Makosa 10 aliyotenda Mungu

Makosa 10 aliyotenda Mungu

Wakati nasoma huu Uzi wako nilikua nacheka mpaka mbavu zinaniuma.

1. Shetani aliumbwa na Mungu kwa namna ya kipekee sana. Na alikua kiongozi mkuu Wa sifa[Lucifer]
Lakini kiburi kilimpanda akataka kuchukua mamlaka ya Mungu. Ezekiel 28: 16-19
Na Mungu ni mwingi Wa Rehema, hakuweza kumtowesha kabisa, kwa sababu Mungu angeonekana katili wakati hayuko ivo.

2. Mungu hayuko mafichoni, Mungu yupo mahari pote. Hata hapo ulipo Mungu yupo. Mungu ni roho.
Yupo mahali pa siri kwa sababu yeye ni mtakatifu hakai na watu wenye dhambi.

3. Gharika wakati Wa nuhu.
Mungu anachukia uovu [Dhambi] kumbuka Hata sodoma na gomora Mungu aliiangiza, sababu ni uovu Wa watu.
Tofauti tulionayo kizazi hiki ni Neema. Mungu alichofanya ni kumtoa Yesu afe, ili azichukue dhambi zetu. Kupitia Yesu tupate msamaha Wa dhambi.

4. Hapo Mimi sielewi, lakini Ninachoelewa Mungu anafanya atakalo. Na hakuna Wa kuzuia

5. Mungu ametimiza. Ni vizazi vingi vimepita, na hapa huna ushahidi Wa idadi ya watu toka Adam mpaka sasa.

6. Sijui

7. Ni kweli kila alichokifanya Mungu kilikua chema.
Lakini baada tu dhambi kungia ulimwenguni kila kitu kika haribika.

Ndio maana Adam na hawa walipokula matunda mti Wa ujuzi Wa mema na mabaya, Mungu akamwambi hawa, hakika nitakuzidishia uchungu Wa kuzaa kwako. Mwanzo 3:16

Kwa hio tunaishi ktk aridhi ambayo imelaaniwa na Mungu.
Hayo majanga ya tsunami, mafuriko. Ni sehemu ya laana ya aridhi.

8. Hapa nakataa. Hivi viumbe havikuumbwa na Mungu.
Ni aina ya mwanadamu maisha anayoishi husababisha Magonjwa.
Fikiria magonjwa kama ukimwi, cancer, nk. Haya miaka kama 150 iliopita hayakuwepo

9.jehanamu ya moto ipo kwa wewe unaeambiwa usiibe, usizini husikii.
Nakutubu dhambi hutaki.
Mungu ameweka haya makao ili wanaopinga amri zake wakae huko

Ndio mana duniani hapa kuna magereza kwa wale wanaokataa kufuata sheria

Mungu anasamehe. Mangapi unamkosea Mungu bado anakupa nafasi ya kutubu?

Shetani ndio alitakiwa awe mfano kwa malaika wengine, lakini yy ndio aliongoza uasi.

Mungu hana kinyongo, yy ndio anaemiliki na kutawala.

10. Hapa umekufuru ndugu Yangu, umeingilia mamlaka ya uumbaji wa Mungu.
Soma Yohana 9:1-4
Vipofu, viwete zote hizo ni Kazi za Mungu.

Chuchu za kiume??? Daa!! Kweli we ni great thinker.
Mungu alimwuumba MTu kwa mfano wake.

Mwanzo 1:26
Huo ni uumbji Wa Mungu. Na Mungu akaona vote alivyo vifanya ni vyema.

Pia nahis wew ungenyimwa chuchu, ungomhoji Mungu, mbona (Mimi sina chuchu?) Mungu hana upendeleo.

Asante. Akili za Mungu hazichunguziki.

Naona kama majibu yako yana utata pia mfano namba 2. Mungu yupo kila sehemu mpaka hapo alipo mleta mada halafu hapo hapo unasema Mungu hakai karibu au walipo wadhambi!!!!!!!
 
Hapo namba moja ndo napata wasi wasi sana.. Mungu wetu ni mkuu na aliumba kila kitu yaan tunaamin/tunaaminishwa kuwa shetani pia aliumbwa na Mungu.
Ila pia tunaambiwa yeye ndo anajua kila kitu maana yake kilichopo,kilichopita na kitakachotokea mbele huko... Sasa ilikuaje akaanza kumuumba shetani huku akijua huyo shetani atakua kikwazo katika utawala wake? Kwa kua yeye ni mkuu mbona ilikua simple tu pale shetani alipozingua angemkamata sweka rumande huko au tia moto aondoe hiyo roho ya laana..

Mimi sio mpinga Mungu wala mpagani.. Ila nahoji tu ili kujua zaidi kuhus Mungu wetu tunaemuabudu....
Mkuu hata mi ni msabath ila kuna wakati namuachia tu Mungu kwasababu kuna maswal hayajibiki na binadam
 
Unajua mi ni mfia dini, ila jibu lako linanipa ukakasi.
Mkuu hata kabla ya kusoma hiyo post yako nimejikuta nacheka sana...hata kama tunaamini, bado tuna haki ya kuuliza.
 
Tanzania nchi huru kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake na akiamua kujamba ana jamba wakati wote.
Mleta mada umejamba sana, tena sii kidogo.
Uwe na uwoga hata robo
Uwoga hata robo???Mbona maandiko yanasema usiogope???...ina maana unapingana nayo???
 
Kwa nini Mungu alimuumba shetani.
Jibu la kisiasa. Yeye ni Mungu muumbaji. Ameumba vingi tu.

Kama maelezo ya kisiasa ya biblia uliyotumia kusema Mungu alimuumba shetani. Jibu ni kuwa shetani alikuwa Lucifer. Malaika mkuu. Alikuwa na sauti nyingi.
Alikuwa mkuu sana.
Alitamani kuwa mkuu kama aliyemuumba.
Akawashawishi malaika wenzake kuwa Mungu si mwenye haki. Wakapanga mapinduzi ila mapinduzi yakashindwa. Simulizi uliyonukuu inaeleza wakaadhibiwa kwa kutolewa huko palikokuwa makazi yao. Ila bado nguvu walikuwa nazo. Mungu akaona haitoshi aliwaacha waranderande. Sasa binadamu hawa waasi wakatushawishi tuendelee kuenda kinyume na mamlaka ya iliyotuweka.
Simulizi inaeleza kuwa by default tunakuwa sehemu ya vita hii ya haki baada ya babu yetu kushiriki.
Mwisho wa hii vita ni atakapoona Yeye imetosha.
Sasa akisema imetosha washiriki by default wataeleza viumbe vingine ubaya wa ukaidi against yeye. Na hapo ameonesha mchezo utahitimishwa kuwa Yeye ni wa haki na waasi wote na shetani habari yao itakuwa imeishia hapo.

Kukosea au kutokosea kwake ni tafakuri ngumu kwangu maana kufuatana na hizo simulizi uwepo wetu naona hauna maana ukilinganisha na nyota tu ninazo ziona na zote kaumba Yeye.
 
Ee Mwenyenzi Mungu muumba mbingu na nchi tunakuomba utusamehe bure
 
Hapo nimetania tu. Kikubwa ni kwamba hakuna Mungu na hakujawahi kuwa na Mungu na hakutakuja kuwe na Mungu.

Ishi tu vizuri na watu wenzako huku ukijua huyo anaeitwa Mungu aliumbwa na wanadamu kwenye mind zao.

HAKUWEZEKANI KUWE NA MUNGU MSHENZI NAMNA HIYO
Ndo madhara ya meditation hayo mnk ndo Dini yenu mpya vijana
 
MUNGU MKUU sisi sote sio wema kwako nakusihi kwa upendo na unyenyekevu msamehe ndugu yangu anayehoji uwezo wako
 
Hii thread ipo kwenye forum ya Jamii intelligence, ila most of the contributors wapo SIMPLE MINDED, yaan mada nzito kama hii watu wanajibu kiwepesi kabisa bila tatizo lolote, watu hawapo tayari kabisa kuumiza akili.
Huyu jamaa anachokiandika anakijua na biblia inavyosema anajua vizuri. ila kama kuna vitu vinamtatiza hana budi kuhoji, kwa mfano mimi pia KUNA VIPENGELE VINGI SANA NAVIJUA KWENYE KITABU CHA LUKA, YESU ANASEMA NGUVU ZAKE NA MAMLAKA YAKE YANATOKA WAPI, NA ALIKATAA KABISA KUITWA MWEMA NA KUSEMA HAKUNA ALIYE MWEMA ILA MUNGU PEKEE. Sasa sielewi kwanini sisi wakristo tunamuita Yesu Mungu, na kumuita Maria mama wa Mungu, huku si kukufuru? kweli Mungu amezaliwa kupitia kinena cha mwanamke? yani pale panapopita KIKONG'OTEO ndo Mungu alipopita?

Mungu hana birthday kwa sababu yeye yupo, alikuwepo, na ataendelea kuwepo, sasa hii tarehe 25 December imetokea wapi wakati Mungu hakuzaliwa? na kama hakuzaliwa hii birthday ya nini?

siwezi kuwalaumu coz MISHIPA YA FAHAMU IMESHALEGEZWA NA MZUNGU KUPITIA INJECTIONS MBALIMBALI. Ndo mana watu wanafeli mashuleni na vyuoni kwa kukosa ujasiri wa kuhoji, mwalimu anafundisha huelewi kipindi kikiisha unalamu ah mwalimu simuelewi, uliuluza swali class? pepa linakuja unafeli..

TUTUMIE UTASHI TULOPEWA KUFIKIRI NA KUHOJI SIO KUWA NA WOGA USIOKUA NA TIJA.. YAAN NI SAWASAWA NA MTU YULE ANAYEOGOPA KUIKOSOA SERIKALI YA CCM PALE INAPOFANYA MAAMUZI AMBAYO NI UNTHINKABLE KISA UNAOGOPA VIRUNGU NA KUFUNGWA.

AMKA.
 
MUNGU MKUU sisi sote sio wema kwako nakusihi kwa upendo na unyenyekevu msamehe ndugu yangu anayehoji uwezo wako
Mkuu ipo hivi,...nina mambo yanayonitatiza kuhusiana na imani, kati ya hayo ni hayo kumi hapo juu. Sasa nimekuja humu jf kutafuta mawazo ya watu wanaoweza kunijibu, then watu wananihukumu....mnaona mimi mkosaji kiasi cha kuanza kuniombea toba....Kwani kosa langu liko wapi??? mbona kwenye maandiko Mungu anasema...haya basi njooni tuhojiane, tusemezane....Ebu tafakari upya.
 
Hii thread ipo kwenye forum ya Jamii intelligence, ila most of the contributors wapo SIMPLE MINDED, yaan mada nzito kama hii watu wanajibu kiwepesi kabisa bila tatizo lolote, watu hawapo tayari kabisa kuumiza akili.
Huyu jamaa anachokiandika anakijua na biblia inavyosema anajua vizuri. ila kama kuna vitu vinamtatiza hana budi kuhoji, kwa mfano mimi pia KUNA VIPENGELE VINGI SANA NAVIJUA KWENYE KITABU CHA LUKA YESU ANA-REFER NGUVU ZAKE NA MAMLAKA YAKE YANATOKA WAPI, NA ALIKATAA KABISA KUITWA MWEMA NA KUSEMA HAKUNA ALIYE MWEMA ZAIDI YA MUNGU. Sasa sielewi kwanini sisi wakristo tunamuita Yesu Mungu, na kumuita Maria mama wa Mungu, huku si kukufuru? kweli Mungu amezaliwa kupitia kinena cha mwanamke? yani pale panapopita KIKONG'OTEO ndo Mungu alipopita?

Mungu hana birthday kwa sababu yeye yupo, alikuwepo, na ataendelea kuwepo, sasa hii tarehe 25 December imetokea wapi wakati Mungu hakuzaliwa? na kama hakuzaliwa hii birthday ya nini?

siwezi kuwalaumu coz MISHIPA YA FAHAMU IMESHALEGEZWA NA MZUNGU KUPITIA INJECTIONS MBALIMBALI. Ndo mana watu wanafeli mashuleni na vyuoni kwa kukosa ujasiri wa kuhoji, mwalimu anafundisha huelewi kipindi kikiisha unalamu ah mwalimu simuelewi, uliuluza swali class? pepa linakuja unafeli..

TUTUMIE UTASHI TULOPEWA KUFIKIRI NA KUHOJI SIO KUWA NA WOGA USIOKUA NA TIJA.. YAAN NI SAWASAWA NA MTU YULE ANAYEOGOPA KUIKOSOA SERIKALI YA CCM PALE INAPOFANYA MAAMUZI AMBAYO NI UNTHINKABLE KISA UNAOGOPA VIRUNGU NA KUFUNGWA.

AMKA.
Mkuu umenena yote kabisa...Mimi nilidhani jf Intellegence wanakuwepo ma critical thinkers but nikagundua kumbe wapo ambao hawajui namna ya kufikiri....Hayo mambo 10 ni baadhi ya vitu vinavyo nitatiza ktk imani, nimeleta humu ili watu nondo wanijibu....badala yake nakutana na vitoto vinatoa vitisho na hukumu....vinajipa majukumu ya Mungu...Kama mtu hana jibu tulia tujulishwe coz bado naamini kuna miamba wa imani humu ndani.
 
Back
Top Bottom