Kawe ni Adha kubwa kwa abiria

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,115
Kituo cha daladala Kawe ni kero kubwa sana kwa watumiaji wa kituo hicho, Kituo hakina ukarabati wowote, iwe masika na kiangazi, hakuna nafuu, ikiwa kiangazi kituo kinapambwa kwa mashimo na mabonde hali inayoathiri magari na abiria pale wanapofika kituoni.

Kwa masika kama kipindi hiki ndio balaa zoto kabisa, kituo kinapambwa na madimbwi ya maji na matope maziito yalijazana kwenye yale mashimo yaliotengenezeka wakati wa kiangazi, matope yameoza yanatoa harufu kali, hakuna sehemu ya abiria kushuka wala kupanda, wanalazimika kupita kwenye tope kama kambale.

Mnaohusika na ukarabati wa kituo cha daladala Kawe mmelala usingizi wa pono wala hamna habari, huwa naona mnakusanya ushuru sijui hizo pesa mnapeleka wapi kama hata ukarabati haufanyiki, basi kama mmeshindwa kukarabati mngepanda mpunga maana tope lile mngevuna magunia ya mpunga wa kutosha mkapata faida si mmeamua stendi iwe majaruba ya mpunga bwana.

Mbaya zaidi Kawe ilipata mbunge aliyejinasibu kwa kuwapeleka wana Kawe Marekani na kuleta Treni ya umeme cha ajabu Stendi tu ya Kawe imemshinda kuisemea ikafanyiwa ukarabati au kwa kuwa yeye haitumii ivyo sio kipaumbele kwake?

1682054974819.jpeg


1682055028046.jpeg

1682055047362.jpeg

1682055069797.jpeg

1682055111703.jpeg

1682055162257.jpeg

 
Njia ya kuingilia kituoni mbaya sana, magari yanagonga chini. Ajabu ni kuwa palimwagwa moramu 2020 Hayati Magufuli alipokuja kufanya mkutano wa 'Nileteeni Gwajimaaaaaa'

Nikajiuliza ina maana mkutano wa siku moja wa CCM ni muhimu kwamba magari yao yapite vizuri yasigonge chini, kuliko maelfu ya wananchi wanaotumia hicho kituo kila siku.
 
HUU USAFIRI NI WA SISI WACHOVU,WAJINGA TU
NDOMANA HAKUNA ANAYE JALI
KUBORESHA UPANDE WA USAFIRI HUO KIUJUMLA
MAANA KWANZA WAHUSIKA HAWATUMI USAFIRI HUO
HAWAPATI ADHA YOYOTE WAO
NYIE/SISI TUPAMBANENI NA HALI ZETU,
HUMU UTASIKIA MALALAMIKO TU KUHUSU USAFIRI WA DALADALA NA MWENDOKASI...
KUNA MTU MWINGINE NAYE KALETA UZI ANASEMA STENDI MBEZI MWISHO INANUKA MIKOJO !

ova
 
Wameangalia weee wakaona watu wenyewe wanaoishi Kawe Ni wachovuwachovu wanaolala kwa Mwamposa pale chini kwenye nyasi wakaamua waachane nao .Hivi Kuna hata Meya anayeishi Kawe?
 
Kituo cha daladala Kawe ni kero kubwa sana kwa watumiaji wa kituo hicho, Kituo hakina ukarabati wowote, iwe masika na kiangazi, hakuna nafuu, ikiwa kiangazi kituo kinapambwa kwa mashimo na mabonde hali inayoathiri magari na abiria pale wanapofika kituoni.
Kawe miaka yote hakuna sitendi mwanzo magali yakipakilia Ukwamani wakatoa huko na kuyaleta pekasi kwa kisingizio heti wanataka kujenga sitendi wanakofanyia mikutano warokole ikawa nitolee mpaka leo
 
Back
Top Bottom