Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Watu wanachooonga!uongozi ni wa ccm sio wa serikali na km wewe sio mwana ccm pilipili usio ila yakuwasha niii?
 
Nina wasiwasi sana na nia ya Kikwete katika kuisafisha CCM kama kaondoa akina Makamba wanaojua mipasho tu bila kuwa na chembe ya ujuzi wa ufisadi isipokuwa ule wa kukatiwa, na kumleta Kinana ambaye ni mjuvi sana wa kusuka ufisadi; mtu aliyewahi kusema eti "meli ni yangu lakini shehena ya pembe za ndovu siijui!". Hapa naona kama vile kikwete anajaribu kuchota maji ya kuisafisha CCM kwa kutumia gunia, siuji kama atafika kweli. Bado mimi naiona CCM kama radioactive ambayo half-life yake ni fupi sana; mwaka 2015 unaweza kuwa ni mbali sana kabla CCM haijamaliza uhai wake labda CDM ivurunde. Akina makamba na wote walioenguliwa ama watapewa nafasi nyingine na hivyo kuendelea kutunza uozo, au watatupwa nje kabisa ya system, na hivyo kuwapa mwanya wa kuanza kuitupia madogo ya kuimaliza kabisa CCM hiyo.
 
Asante mkuu kwa taarifa ila wafie mbali hawa jamaa hawana dhamira ya kweli kumsaidia mtanganyika wa kawaida!
 
Ccm wamefanya kazi kubwa kumteua Mkama ambaye hakutegemewa sana. Naamini hii surprise element italeta mabadiliko makubwa ndani ya ccm. Na hiyo itasaidia maendeleo ya nchi
 
ccm sikio la kufa, solution sio Mukama, mwenyekiti wao ndugu Jk ndio tatizo kuu aka janga la chama, hana maamuzi, msimamo wala mtazamo. Atoke yeye ccm wajijenge!
 
Obama alisema "You can put lipstick on a pig, but it's still a pig"
WanaCCM go figure...
 
Mukama katulia sana alikuwa utendaji wake si wa kubwabwaja ni msomi anapenda kujibu hoja alikuwa JIJI THEN katibu mkuu afya then katibu mkuu maji mpaka akastaafu.akateuliwa na rais kuwa mkurugenzi wa bodi habari.na amehusika sana kutunga ilani ya ccm 2010-2015 hivyo watu wenye bongo zao wanarudi chamani pia ni mtu wa system.

Una maana gani kwa kusema ni mtu wa system? Mwizi, fisadi, au nini?
Huko kote amefanya nini kuleta mabadiliko?
 
Are you serious? Kuna wanaojali watanzania ndani ya hili shirika la majasusi? Pole kwa kuwa na hope ya ccm na ufisadi wao. Jitihada zako elekeza mahali unapojua kuna hope sio ulioyaona. Hujui historia ya ccm na unamategemea itatoka shimoni ili wakutawale tena. Please man.
Mkuu Niweze, umegubikwa na ugonjwa unoitwa "u-coconut" kwa chama chako.Hata madudu yake huyaoni wala husikii, ni kama mtu aliye katika mapenzi.Hata hivyo vyama vingine vimetoa changamoto nzuri sana na hatimaye CCM kuamka toka usingizi wa pono.
Shirika la kijasusi ni lipi hilo tupe mifano.
Kwa misingi ya real-politik CCM ipo na itakuwepo.Wengi wetu tuliikandia pale inapobidi kwa nia ya kusahihisha yale madudu yaliyomo ndani yake.Kufikiri kuwa kitaondoka hivi karibuni au kufa is far fetched.Uzuri wa mfumo CCM wanaweza kujisahihisha bila chama kufa, tofauti na vyama vingine.
Kwa taarifa yako sisi wengine tunaifahamu CCM toka pengine hujazaliwa!!!!
 
A. KINANA - MAKAMU MWENYEKITI.

MR. MUKAMA - KATIBU MKUU.

NAPE NAUYE-ITIKADI NA UENEZI,AFADHALI.

KUNA KITU NINACHOKIONA HAPA AMBACHO NI WOGA WA KUFA....YANI KAMA VILE MTU ALIYEDUMBUKIA KWENYE MAJI ASIYEONA PA KUJISHIKA,HIYO NDIYO CCM NIIONAYO MIMI BUT I NEED UR MAWAZO.:redfaces:
 
Kiukweli methodman; jk sasa ameanza vizuri kwa kuukubali ukweli wa mambo, kwamba ufisadi upo chamani! Huwezi kumuadhibu mtoto wa jirani aliyekuibia shati na ukashindwa kumuadhibu mwanao aliyekuibia gari. Sasa nina matumaini jk ameamua. Nauye poa, lakini mukama simfahamu vizuri siwezi ku-comment kitu kwake. Kinana!!!pia naye si strong!!!!! Sasa sijui itakuwaje. Mimi najua jk anawafahamu vizuri watu wake; ninachomuomba asifanye makosa tena.
 
Wilson Mukama ni mkorofi na mkali ila sijui kama ukorofi wake na ukali utasaidia kuwakemea na kuwatisha mafisadi
 
Mwanajf, kuna taarifa zimenifikia hivi punde zikisema kuwa Mhe.Samuel Sitta amepita katika mchakato wa kuwa Katibu Mkuu wa CCM kuchukua nafasi ya Bw.Makamba.Uamuzi wa kumchukua Ndugu Sitta umetokana na umahiri wake katika kupiga vita ufisadi na pia uzalendo alionao kwa nchi yake.Itakumbukwa alipo kuwa Spika wa Bunge aliweza kuliendesha Bunge kwa "Speed and Standards",kitu ambacho kilimfanya akubalike hata kwa wananchi wa kawaida.
Lakini pia uteuzi huo utakifanya chama hicho kupata Katibu Mkuu Mtendaji ambaye atavunja makundi yaliyopo ndani ya chama hicho hivi sasa.Sitta amefanikiwa kuwadondosha makada wenzake kama Jaka Mwambi,Wilson Mukama n Lukuvi.
 
wacha ninywe diclopar ... mnatuchangaya ...
 
Which is which? Jana tuliambiwa Mukama ndio katibu mkuu mpya, leo ni Six!! confirm kwanza basi ndipo mtuwekee hapa jamvini.
 
Mwanajf, kuna taarifa zimenifikia hivi punde zikisema kuwa Mhe.Samuel Sitta amepita katika mchakato wa kuwa Katibu Mkuu wa CCM kuchukua nafasi ya Bw.Makamba.Uamuzi wa kumchukua Ndugu Sitta umetokana na umahiri wake katika kupiga vita ufisadi na pia uzalendo alionao kwa nchi yake.Itakumbukwa alipo kuwa Spika wa Bunge aliweza kuliendesha Bunge kwa "Speed and Standards",kitu ambacho kilimfanya akubalike hata kwa wananchi wa kawaida.
Lakini pia uteuzi huo utakifanya chama hicho kupata Katibu Mkuu Mtendaji ambaye atavunja makundi yaliyopo ndani ya chama hicho hivi sasa.Sitta amefanikiwa kuwadondosha makada wenzake kama Jaka Mwambi,Wilson Mukama n Lukuvi.

peleka kwenye magazeti ya udaku hiyo taharifa
 
Wilson Mukama ni mkorofi na mkali ila sijui kama ukorofi wake na ukali utasaidia kuwakemea na kuwatisha mafisadi

JF mark my words, kama Mkama atakuwa katibu mkuu wa ccm, kazi ya kuondoa ccm madarakani ni nyepesi kama kuua tembo kwa kutumia bua.

Alihamishwa wizara ya afya kwenda maji kutokana na ufisadi na ufujaji aliofanya wizara ya afya. Ni mropokaji balaa hashauriki. Hushambulia mtoa hoja siyo hoja.
 
hata siku moja sitta hawezi kuwa katibu mkuu
 
Back
Top Bottom