Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Mimi naona kasaidia sana kui-promote JF!!! Asante Mch. Dr. Mh. Mama Lwakatare!!!


Pesa za kanisani hazimtoshi sasa anafikiri JF inaharibia posho ya laki mbili kwa siku!!!??
 
Mama ameshikwa pabaya! NAdhani anazidi kuipa JF umaarufu kwa yakini hata wale Wabunge na wananchi ambao hawaijui JF basi watakuwa na shauku ya kujiunga nayo nao waone kuna nini humo na hatimae kuzidi kuipa umaarufu JF na mwishowe kufanya hata wale wabunge ambao huona uoga kutoa malamiko mjengoni wayatoe humu! mbona anazidisha hatari kwa serikali ?
 
Kwanza huyu mama atuambie mumewake yupo wapi??
Kwanini aliachana naye, kwa sisi waislam mwanamke ambaye hajaolewa hatakiwi kuongea lolote, alipoanza kufanikiwa tuu akamdhalau mumewake na kuvunza ndoa leo anatuambia nini, wee vuna unachovuna na ujue kunamwisho wake!
 
nchi yenu imejaa wezi na wauwaji...ninyi watu amkeni piganieni taifa lenu
 
Huyu mama kasahau kuwa yeye ni mchungaji!
Sasa JF inamkelaje nahisi yuko kibiashara zaidi!
Alafu wanaosali kwake hali ya maisha ikiimprove kwa kuwa na serikali inayojari watu wake lazima wamwache.
Ni shida tuu zawapeleka watu pale kwake ambazo nyingi ya izo husababishwa na CCM ndo maana wakampa viti maalum ili kula vichwa
 
katika hali ambayo hata yeye mwenyewe hakuikusudia mama huyu mbunge wa viti maalum ameitangaza jf bungeni, Tanzania na dunia nzima pale alipodhamiria kwa dhati kuishtaki jf bungeni akitarajia kufungwa kwa mtandao huu na ikawa kinyume cha haki za upatikanaji wa hahari hvyo kuiacha jf iking'ara kama theluji ya ml. KILIMANJARO. nakushukuru sana mama, mchungaji, mheshimiwa sana na nakukaribisha jf uje uchangie mawazo yako.
 
JF hawawezi kuifunga wala kuifuta... Wangekuwa na uwezo wangefanya hivyo siku nyingi!!

JF ni kama sindano, ili upone, lazima ikuchome
 
uoga wa mabadiliko walionao ccm! Watafunga hadi fb,twitter haha na bado

hata wakifanikiwa kufunga zoote hizo tutatumia msg kwenye simu na wakiweza huko hata kwa barua, anachosema yasiwepo mawasiliano. Duu kweli magamba wanakazi!
 
Huyu mama tangu amechaguliwa viti maalumu hajawahi kuongea chochote, leo kutudhihirishia kama sio bubu ameona afungue domo lake kwa kutaka kuichongea JF, Hana jipya huyo
 
Namuomba aje hapa barazani afu atetee huo msimamo wake wa kuifungia JF kama kweli ana huo moyo..wewe mama ni malaika hata usikosolewe? jaribu kutenda mema na utubu yote ya kweli yasemwayo juu yako haswa kuhusu unyanyasaji wa watumishi katika shule zako...
 
Kwa mwendo wa Jf ya sasa sitashangaa ikifungiwa tumeacha kujenga hoja tumegeuka ni kijiwe ya wahuni na matusi.
 
Naamini Mama Mchungaji anafuatilia mada hii kwa umakini ili ajue wanaJF watasema ninni Mama tafadhali soma hii [SUP]24[/SUP]``,Hakuna mtu anayeweza kuwatumikia mabwana wawili, kwa sababu, ama atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au atamthami ni mmoja na kumdharau mwingine. Huwezi kumtumikia Mungu na mali.'' Kwa ushauri wangu kwa mama mch. namwona kama mbwa mwitu aliye katika ngozi ya kondoo, inaonekana kutokana na maandishi hayo hapo mwanzo, Yeye anamtumikia nani!!!??
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Kuongezeka kwa makanisa mengi ya kisanii..ni changamoto kwa serikali na mamlaka inayohusika na mapato waweke utaratibu wa kukusanya kodi kutoka katika makanisa haya. maana kwa kifupi wanapata fedha nyingi mno kwa muda mfupi kwa kisingizio cha kutoa huduma ya kiroho, ni muda muafaka serikali ifunguke na kuanza kukusanya mapato kutoka kwenye biashara za aina hii!
 
Matusi yakiwa sehemu ya hoja za msingi na kuonekana ni jambo la kaiwada hakika mimi naona tunamwangusha mwanzilishi wa forum hii na wala hatumtendei haki
 
Mi ningependa kujuwa ametoa sababu zipi zinazomfanya atake JF ifungwe....... Kama ni siri zipi hizo ...?? Maana kama ni siri, zisipokuja hapa JF, basi zitakwenda kwa Slaa na wengine nao watazitoa kwenye mikutano ya hadhara.. Kwani ile barua ya kuchangishana ili kufanikisha bajeti ya wizara ya nishati na madini haikuwa siri..??? AU atataka na yule mbunge wa CCM aliyeisoma bungeni naye afutwe..?? Huko ni kukikimbia kivuli chake..ansahau kuwa juwa likiwaka tu kinarudi.....
 
Kama kuna siku magamba watakua wamekosea step ni kufunga JF maana kitakochokuja kitakuwa moto zaidi ya JF.

Zipo nchi zinafunga mitandao kama hii au kuwekewa sheria kali kama ikitumika vibaya na washiriki kama china, korea kasikazini, saudi Arabia, Irani
 
Back
Top Bottom