Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

wanasema eti tunaandika matusi, wanataka kujua owner wa jamii forum. swali limeulizwa leo hii bungeni.

Wanashindwa kujadili mambo yanayohusu maendeleo ya taifa, wanataka kulalamika kuhusu JF. Kwani wamechaguliwa na Wananchi ii kwenda kujadili mawazo ya watu au kujadili mambo yanayohusu Taifa.

JF hili ni bunge letu na sisi tunatoa mawazo yetu hapa kama wao wanavyotoa pale Bungeni.

Sasa hili bunge letu la JF ni kwamba linajadili mambo kiunsdani na yaliyo ya kweli ndio maana wanataka kutufunga midomo. haiwahusu wao kujua Owner ni nani!!!! Mbona sisis wao wanajadili mambo yasiyo kuwa na maana lakini hatuwafungi midomo.

Katika ya Tanzanai inaturuhusu kutoa mawazo yetu tupo huru kwa hili. Na kama wanafungua hii Website ni heri kwani watajua kuwa na sisi tuna uwezo wa kujadili mambo ingawa hatulipwi Posho kma wao, lakini tungepewa nafasi huenda matatizo yanayojitokeza Tanzania sasa yangepata muafaka, kwani mawazo yanayotolewa hapa ni mazuri sana na ya kujenga.

Nakumbuka kulikuwa na website moja inayoitwa bcstimes ambayo ilikuwa inamilikiwa na magazeti ya Majira, kutokana na mawazo mazuri tuliyokuwa tunatoa waliamua kuweka mijadala yetu katika gazeti, yaani tulikuwa na ukurasa kabisa kwa ajili ya mijadala ya members. Lakini sasa kila nikijaribu siipati tena ile website, sijui ndio Bunge la Tanzania wameamua kuipiga mkwara nayo.
Pia na hata kwenye gazeti siku hizi hakuna tena ule ukurasa. Nina wasiwasi na wabunge huenda wameshatia mkono kuifunga ile website.

NAOMBA WATUACHE BUNGENI WAJADILI YANAYOWAHUSU NAO WAKITAKA KUJISAJILI HAPA WAPO HURU LAKINI SIYO KUFANYA NDIO HOJA YA KUPELEKA BUNGENI.

MKOMEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE KABISAAAAAAAAAAAAAAAAAA


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Ni ile thread ya yeye kuua kiwanda ndio imemwamsha nini???

Mama Mchungaji Wananchi bungeni hamtuzungumzii ndio mana tuko huku kufarijiana. Wewe tenda mema utasifiwa tu.

Na uoga wa nini? Ninyi si ndio wenye V8s na VXs? Sasa unaogopa keyboard?
 
Sio kwamba jamiiforums niya Chadema, chochote kinachoipinga serikali nicha Chadema, vyote vinavyoisifia serikali vina malengo mazuri na serikali, hivyo ni bora kufunga vyote vinavyo ipinga serikali maana itakuwa kuwakomoa chadema, hata waje waliokataa kuvua magamba maana wameipinga mikakati ya CCM.

Baada ya hapo wawafungulie mashtaka wezi wa Epa maana wameipinga serikali kwa kutorudisha fedha, baada ya hapo wawanyang'anye lesini madaktari maana wameigomea serikali kwa kupinga kutendewa vibaya sserikali.Wabunge wa ccm fikra zao ni chafu kama uchafu tunao ona kwenye chama chao.
 
JF ni tatizo kubwa.... hahaha watajiju, waziri amesema haijasajiliwa TZ hivyo hawawezi kuwafuatilia... waziri anawashauri wabunge wajiandae vya kutosha wanapoleta madai kuhusu taarifa za mitandao, kwani siku hizi unweza kupata taarifa popote na wakati wowote, aamue ni ipi ataisoma... safi sana WAZIRI

Lwakatare kaipaisha JF sasa wabunge wataanza kuingia kuchungulia karibuni sana wabunge
 
HIVI HUYU MAMA UCHUNGAJI WAKE ALIUPATA WAPI?MAANA NAONA ANANIPA WASIWASI SASA,
KAMA AMEKOSA MASWALI YA KUULIZA NI BORA ASINZIE KAMA WENGINE.

NILIKUWA NAFATILIA BAADHI YA MISA ZAKE KWENYE TV,ILA KUANZIA LEO NITAACHANA NA HIYO MAMBO,
HAYA YOTE NI MATATIZO YA KUPEANA VYEO-ANGEGOMBEA ANGEWEZA SHINDWA.

KILA MTANDAO WANATAKA KUUFUNGIA,WALISHAFUNGIA blog ya maishamatamu,ila imesharudi hewan,yan kila sehem wanataka kubana,JAMANI HII NCHI MSIJE IFANYA KAMA NORTH KOREA,MNATAKA CENSORSHIP KWENYE KILA KITU-HAMTAWEZZA...
 
attachment.php

Na nila shaka hizi picha zinazowaumbua, wao wameona ni matusi. kama hoja zimekwisha hakuna haja ya kuendelea na bunge, Spika aahirishe hadi mwezi wa Sita. Sio kukaa kila siku kumbe hawana ya kujadili wanakula Posho tu

MKOMEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!!!
 
Ni ile thread ya yeye kuua kiwanda ndio imemwamsha nini???

Mama Mchungaji Wananchi bungeni hamtuzungumzii ndio mana tuko huku kufarijiana. Wewe tenda mema utasifiwa tu.

Na uoga wa nini? Ninyi si ndio wenye V8s na VXs? Sasa unaogopa keyboard?

Invisible anafanya kazi ya kihuni

Huyu mama kafungua vita dhidi ya JF sasa why cant she get piece of her own medicine?
 
Natamani waseme na FACEBOOK nayo pia ifungwe maana tutahamia huko wote
 
Mkuu huyu mama anafadhiliwa na wabaka haki hasahasa Wafisadi. Watanzania tuwe macho tunanyimwa haki. Mpaka hata mtu anaejifanya wa Mungu anaungana nao kutumaliza.
 
JF ni moto inaumiza vichwa vya mafisadi wa siasa mpaka mafisadi wa dini wanachanganyikiwa badala ya kukemea maovu na wezi yeye anapambana na JF wakati hata hajui mabadiliko ya teknolojia yalivyo ingekuwa rahisi kufungia JF kama anavyofikiria basi US wangekuwa wameshaifungia wikileaks zamani
 
JF ni ya wakereketwa......kama una kero yao iweke mezani tuijadili, JF haina chama, dini wala kabila.
Karibu Mama Lwakatare
 
Wana JF kutokana na mtandao huu wa kijamii kuibua na kueneza siri za Serikali Wabunge wa CCM wameridhia Mtandao huo ufungwe kama ilivyokuwa Ze Utamu na Mtoa Hoja ni Mchungaji Getrude Lwakatale, Leo pia kapeleka swali lake Bungeni.

Waziri kaitetea JF na kuwashauri wabunge kuwa ni chombo cha habari cha kijamii.

Huyu spika Ndugu Job Ndugai ati anamlazimisha waziri asema JF ni mbaya...kwa kweli namshukuru sana waziri ajaisema sana vibaya JF.Ila cha kushangaza watu wenye matatizo ndio wanaichukia sana JF.Huyu waziri ana shida na JF maana yeye ni msafi,wachafu ndio wanaiogopa JF.
 
Back
Top Bottom