Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

- Mukama a great man and good leader, one of CCM's long time behind the scene propangandists, loongtime Chuo cha Kivukoni, my very close loongtime friend, and with Kinana it means only one thing, the end of Mafisadi.

- Alikuwa ni Mukama, aliyegundua ubadhirifu wa ajabu sana uliofanywa Jiji na kumuarifu Rais no wonder aliyetoka huko mlo ukaisha! This is great change for CCM, isipokuwa ni mapema sana kutabiri what it means to Taifa, lakini with Kinana ninaamini this to be the end of Mafisadi.


FMeS!

Mkuu FMES; Kung'oa ufisadi ccm ni kazi ngumu ambayo ni muujiza kufanywa na mtu aliye ndani ya CCM!

Hata ukija na nia yako nzuri, ni vigumu kubadili kitu ambacho wengi wa viongozi wanakiona kama njia sahihi....!

 
quote_icon.png
Originally Posted by myhem
Hivi huyo Meghji anapendewa nini? mbona anabebwa sana?



Habebwi na mtu, huombwa na kuangukiwa, ni mchapa kazi sana, na kichwa, wacha. Waulize wanaomjuwa. Si mwanamke wa kawaida.

Tupe tafsiri nzuri za hayo maneno kwenye nyekundu, kwani huyo mama anasifa chafu na njia zake za kupata uongozi, wanashindana na Sofia Lion wekundu wa msimbazi.
(Kamuozesha mwanae kwa kilaza) ili aendelee kuheshimiwa akiwa anaenda kwao visiwa vya Commoro. Wanaomjua zaidi ni Mzee Ruksa Aliyemlea (Ungeweka Neno Kumfahamu sababu Kumjua lina maana ya Kujamiiana)

Sitoshangaa kuja kusikia Binti wa megji anapewa ubunge wa viti maalum. kutokea bagamoyo...
 
Baada ya kikao, RA alisema "They won the battle but the fight is still on"

Naitafsiri kauli hii Kama RA haoni wa kumtisha, anajua anachotarajia au anachotaka kufanya karibuni.

mkuu mi naona huyu bwana atakua na siri nzito za mkuu wa kaya na za chama pia,so wakimwaga mboga(wakimchomoa)yy atamwaga ugali(atamwaga siri hadharani).Movie ndo kwanza inakaribia patamu
 
Kuna ukweli katika hili kwani akiwa Mkruguenzi wa Jiji nilipambana naye katika kesi ya jalala la Vingunguti. Alikuwa anatubeza sana na alikuwa haoni kama Jiji lilikiuka sheria kuanzishwa jalala pale. Lakini alikutana na watu wasiogopa na tulieweza kupata amri ya kufungwa kwa Jalala hilo la Vingunguti. Na jinsi nilivyomsikia mwaka jana wakati wa mchakato wa uchaguzi ni wazi kuwa Makamba ni mwanafunzi katika ubishi huyu jamaa ana tabia kama ya Stephen Wassira. Hivyo ubabe utaongezeka na CCM sasa inafanya kazi ya kujizika.

...la kuvunda, halina ubani. tunahesabu siku tu.
 
kwa sisi wakurya akuna kabila tunalo dhalau kama la akina mukama kwa sifa yao ya kwanza wanaingoza kwa umbea na kuchukua maneno hapa na kuyapeleka pale na kama mnabisha tutakuja kulizungumza hapa jf tena juu ya huyu bwana atakavyo zidi kukiangusha chama fisadi, nawakilisha
 
Yaani wamemtosa mzee Yusufu baada ya kuwafanyia kazi nzuri waliyomtuma aifanye ya kuanzisha ccm B iliyompamba JK kwa mbinu chafu za kuwachafua akina salim, sumaye nk? ama kweli ccm hawana shukrani. kama ni kuondoka, ilitakiwa mwenyekiti aonyeshe njia ndipo yusufu, aziz, andrea vijisenti, chiligati, tambwe, edward, kingunge, pius, kawambwa, sophia, ghasia, mkulo, stefano wassira, nchimbi, beno nk, nk nao wafuate.

Pole sana mzee wetu yusufu, vumilia tu maana hata akina kolimba na mangula nao yaliwakuta. hii ndiyo ccm yetu!
 
kwa sisi wakurya akuna kabila tunalo dhalau kama la akina mukama kwa sifa yao ya kwanza wanaingoza kwa umbea na kuchukua maneno hapa na kuyapeleka pale na kama mnabisha tutakuja kulizungumza hapa jf tena juu ya huyu bwana atakavyo zidi kukiangusha chama fisadi, nawakilisha

Eghaki Mura!! Ukabila wa nini tena!?
 
chomete;kwa sisi wakurya akuna kabila tunalo dhalau kama la akina mukama kwa sifa yao ya kwanza wanaingoza kwa umbea na kuchukua maneno hapa na kuyapeleka pale na kama mnabisha tutakuja kulizungumza hapa jf tena juu ya huyu bwana atakavyo zidi kukiangusha chama fisadi, nawakilisha

St.p.d and irrational argument----crap minded



 
Mkama akishirikiana na Profesa aliyefahamika kwa jina moja la Luhanjo, ndiyo waliofanya tathmini ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na kupendekeza kwamba lazima baadhi ya wanachama watoswe kuokoa chama hicho. Inadaiwa kuwa miongoni mwa ajenda za kikao hicho ni kujivua gamba ambayo hatua ya kujiuzulu kwa sekretarieti na kamati kuu ni utekelezaji wake.

Inadaiwa kwamba kujiuzulu kwa Kamati Kuu kulitokana na mvutano wa wajumbe ambao walionyesha kugawanyika, huku kundi moja likitaka Mbunge wa Igunga na Mjumbe wa CC, Rostam Aziz, Mbunge wa Bariadi Mashariki na mjumbe wa kamati hiyo, Andrew Chenge wajiuzulu na jingine likipinga.

Baada ya mvutano mkali wa wajumbe hao na kuchukua muda mrefu, inadaiwa Rais Kikwete aliilazimisha kamati nzima kujiuzulu. Awali, ilidaiwa kuwa ajenda hiyo ya kuwataka wajumbe hao wawili wajiuzulu ingewasilishwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu, huku kundi linalodaiwa kupinga ufisadi likitaka wafukuzwe uanachama.
 
kuna mtu anapingana na wewe, anasema Kinana ni mtu anayependa pesa sana, na hajali anatumia njia ipi kuipata!

- Well, sawa sawa mkuu, lakini ninavyojua ni kwamba amekuwa mstari wa mbele sana kuwapinga mafisadi ndani ya chama so ninaamini kwamba between yeye, Nape na Mukama ambaye originally ni mtu wa Mwalimu ni kwamba:- 1. Mbio za mafisadi na Urais hapa zimefika mwisho 2. CCM imejiokoa big time na 2015 3. Huu ndio mwisho wa UV-CCM na ndoa yao na mafisadi 4. Sasa CCM itaanza ku-reasonate na wananchi tena baada ya kuwa njia panda nao kwa muda mrefu sana. 5. Mabadiliko haya ni ushindi mkubwa sana kwa Wapiganaji wa CCM hasa Six, sasa ni wakati wao wa kuingiza idea zao ndani ya Chama.

- However: Ni mapema mno kusema nini msalahi ya taifa katika haya mabadliko, na pia Wapiganaji wanatakiwa kujipanga vizuri bila ya kuanza tamaa ya madaraka, maana 2015 politically bado ni mbali sana, Mafisadi hawawezi kuingia Upinzani, sio siri kwamba kuna watakaorudi CC lakini nguvu sasa imeisha, according to the dataz za kikaoni walioshutumiwa sana ni Rostam, Chenge na Makamba, el hakuguswa kabisa, meaning kwamba alishajua mapema na kuweka amani ya siasa na kundi liloshinda hapa na one more political mistake he is done!

- All and all, politically the big winner wa all this ni bm na 6 na mbio za 2015!


FMeS
 
- According to the dataz toka kikaoni, Wajumbe toka Visiwani wanataka mafisadi wote waondolewe katika chama na wavuliwe ubunge pia!, Vuta nikuvute mpaka usiku lakini haikupatikana muafaka sasa kesho tena!

- Je Nape kupewa ubunge na Rais? IDodomyaaaaa!aghhhrrrrrrr I loove it!


FMeS!
 
Mie sioni na sijui kwanini EL aliekubali kujiuzulu bado mna mfuata fuata, kuna mijizi mingi bado imo humo ndani wala hamuwasemi!!!
Edward Lowassa ni BORA mara millioni Trillioni zaidi ya wengi waliomo CCM, mtabisha lakini ukweli mnaujua na upo wazi.

EL was getting things DONE.... Mnataka kuwa na viongozi legelege wanaolalamika kama sisi wananchi tulio vijijini?
Mnataka viongozi wasio na MENO?, EL tayari ana hela kaiba au hakuiba haijalishi...ataingia kuchapa kazi ndo alichobakisha.

Jaribuni ku focus kwenye real issues zilizopo na sio kumwandama asiyekuwepo hata kwenye system!

Wenzako wameshindwa kumsafisha, wewe utaweza? Analaana ya mtu aliyekufa huyo!
 
Mie sioni na sijui kwanini EL aliekubali kujiuzulu bado mna mfuata fuata, kuna mijizi mingi bado imo humo ndani wala hamuwasemi!!!
Edward Lowassa ni BORA mara millioni Trillioni zaidi ya wengi waliomo CCM, mtabisha lakini ukweli mnaujua na upo wazi.

EL was getting things DONE.... Mnataka kuwa na viongozi legelege wanaolalamika kama sisi wananchi tulio vijijini?
Mnataka viongozi wasio na MENO?, EL tayari ana hela kaiba au hakuiba haijalishi...ataingia kuchapa kazi ndo alichobakisha.

Jaribuni ku focus kwenye real issues zilizopo na sio kumwandama asiyekuwepo hata kwenye system!

Hakuna binadamu anayetosheka na hela. Yaan unataka tuamini kwamba kwakuwa ana hela basi hatatafuta zingine hata kwa njia zisizo halali
 
Una uhakika gani kama Zakia sio muadilifu, kuna ushahidi wo wote? Usilete ya Kagoda maana she was not involved.

Mbona sio siri kama unafuatilia mijadala ya hapa JF utafahamu hilo. BTW kuna wakongwe hapa naona wamekupa thanks lakini wanaufahamu ukweli. Kwani hata JK mwenyewe si ndio papa lenyewe au mnataka lugha ghani? Zama za ukweli ndio hizi na ukweli utawaokoa Chichiemu.
 
Hizi siasa za ccm kaazi kweli. Nyoka hata ajivue gamba anabaki kuwa nyoka tu. Kama wana nia ya dhati, serikali ya ccm iwachukulie hatua za kisheria hao wote wanaotuhumiwa. Vinginevyo ni sawa na kibaka anayefukuzwa na raia halafu ajaribu kujificha katikati ya uwanja wa mpira!! HATUDANGANYIKI.

Hizi kelele ni za kila siku utamchukuliaje hatua JK na genge lake la mafisadi wakati wao ndio wamebeba dhamana kinyemela? Its a big question and no one dares to ask? Rejea wizi wa kura wakati wa uchaguzi na mgogoro ambao bado unatokota kule Arusha. Then hujaongelea mambo ya Dowans etc.
 
Back
Top Bottom