Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Walifuta 'Jambo Forums' tunapeta na 'Jamii Forums' na wakifanikiwa kuifuta 'Jamii Forums' tutaibuka na 'Jiamini Forums' ilmradi JF haifi! Itakuwa inapitia tu hatua mbalimbali za kukua na kuimarika zaidi.
 
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga, amewaeleza wabunge kuwa, mmiliki wa mtandao wetu wa jamii forum anaweza kuwa Mtanzania au si Mtanzania.

Ameyasema hayo bungeni mjini Dodoma wakati anajibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Getrude Lwakatare (CCM).

Mbunge huyo amedai kuwa, Mtandao huo umekuwa ukisambaza habari za uongo kwa watu mbalimbali na haujachukuliwa hatua hivyo alitaka kumfahamu mmiliki wa mtandao huo.

Kitwanga amesema, uanzishwaji wa tovuti za kijamii haulazimishi mtu kujisajili wala kujitambulisha , na huanzishwa na mtu yeyote popote duniani.

"Kutokana na asili na miundo ya tovuti za kijamii, mamlaka haisajili wala kutoa leseni kwa tovuti hizo, kimsingi maudhui yanayoadikwa katika tovuti hizo za kijamii ni maoni binafsi ya watu yasiyoangaliwa iwapo ni ya kweli au la" amesema Kitwanga.

Baada ya Mbunge wa Viti Maalum, Hilda Ngoye (CCM) kuuliza swali la nyongeza, wakati Kitwanga anajiandaa kumjibu, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimtaka kiongozi huyo wa Serikali, ajibu hasa swali kuhusu ' Jamii Forum na matatizo yake makubwa'
Ngoye amedai kuwa, baadhi ya mambo yanayoandikwa kwenye mtandao wa Jamii Forum yana madhara katika jamii yakiwemo matusi ya nguoni na ni kinyume cha utamaduni wa Mtanzania.

Aliuliza kama Serikali ipo tayari kuwasilisha bungeni muswada , Bunge litunge sheria ili mtandao huo uache kuandika mambo ya maudhi na uchochezi.

Alitaka pia kufahamu kama Serikali ipo tayari kuwasilisha bungeni muswada ili Bunge litunge sheria itakayozuia watoto kusoma ‘mambo machafu' kwenye ‘internet café' vikiwemo vitendo vya ngono.

Kitwanga amesema, suala la kudhiti mitandao ya kijamii litakuwa kwenye Muswada wa Sheria ya Habari.

Amesema, suala la maadili ya watoto ni jukumu la wazazi, na kwamba ndiyo wanaowapa fedha za kwenda ‘Internet café'.

Amesema, kutokana na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, kuna namna nyingi zinazowawezesha watoto kuona ‘mambo yasiyofaa' zikiwemo simu za mkononi, ipad, na laptops.

Amesema ni wajibu wa wazazi kuhakikisha kuwa watoto wao wanakua kwa mujibu wa maadili ya taifa.

...Huyu Charles Kitwanga amefanya tofauti na mawaziri wetu wengi (kwa mfano H.Mponda) ambao wanaleta siasa hata katika mambo yanayohitaji majibu ya kitaalamu. na huyu Ndugai kilaza kweli; haelewi hata maana ya "user generated content" sijui alitarajia waziri aseme nini kuhusu hicho anachokiita jamii forum na matatizo yake makubwa.
 
baadala ya kujadili hoja za msingi za kimaendeleo wameanza kuingilia mpaka kwanye maisha yetu ya kujuzana habari na mijara ,wangejua kwamba jamiiforum inasaidia kiasi gani katika maswala kimaendeleo, wala wasingefikiria hata hilo wazo ,watu tunapata elimu na kusaidia katika maswala ya kamaendeleo
 
Mama rwakatare hivi anajua hata matumizi ya mtandao? Manake ukisema usajili blogs zote, mbona kutakucjhwa?
 
Ni fedheha kuwa mtu mwanadamu then ukawa mwana CCM ni aibu sana .Ndugai ni mtupu hamkujua ?Anajipendekeza tu huyu opportunist .JF inawachoma sana wanaiogopa zaidi ya kitu chochote .Hapa tupo kubakia hakuna kutetereka .
 
Kwa nafasi yake ya uongozi, Mama Lwakatare ilitakiwa atambue mapema kabisa, nini maana ya dhana ya "freedom of speech". Katiba ya sasa ya Tanzania inawanyimwa wananchi haki hii. Katiba inawapa wananchi haki hii kwa mkono wake wa kulia, lakini inaipokonya kwa mkono wa kushoto pale inavyohitimisha kwa kusema "ili mradi sheria inazingatiwa" .Hapa Jamii Forums wananchi wanalindwa na Article 19 ya Universal Declaration Of Human Rights - which calls for the protection of free expression in all media.

Busara kwako Mama Lwakatare na wanasiasa/viongozi wengine ni kuja tu na kauli za kukanusha taarifa mnazizona humu kwamba sio za kweli, iwapo mtaona umuhimu wa kufanya hivyo, huku mkitoa maelezo yenu mbadala, kuweka mambo sawa. lakini sio kuja na hoja hafifu kama hizi kwamba Jamii Forums inasambaza taarifa mbalimbali za uongo, hivyo wamiliki wachukuliwe hatua.

Mheshimiwa Lwakatare, ungefanya utafiti wako kabla, ungetambua kwamba, sio tu kwamba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haina 'authority' juu ya suala lako, lakini muhimu zaidi ni kwamba haina 'discretion' wala 'jurisdiction'. Vinginevyo wamiliki wa Jamii Forums washawishike kwenda kujisajili "TZNIC", ili TCRA ipate nafasi kufanikisha malengo hayo kupitia mchakato wa "Internet Censorship".

Vinginevyo pole sana Mama. Ushauri wa wengi kwako ni kwamba, tumia nafasi uliyonayo kuendeleza mapambano dhidi ya umaskini, hasa kina mama, pia kufanya kazi kwa bidii kwa maslahi ya taifa ya ujumla. Tupo tunaotambua mchango wako. Endelea kujikita huko, kwani kwa kufanya hivyo, utashangaa jinsi gani Jamii Forums itakavyokumwagia pongezi nyingi, mimi nikiwa mmoja wao.
 
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga, amewaeleza wabunge kuwa, mmiliki wa mtandao wetu wa jamii forum anaweza kuwa Mtanzania au si Mtanzania.

Ameyasema hayo bungeni mjini Dodoma wakati anajibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Getrude Lwakatare (CCM).

Mbunge huyo amedai kuwa, Mtandao huo umekuwa ukisambaza habari za uongo kwa watu mbalimbali na haujachukuliwa hatua hivyo alitaka kumfahamu mmiliki wa mtandao huo.

Kitwanga amesema, uanzishwaji wa tovuti za kijamii haulazimishi mtu kujisajili wala kujitambulisha , na huanzishwa na mtu yeyote popote duniani.

"Kutokana na asili na miundo ya tovuti za kijamii, mamlaka haisajili wala kutoa leseni kwa tovuti hizo, kimsingi maudhui yanayoadikwa katika tovuti hizo za kijamii ni maoni binafsi ya watu yasiyoangaliwa iwapo ni ya kweli au la" amesema Kitwanga.

Baada ya Mbunge wa Viti Maalum, Hilda Ngoye (CCM) kuuliza swali la nyongeza, wakati Kitwanga anajiandaa kumjibu, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimtaka kiongozi huyo wa Serikali, ajibu hasa swali kuhusu ' Jamii Forum na matatizo yake makubwa'

Ngoye amedai kuwa, baadhi ya mambo yanayoandikwa kwenye mtandao wa Jamii Forum yana madhara katika jamii yakiwemo matusi ya nguoni na ni kinyume cha utamaduni wa Mtanzania.

Aliuliza kama Serikali ipo tayari kuwasilisha bungeni muswada , Bunge litunge sheria ili mtandao huo uache kuandika mambo ya maudhi na uchochezi.

Alitaka pia kufahamu kama Serikali ipo tayari kuwasilisha bungeni muswada ili Bunge litunge sheria itakayozuia watoto kusoma ‘mambo machafu' kwenye ‘internet café' vikiwemo vitendo vya ngono.

Kitwanga amesema, suala la kudhiti mitandao ya kijamii litakuwa kwenye Muswada wa Sheria ya Habari.

Amesema, suala la maadili ya watoto ni jukumu la wazazi, na kwamba ndiyo wanaowapa fedha za kwenda ‘Internet café'.

Amesema, kutokana na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, kuna namna nyingi zinazowawezesha watoto kuona ‘mambo yasiyofaa' zikiwemo simu za mkononi, ipad, na laptops.

Amesema ni wajibu wa wazazi kuhakikisha kuwa watoto wao wanakua kwa mujibu wa maadili ya taifa.
I have picked three things from Hilda
uongo.... Kwangu mimi JF inasema kweli in cases unless anaingia jukwaa la jokes/udaku AMA chitchat
matusi.... Labda sijui matusi ni nini, pia nicheki Yale magazeti ya shigongo na Athari Zake Kwani haihitaji kulogin kusoma magazeti
usajili.... Hebu aisajili kwanza facebook

Hilda ngoye, another muppet
 
Mama rwakatare hivi anajua hata matumizi ya mtandao? Manake ukisema usajili blogs zote, mbona kutakucjhwa?

Nimepata shaka sana kama amesoma kiasi cha kujua kompyuta. Labda wale watoto wake wanyanyua vyuma ndo wanamsomea mtandao umeandika nini
 
Kama kuna siku magamba watakua wamekosea step ni kufunga JF maana kitakochokuja kitakuwa moto zaidi ya JF.
Ingekuwa imesajiliwa bongo wangeshaifungia, so owners wamecheza game safi.

Wakiwazuia watanzania kuiona, itakuwa sawa na kuwanyima uhuru wa habari.

There is nothing they can do, ninaamini wabunge wengi wamo humu wanatumia nick names, so angewaomba wabunge waache matusi wakati wanatetea hoja zao humu.

Pia nina uhakika kuna wale wanaowalipa waje kutetea mafisadi humu, since mafisadi hawasafishiki kwa hoja kwasababu all the facts wana JF wako aware nazo na nyingi zilianzia humu na bado zipo, basi the last resort ni personal attacks na matusi na udini etc, hapo ndo utajua why they say mpambe nuksi kuliko bosi mwenyewe.
 
watuachie JF yetu ... tumetoka nayo mbaali
 
Unajua kila mara ninapoiangalia avatar yako nashangaa sana, najiuliza hivi huyu mtu kasoma "Mein Kampf"? Anamjua Hitler na nini Hitler kafanya?

Lakini always naamini katika freedom of expression na siamini katika censorship, kwa hiyo nakuacha tu.

Leo nakuja kuona anayempenda Hitler amshangaa ampendaye shetani.

JF has never failed me yet!
Kiranga ini bora kumpenda shetani kuliko Hitler..kwani inawezekana existence ya shetani ni kama hoax tu na unaweza kukuta shetani ha exist.huyu jamaa inawezekana kweli hamjui wala hajasoma historia ya hitler vizuri.
 
wameshindwa kujadili MGOMO WA MADAKTARI na hali mbaya ya uchumi WANAJADILI JF? Kweli magamba wamezeeka akili


AM hata waliozeeka akili wana nafuu kubwa sana maana wanakuwa na hekima na busara za hali ya juu, hawa magamba ni mataahira.
 
Ni ile thread ya yeye kuua kiwanda ndio imemwamsha nini???

Mama Mchungaji Wananchi bungeni hamtuzungumzii ndio mana tuko huku kufarijiana. Wewe tenda mema utasifiwa tu.

Na uoga wa nini?
Namimi nimeshangaa mchungaji aliyesahau hata biblia anayoihubiri kila siku. Kama yeye hana uozo wowote Mungu wa kweli atamlinda siku zote; Yeye asimamie tu ukweli; and (the truth will always set her free). Kwa mtindo huu wengi tumeanza ku-question imani yake .
 
kwa nini haitakiwi na Magambaz? Tutumie busara kutafakari ili tupate jibu inawezekana na sisi wana JF tuna matatizo. Lakini kweli sometimes baadhi yetu wanakwenda nje ya maudhui ya JF. Sasa kama utaanza kusema fulani mjinga, Kilaza, kubeza kitu kitu na mambo kama hayo hayo, kweli tunakuwa hatuko tena kwenye lengo la kukosoa, kuboresha, kushirikisha ili mwisho wa siku maendeleo kwa watanzania.

Wang'ayo, usinijumushe na mimi katika mawazo mgando kama yako ya kuishabikia ccm kwa kila kitu! kwani katika nchi hii chama cha magamba pekee ndicho chenye hatimiliki ya kusema fulani mjinga, Kilaza na kubeza kitu kitu cha wapinzani wao? Kama la mbona ndo zao kila siku kupitia TBC, Redio Uhuru, magazeti ya Habari leo,Jamba leo, Majira, Uhuru, nk?
 
Mimi nahisi kama yeye ndo Faiza Foxy vile.

Hapana sio Faiza Foxy. Faiza Foxy namfahamu sana, ameajiriwa na Ikulu, watu wanamuita personal assistant wa JK idara ya mawasiliano (sijajua kama hiyo ni title aliyoajiriwa nayo) anakisomo chake vizuri tu lakini ndio kama vile tena....... maslahi yametangulia uzalendo.
 
Alivyoakuwa na mgogoro na yule partner menzake walioanzisha naye shule za St. Mary's; ilisemekana huyo partner wake alitoa siri kwamba shule walianzisha kwa hela za wafadhili i.e. waliomba hela kwa wafadhili kwaajili yakusaidia watoto wasiojiweza wao wakafanyia kitega uchumi. Hii ilikuwa ni tetesi sijui kama kuna mtu aliweza ku-validate or even care kufanya uchunguzi.
 
hana maana yoyote huyo mama. Hapa Jf ni kitovu cha mabadiliko ya fikra. Kamwe hataweza kuizima kama hana la maana la kuongea ni bora akae kimya
 
Back
Top Bottom