Baada ya gazeti la habari leo, Tanzania Daima na mengineyo kuandika habari kuhusu Jamii Forums watu makini wameanza kuingia kwenye mitandao na kuanza kuitafuta JF waone kuna nini hadi baadhi ya Wabunge wailalamikie. Mdau mmoja kutoka dodoma anasema baadhi ya wabunge waliokuwa hawaijui JF waliamua jana jioni kuulizana na weng wao wakaingia kuona kuna nini. Zoezi hili si kwa wabunge tu bali hata watu wengine makini.......wameanza kuperuzi kuon JF kuna nini. Leo JF itakuwa na guests wengi kuliko Members katika baadhi ya thread. Then baadhi ya wadau wanahoji matusi yanayoongelewa na Mchungaji Rwakatare.......yako Mambo ya Kikubwa na nilazima uwe member......sasa yeye kilichomtuma kuwa member tena inawezekana Premium Member ili aone mambo ya kikubwa ni nini? Alienda kutafuta nini kule?
Baadhi ya habari kuhusu Jamii Forum kama ilivyopewa kipaumbele leo ni hii hapa
Habari za Kitaifa
Jamii Forum haijasajiliwa Tanzania
MTANDAO wa kijamii wa Jamii Forum haujasajiliwa Tanzania, Bunge limeelezwa.
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Charles Kitwanga, amewaeleza wabunge kuwa, mmiliki wa mtandao huo anaweza kuwa Mtanzania au si Mtanzania.
Ameyasema hayo bungeni mjini Dodoma wakati anajibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Getrude Lwakatare (CCM).
Mbunge huyo amedai kuwa, Mtandao huo umekuwa ukisambaza habari za uongo kwa watu mbalimbali na haujachukuliwa hatua hivyo alitaka kumfahamu mmiliki wa mtandao huo.
Kitwanga amesema, uanzishwaji wa tovuti za kijamii haulazimishi mtu kujisajili wala kujitambulisha , na huanzishwa na mtu yeyote popote duniani.
Kutokana na asili na miundo ya tovuti za kijamii, mamlaka haisajili wala kutoa leseni kwa tovuti hizo, kimsingi maudhui yanayoadikwa katika tovuti hizo za kijamii ni maoni binafsi ya watu yasiyoangaliwa iwapo ni ya kweli au la amesema Kitwanga.
Baada ya Mbunge wa Viti Maalum, Hilda Ngoye (CCM) kuuliza swali la nyongeza, wakati Kitwanga anajiandaa kumjibu, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimtaka kiongozi huyo wa Serikali, ajibu hasa swali kuhusu Jamii Forum na matatizo yake makubwa
Ngoye amedai kuwa, baadhi ya mambo yanayoandikwa kwenye mtandao wa Jamii Forum yana madhara katika jamii yakiwemo matusi ya nguoni na ni kinyume cha utamaduni wa Mtanzania.
Aliuliza kama Serikali ipo tayari kuwasilisha bungeni muswada , Bunge litunge sheria ili mtandao huo uache kuandika mambo ya maudhi na uchochezi.
Alitaka pia kufahamu kama Serikali ipo tayari kuwasilisha bungeni muswada ili Bunge litunge sheria itakayozuia watoto kusoma mambo machafu kwenye internet café vikiwemo vitendo vya ngono.
Kitwanga amesema, suala la kudhiti mitandao ya kijamii litakuwa kwenye Muswada wa Sheria ya Habari.
Amesema, suala la maadili ya watoto ni jukumu la wazazi, na kwamba ndiyo wanaowapa fedha za kwenda Internet café.
Amesema, kutokana na kukua kwa teknolojia ya mawasiliano, kuna namna nyingi zinazowawezesha watoto kuona mambo yasiyofaa zikiwemo simu za mkononi, ipad, na laptops.
Amesema ni wajibu wa wazazi kuhakikisha kuwa watoto wao wanakua kwa mujibu wa maadili ya taifa.