Wanashindwa kujadili mambo yanayohusu maendeleo ya taifa, wanataka kulalamika kuhusu JF. Kwani wamechaguliwa na Wananchi ii kwenda kujadili mawazo ya watu au kujadili mambo yanayohusu Taifa.
JF hili ni bunge letu na sisi tunatoa mawazo yetu hapa kama wao wanavyotoa pale Bungeni.
Sasa hili bunge letu la JF ni kwamba linajadili mambo kiunsdani na yaliyo ya kweli ndio maana wanataka kutufunga midomo. haiwahusu wao kujua Owner ni nani!!!! Mbona sisis wao wanajadili mambo yasiyo kuwa na maana lakini hatuwafungi midomo.
Katika ya Tanzanai inaturuhusu kutoa mawazo yetu tupo huru kwa hili. Na kama wanafungua hii Website ni heri kwani watajua kuwa na sisi tuna uwezo wa kujadili mambo ingawa hatulipwi Posho kma wao, lakini tungepewa nafasi huenda matatizo yanayojitokeza Tanzania sasa yangepata muafaka, kwani mawazo yanayotolewa hapa ni mazuri sana na ya kujenga.
Nakumbuka kulikuwa na website moja inayoitwa bcstimes ambayo ilikuwa inamilikiwa na magazeti ya Majira, kutokana na mawazo mazuri tuliyokuwa tunatoa waliamua kuweka mijadala yetu katika gazeti, yaani tulikuwa na ukurasa kabisa kwa ajili ya mijadala ya members. Lakini sasa kila nikijaribu siipati tena ile website, sijui ndio Bunge la Tanzania wameamua kuipiga mkwara nayo.
Pia na hata kwenye gazeti siku hizi hakuna tena ule ukurasa. Nina wasiwasi na wabunge huenda wameshatia mkono kuifunga ile website.
NAOMBA WATUACHE BUNGENI WAJADILI YANAYOWAHUSU NAO WAKITAKA KUJISAJILI HAPA WAPO HURU LAKINI SIYO KUFANYA NDIO HOJA YA KUPELEKA BUNGENI.
MKOMEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE KABISAAAAAAAAAAAAAAAAAA
MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!