Mambo ya kuzingatia unapokula Pweza na Ngisi njiani

Ni kweli kabisa mkuu sio salama, lakini kukwepa hiyo ishu ni ngumu sana.

Kwanza muda, hapo unaposema jamaa azioshe kwa uzuri hizo bakuli na wateja wanamsubiri ni ishu sana mzee, kuna wateja watachoka kusubiri atawapoteza.

Pili mkuu ni hasara kutumia izo stick hovyo hovyo namna hiyo na kwa njia hiyo atachafua vyombo vingi na muda wa kuosha hana achilia mbali kununua hizo stick mara kwa mara.
Jamaa yako huyo atajirekebisha kwa mambo machache tu mengi utakuta kama yalivyo.
Hakika.
 
Leo muda wa jioni nilikuwa maeneo ya Mbezi ya Kimara nilikuwa nimesimama namsubiri rafiki yangu pembeni kwa mbele kulikuwa na mtu anauza supu ya pweza na vipande vyake na ngisi na kachori.Nikiwa pale walikuja watu kadhaa kununua nilichokiona.

Mteja alikuwa anachukua kijiti cha kuchomea anatoboa mmoja anachovya kwenye pilipili kisha anaweka mdomoni hii ilikuwa ni inajirudia mwingine akawa akishaweka mdomoni anatoboa na kijiti chake kile kile kipande cha pweza anaona sio kikubwa anavyotaka anakisogeza anatafuta kitakachomvutia, kwa kijiti kile kile ambacho tayari alikuwa anakitoa mdomoni, Ilibidi kuongezea umakini wangu eneo lile nikiwaza mimi pia nakulaga vitu hivi akaja mtu akawekewa supu akamaliza akarejesha kibakuli muuzaji akakirusha kwenye ndoo ndogo pembeni uliyokuwa na maji nusu, wakaja watu kadhaa inaonekana tayari alikuwa ni mtu mwenye wateja wake vizuri, baada ya vibakuli kadhaa kujumuika kwenye ndoo akavichovya chovya kwa kuzungusha kwenye ndoo akavikumuta akaweka mezani, walikuja watu wa rika zote pale na jinsia tofauti, niliumia moyoni maana niliwaza afya zao nilisubiri watu wapungue kisha nikamfwata akiwa mwenyewe Muuzaji anangoja wateja nikamweleza Kuna mapungufu nayaona mkuu alipoona nazungumza naye kirafiki alinisikiliza.

Mwishowe nikampa mambo ya kuzingatia

1.Vyombo unavyotumia vioshe na sabuni kisha visuuze vyema na uweke maji ya moto ukiweza nilimwonyesha vyombo alivyoviweka mezani kutumika vikiwa na mafuta mafuta.

2. Nikamweleza unapoweka mtu kuchoma waambie ukitoboa ukaweka mdomoni kitupe hicho uchukue kijiti kingine.

3. Kuepuka suala la mtu kuchovya kwenye pilipili kuweka mdomoni kisha kutumia kijiti hicho anachovya tena kwenye pilipili wawekee visahani mtu ajichukulie pweza wake na kachori au ngisi wake kisha mimina pilipili yake atumie kuepuka mwingiliano sana na contamination.

Alinishukuru maana sikuonesha kumkaripia wala kuonyesha hisia zangu nilivyoumizwa na jamaa akaniambia ww umenishauri vyema.

Wito wangu kwa ndugu tunaokula vitu barabarani wapo wengine wanaenda kununua mahindi ya kuchoma analishika hili analiacha analishika tena lingine wewe ukija unaweka mdomoni tu bila kuzingatia afya yako na lingine linakuwa pembeni lishapoa muuzaji analipasha kishkaji anakupa, yakupasa kuwa makini usijekupata minyoo Njiani, au kuhara au kuumwa tumbo au Hata uviko-19 kirahisi kupitia kula sehemu ambazo hawazingatii usafi na afya pia wauzaji wa vitu hivi nawasihi kuongeza usafi na ustarabu.

Niishie hapo natumaini wengi watabadilika kama brother niliyemshauri leo, Mbezi ya kimara.
Nawatakia biashara njema katika kujitafutia kipato.
Mkuu, kama ni wizara basi weye wafaa kusimamia biashara ndogondogo.

Hizi biashara zikipangwa uzuri wajasiriamali wadogo wanatoboa.

Ni mipango tu na usimamizi mzuri.

Pale Mbezi Kimara ni eneo zuri sana likipangwa kwa mpangilio wa kitaalam.
 
Leo muda wa jioni nilikuwa maeneo ya Mbezi ya Kimara nilikuwa nimesimama namsubiri rafiki yangu pembeni kwa mbele kulikuwa na mtu anauza supu ya pweza na vipande vyake na ngisi na kachori.Nikiwa pale walikuja watu kadhaa kununua nilichokiona.

Mteja alikuwa anachukua kijiti cha kuchomea anatoboa mmoja anachovya kwenye pilipili kisha anaweka mdomoni hii ilikuwa ni inajirudia mwingine akawa akishaweka mdomoni anatoboa na kijiti chake kile kile kipande cha pweza anaona sio kikubwa anavyotaka anakisogeza anatafuta kitakachomvutia, kwa kijiti kile kile ambacho tayari alikuwa anakitoa mdomoni, Ilibidi kuongezea umakini wangu eneo lile nikiwaza mimi pia nakulaga vitu hivi akaja mtu akawekewa supu akamaliza akarejesha kibakuli muuzaji akakirusha kwenye ndoo ndogo pembeni uliyokuwa na maji nusu, wakaja watu kadhaa inaonekana tayari alikuwa ni mtu mwenye wateja wake vizuri, baada ya vibakuli kadhaa kujumuika kwenye ndoo akavichovya chovya kwa kuzungusha kwenye ndoo akavikumuta akaweka mezani, walikuja watu wa rika zote pale na jinsia tofauti, niliumia moyoni maana niliwaza afya zao nilisubiri watu wapungue kisha nikamfwata akiwa mwenyewe Muuzaji anangoja wateja nikamweleza Kuna mapungufu nayaona mkuu alipoona nazungumza naye kirafiki alinisikiliza.

Mwishowe nikampa mambo ya kuzingatia

1.Vyombo unavyotumia vioshe na sabuni kisha visuuze vyema na uweke maji ya moto ukiweza nilimwonyesha vyombo alivyoviweka mezani kutumika vikiwa na mafuta mafuta.

2. Nikamweleza unapoweka mtu kuchoma waambie ukitoboa ukaweka mdomoni kitupe hicho uchukue kijiti kingine.

3. Kuepuka suala la mtu kuchovya kwenye pilipili kuweka mdomoni kisha kutumia kijiti hicho anachovya tena kwenye pilipili wawekee visahani mtu ajichukulie pweza wake na kachori au ngisi wake kisha mimina pilipili yake atumie kuepuka mwingiliano sana na contamination.

Alinishukuru maana sikuonesha kumkaripia wala kuonyesha hisia zangu nilivyoumizwa na jamaa akaniambia ww umenishauri vyema.

Wito wangu kwa ndugu tunaokula vitu barabarani wapo wengine wanaenda kununua mahindi ya kuchoma analishika hili analiacha analishika tena lingine wewe ukija unaweka mdomoni tu bila kuzingatia afya yako na lingine linakuwa pembeni lishapoa muuzaji analipasha kishkaji anakupa, yakupasa kuwa makini usijekupata minyoo Njiani, au kuhara au kuumwa tumbo au Hata uviko-19 kirahisi kupitia kula sehemu ambazo hawazingatii usafi na afya pia wauzaji wa vitu hivi nawasihi kuongeza usafi na ustarabu.

Niishie hapo natumaini wengi watabadilika kama brother niliyemshauri leo, Mbezi ya kimara.
Nawatakia biashara njema katika kujitafutia kipato.
Mimi nikikuta muuza chakula ana toothpick mdomoni naghairi kula hata niwe na njaa kali kiasi gani
 
Unapata huduma kwa kadri unacholipia, ukitaka usafi inabidi uende huko kwenye migahawa na hoteli kubwa nunua sea food platter...hizi za mtaani huwezi kukwepa mapungufu madogo madogo kama hayo
Mkuu huko five star ndio watu wanakula vibovu kabisa
 
Leo muda wa jioni nilikuwa maeneo ya Mbezi ya Kimara nilikuwa nimesimama namsubiri rafiki yangu pembeni kwa mbele kulikuwa na mtu anauza supu ya pweza na vipande vyake na ngisi na kachori.Nikiwa pale walikuja watu kadhaa kununua nilichokiona.

Mteja alikuwa anachukua kijiti cha kuchomea anatoboa mmoja anachovya kwenye pilipili kisha anaweka mdomoni hii ilikuwa ni inajirudia mwingine akawa akishaweka mdomoni anatoboa na kijiti chake kile kile kipande cha pweza anaona sio kikubwa anavyotaka anakisogeza anatafuta kitakachomvutia, kwa kijiti kile kile ambacho tayari alikuwa anakitoa mdomoni, Ilibidi kuongezea umakini wangu eneo lile nikiwaza mimi pia nakulaga vitu hivi akaja mtu akawekewa supu akamaliza akarejesha kibakuli muuzaji akakirusha kwenye ndoo ndogo pembeni uliyokuwa na maji nusu, wakaja watu kadhaa inaonekana tayari alikuwa ni mtu mwenye wateja wake vizuri, baada ya vibakuli kadhaa kujumuika kwenye ndoo akavichovya chovya kwa kuzungusha kwenye ndoo akavikumuta akaweka mezani, walikuja watu wa rika zote pale na jinsia tofauti, niliumia moyoni maana niliwaza afya zao nilisubiri watu wapungue kisha nikamfwata akiwa mwenyewe Muuzaji anangoja wateja nikamweleza Kuna mapungufu nayaona mkuu alipoona nazungumza naye kirafiki alinisikiliza.

Mwishowe nikampa mambo ya kuzingatia

1.Vyombo unavyotumia vioshe na sabuni kisha visuuze vyema na uweke maji ya moto ukiweza nilimwonyesha vyombo alivyoviweka mezani kutumika vikiwa na mafuta mafuta.

2. Nikamweleza unapoweka mtu kuchoma waambie ukitoboa ukaweka mdomoni kitupe hicho uchukue kijiti kingine.

3. Kuepuka suala la mtu kuchovya kwenye pilipili kuweka mdomoni kisha kutumia kijiti hicho anachovya tena kwenye pilipili wawekee visahani mtu ajichukulie pweza wake na kachori au ngisi wake kisha mimina pilipili yake atumie kuepuka mwingiliano sana na contamination.

Alinishukuru maana sikuonesha kumkaripia wala kuonyesha hisia zangu nilivyoumizwa na jamaa akaniambia ww umenishauri vyema.

Wito wangu kwa ndugu tunaokula vitu barabarani wapo wengine wanaenda kununua mahindi ya kuchoma analishika hili analiacha analishika tena lingine wewe ukija unaweka mdomoni tu bila kuzingatia afya yako na lingine linakuwa pembeni lishapoa muuzaji analipasha kishkaji anakupa, yakupasa kuwa makini usijekupata minyoo Njiani, au kuhara au kuumwa tumbo au Hata uviko-19 kirahisi kupitia kula sehemu ambazo hawazingatii usafi na afya pia wauzaji wa vitu hivi nawasihi kuongeza usafi na ustarabu.

Niishie hapo natumaini wengi watabadilika kama brother niliyemshauri leo, Mbezi ya kimara.
Nawatakia biashara njema katika kujitafutia kipato.
Angalizo zuri. Watu wengi wanaambukizana magonjwa ikiwemo ugonjwa wa homa ya ini kwa njia kama hizi. Tuchukue tahadhari
 
Back
Top Bottom