Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Wana JF kutokana na mtandao huu wa kijamii kuibua na kueneza siri za Serikali Wabunge wa CCM wameridhia Mtandao huo ufungwe kama ilivyokuwa Ze Utamu na Mtoa Hoja ni Mchungaji Getrude Lwakatale, Leo pia kapeleka swali lake Bungeni.

Waziri kaitetea JF na kuwashauri wabunge kuwa ni chombo cha habari cha kijamii.

ndio tatizo letu watanzani ukweli hatuupendi wote waichukiayo JF ana sababu au madhambi yake ambayo anajua siku moja yatawekwa hadharani hatuuwezi uwazi , hatuiwezi democracy.
ila huu ni mwanzo tu ukweli utaendelea na hata kama watafanikiwa kutubana huku tutatafuta namna nyingine tu mapinduzi na mabadiliko yataendelea tuuu

hii ni kwake na kila mmoja mwenye mawazo na mipango kama yake.
 
Ha ha ha haaah!! Dokta ugomvi unauweza?

ndio maana wengine tukiwakumbuka watu kama akina regia tunatokwa na machozi.. why regia wakati watu wa kufa wamejaa kibao pale bungeni..mtu analipwa kwa ajili ya kuwatetea watu badala yake anazuia vitu vinavyoiamsha serikali sababu tu yeye ananufaika na familia yake... mtu kama huyu ana tija gani kwa ustawi wa watz..
 
usishangae uchaguzi utakapokaribia watafunga tuuu, serikali yetu kwa zengweeeeeeee
 
Wana JF kutokana na mtandao huu wa kijamii kuibua na kueneza siri za Serikali Wabunge wa CCM wameridhia Mtandao huo ufungwe kama ilivyokuwa Ze Utamu na Mtoa Hoja ni Mchungaji Getrude Lwakatale, Leo pia kapeleka swali lake Bungeni.

Waziri kaitetea JF na kuwashauri wabunge kuwa ni chombo cha habari cha kijamii.
ole wao wafanyao unafiki na madhambi huku wakijitia ni watumishi waaminifu wa mungu. siku moja wataumbuliwa tena kwa matendo yao wenyewe.
 
Huyu kalewa pesa za sadaka na zile za viti maalim mapepo yameanza kuamka sasa ana bwabwaja mpeni pole sana .
 
huyu mama inasemwa anauza UNGA, hawezi kuipenda JF hata siku moja
mama-lwakatare.jpg
 
Huyu mama mchungaji kama kayasema hayo basi kuna nyuzi zimemgusa humu. Hawa wana siasa wasiokubali kupokea "criticism" walikuwa hawafai kabisa kuwa wana siasa. Anafikiri JF ni kanisani kwake humu, kila atakalo sema watu watamchekelea tu.


Hawa ndio wale wanaoingia siasa kwa sifa na pesa zao na si kwa kuwa ni wana siasa. Mie alivyoingia nikajuwa anhaa sasa, tumepata msemaji ambae atakwenda mjengoni kufanya mambo, kumbe si lolote si chochote. Waondoe tu hivi viti vya kupeana.

Ushatoka Bungeni tayariii!!!!!
 
Kibonde kaikana haijui jamiiforums anashangaa hivi mitandao kama ze utamu bado imebaki ....
 
Wakuu,
JF inapata promo bila malipo. Alianza mzee wetu Msekwa, sasa Waheshimiwa wanatumia milioni 64(za posho kwa siku) kuijadili! Duh...

Hii inapeleka ujumbe kuwa wanaisoma kwahiyo ni dhima yetu kuiboresha kwani sisi tuna uhakika sasa wanapata maoni yetu kiulaini.

Kinachomsumbua mama Mchungaji pamoja na mambo mengine, ile habari iliyoeleza kuwa amemilikishwa kiwanda cha Mang'ula, mama akaamua kuchukua mashine na kuzifanya vyuma chakavu.

Wapo waliohoji utaratibu uliotumika kumpa mmililki wa 'academy' uendeshaji wa kiwanda cha spea.

Hili linamsumbua Mama wa kiroho maana yanawezaibuka yatakayo compromise integrity yake mbele ya wanakondoo.

Mpeni salaam ametukumbusha na soon atakuwa mada JF in fair and respected way but not in favor
 
Kwa mwendo wa Jf ya sasa sitashangaa ikifungiwa tumeacha kujenga hoja tumegeuka ni kijiwe ya wahuni na matusi.
Na wewe umeanza au ndo wale wale,nilijua tuu kuwa JF inakukera, INAKUNYIMA USINGIZI!!!!!!!!!!

 
mama Rwakatale leo analo................. kaazi kweli kweli
 
Wana JF kutokana na mtandao huu wa kijamii kuibua na kueneza siri za Serikali Wabunge wa CCM wameridhia Mtandao huo ufungwe kama ilivyokuwa Ze Utamu na Mtoa Hoja ni Mchungaji Getrude Lwakatale, Leo pia kapeleka swali lake Bungeni.

Waziri kaitetea JF na kuwashauri wabunge kuwa ni chombo cha habari cha kijamii.

hatuwezi kutumikia mabwana wawili maana utampenda huyu na kumchkia huyu ama utaambatana na huyu na kumuacha huyu
 
Najaribu kuwaza kama p..tb joshua angeacha sinagogu akawa mbunge...hata kristo angeumia..
 
Back
Top Bottom