Sijamdhihaki nimesema kweli. Kwani kuna uongo hapo??
Kama lengo lako ni kutafuta Kiki basi imekula kwako. Kinyume cha hapo utubu kwa maana hicho ulicho kipost ni dhahiri umemkufuru Muumba wako!! Au labda km tayari umesha jiunga na kile chama hvyo unataka kuwaonyesha kuwa umeiva kiasi gani kwa kuwa mpinzani wa Mungu?? Huo sio ujanja.
Je umesahau amekuumba kwa kitu gani hata leo ukawa mkosoaji na mshindani wake?
Quran 16:4
"AMEMUUMBA MWANADAM
KWA TONE LA MANII. TAHAMAKI AMEKUWA MSHINDANI DHAHIRI (WA KUMKATAA MWENYEZI MUNGU)".
Bila shaka unafanya haya kwa kuwa huna ilmu nayo hvyo unataka upate wachache wa kuwapoteza. Imani yako iko wapi ndugu??
Qur 6:120
".....NA HAKIKA WENGI HUWAPOTEZA (WENGINE) KWA MATAMANIO YAO BILA YA KUWA NA ILIMU. BILA SHAKA MOLA WAKO ANAWAJUA VYEMA WALE WARUKAO MIPAKA".
Na hiki ulicho kifanya uliongozwa na SHETANI kwa malengo yako ya kuwashuhudia watu wakibishana kati ya wanao kuunga mkono na wanao kupinga. Allah anasema katika
Quran 6:121
".... NA KWAYAKINI SHETANI WANAWAFUNULIA MARAFIKI ZAO KUBISHANA NANYI (KATIKA MAMBO NAMNA HAYA, YASIYOKUWA NA MAANA). NA KAMA MKIWATII MTAKUWA WASHIRIKINA".
Kwa hiyo kila atakaye isoma hiyo posti yako kisha aka base kwenye upande wako wa kumkosoa Mungu na kumuona ana mapungufu basi naye atakuwa amejiingiza kwenye dhambi ya shirk chanzo ni wewe.
Mwisho nikukumbushe tu, hiki ulicho kifanya ni kitendo cha kumkufuru Mungu, hvyo tubu kwa Mola kabla haijafika siku yako ya kutolewa roho
ANAYE KUFURU
QUR 30:44 "Anaye kufuru, (madhara) ya kufuru yake ni Juu yake (mwenyewe). Na wafanyao mema, (hao) wanazitengeneza nafsi zao".
Ndugu yangu, wewe siyo wa kwanza kumkufuru Mungu, siku moja ukipata nafasi fanya safari ya kutembelea huko MISRI ukamuone FIRAUN ambaye alikuwa ni bingwa wa kumkufuru Mungu. Lakini Allah alimuahidi kuwa atautunza mwili wake ili uwe funzo kwa vizazi vijavyo. Kisa cha firaun ni ishara tosha kuwa Allah yupo, na muweza wa yote.
Quran 10:92 Allah akasema
"LEO BASI TUTAKUOKOA KWA MWILI WAKO ILI UWE ISHARA KWA AJILI YA WALIO NYUMA YAKO. NA HAKIKA WATU WENGI WAMEGHAFIRIKA NA ISHARA ZETU".
sasa ili uweze kumshuhudia firaun na ishara nyinginezo za Allah basi hunabud kusafiri Kama quran 30:42 inavyo tueleza.
"SEMA: SAFIRINI KATIKA ARDHI NA TAZAMENI JINSI ULIVYOKUWA MWISHO WA WALE WALIO TANGULIA. WENGI WAO WALIKUWA NI WENYE KUSHIRIKISHA.
nenda Misri ukauone mwili wa firaun/farao mpaka leo bado upo. Ni maoni yangu tu!!