Makosa 10 aliyotenda Mungu

Makosa 10 aliyotenda Mungu

Ikiwa watu wanazaliwa wakiwa wajinga, kosa ni la nani? Muumbaji, siyo? Kwa hivyo yeye ndiye atakuwa na ujinga kwa kushindwa kutumia uwezo wake kuumba watu werevu. Simple logic.



Kinyume cha ujinga ni uerevu, sasa niambie nani anazaliwa akiwa muerevu?? na kipimo cha uerevu ni kipi ili tukimuona muerevu tumtambue??. Simple questions.
 
Inakuwa ngumu mtu kukuelewa mkuu ikiwa hujavunja hoja za misingi ya hiyo dhana,ukiishia tu kupinga yale yenye kuelezwa kuhusu Mungu bila kupinga msingi wenyewe wa hiyo dhana inakuwa sawa na bure.
Msingi wa dhana ya Mungu ni ukomo wetu wa kufikiri. Basi!. Na huu ni utumwa mkubwa sana.

Ndugu, jiulize, kwa nini Mungu wa upendo aliacha kivuko kinachobeba watu mia kubeba watu mia mbili? Alishindwa kuzuia hilo pamoja na uwezo na upendo wake wote?

Ndugu, jioe muda wa kujitumia. Tafakari sana. Wanaopaswa kuwa na upendo ni wanadamu ambazo wangeamua kusimamia taratibu, ajali hiyo isingetokea.

Kusema Mungu kapanga ni ukomo mbaya sana wa kifikra. Ni umbumbumbu unaotufanya kuwa utumwani milele. Hicho kivuko kilizidisha watu na waliosimamia kujaa hivyo ni watu, siyo Hugo Mungu. Ila, kwa mini Mungu wa upendo muweza vyote hakuzuia? Au ndicho alichoweza? Kuangamiza watu 200 kwa pamoja? Hakuna na huruma na familia, watoto, wahitaji wanaoachwa?

Jibu rahisi in kuwa kila jambo lipo ndani ya uwezo wetu wanadamu. Tunayasabisha sisi, ila kwa kuwa yupo Mungu, yakitokea ni mipango yake. Aibu, utumwa, ujinga, umbumbumbu!
 
Thibitisha Mungu yupo.

Kukuelezea elimu ya Marekani ni sawa na kumfundisha claculus sisimizi.
nimethinkiiiiii nimegundua kuwakweli Mungu yupo na ili ujue Mungu yupo jiulize wewe umekujaje duniani amekuleta nani? ukishajua haya ndo uendelee kufikiria mengineyo
 
Unarudia rudia tu maswali yale yale, tushajadili haya.

Awali kabisa, uthibitisho ni lazima uweze kupimika. Usipoweza kupimika hauwezi kuwa uthibitisho.

Pili, uthibitisho ni lazima uwe logically consistent. Sio uthibitisho hauna logical consistency. Sio nakuuliza kuthibitisha kwa njia inayoweza kuwa falsified, wewe unahubiri kwa ushairi vague ambao hausemi lolote linaloweza kuwa fasified.

Tatu, uthibitisho ni lazima usiwe self contradictory, usiwe na elements zinazojipinga zenyewe. Sio tunathibitisha wewe umeoa, unaniambia umeoa, halafu hapo hapo unniambia wewe ni bachelor huna mke.This is a special case of lacking logical consistency.

Nne, uthibitisho ni lazima uweze kutabiri vitu specific, kwamba vitatokea mbeleni, katika muda specificna realistic, kwa namna specific,vinayoweza kupimwa, katika maisha yetu haya na si habari za baada ya kufa ambako hatujui hata kama tutaweza kupima chochote.

Tano, uthibitisho ni lazima uwe na ushahidi usiopingika kimantiki katika fremu yenye kukubalika na pande zote. Sio unathibitisha mambo kwa mistari ya Quran, wakati Quran yenyewe kwangu ni kitabu chenye makosa mengi sana ya kujipinga chenyewe.

Hayo ni machache tu kwa sas.
Kaka mkubwa naelekea katika ile safari niliyokuwa naisubiri kwa hamu sana. Safari ya kuonyesha haki iko wapi na kina nani wenye haki.

Naanzia hapa :

Wewe unawezaje kuthibitisha kutokuwepo kwa Mola kutokana na vigezo vyako hivyo ? Hapa chini nakueletea uthibitisho wa haki na vigezo vya ithibati.

Vigezo au vijenzi vya ithibati.

1. Katika kuthibitisha jambo kwanza lazima ujue nini unachotakiwa kukithibitisha. Je jambo husika linaweza kuthibitishwa au kinyume chake ?

2. Lazima ujue ni wapi ithibati ilipo,yaani kwa lile ukusudialo kulithibitisha lazima ujue wapi utapata ithibati.

3. Lazima uwe na elimu ya kile unachotakiwa kukithibitisha.

4. Ni yapi maegemeo yako katika ithibati zako,je unatumia hoja za kihisia,hoja za kiakili au unatumia nukuu za ki ufunuo ?


Mizani au vipimo vya Ithibati

Nakuja..............!
 
Inakuwa ngumu mtu kukuelewa mkuu ikiwa hujavunja hoja za misingi ya hiyo dhana,ukiishia tu kupinga yale yenye kuelezwa kuhusu Mungu bila kupinga msingi wenyewe wa hiyo dhana inakuwa sawa na bure.
Hawa watu kutoijua misingi ndio huwa kuna waangusha sana,huishia kuyasema yale ambayo kiuhalisia hawawezi kuyathibitisha hata kwa dakika moja.

Mathalani huwa wanasema Uwepo wa Mola ni matokeo ya fikra za mwaadami,ukiwauliza kivipi ? Bro hapo nanga itapaa hupati jibu.
 
Kinyume cha ujinga ni uerevu, sasa niambie nani anazaliwa akiwa muerevu?? na kipimo cha uerevu ni kipi ili tukimuona muerevu tumtambue??. Simple questions.
Mada ya uerevu na ujinga ni mpya kwenye Uzi huu. Kufahamu mtu mjinga na mwerevu ni yupo, sidhani kama kunawea kuthibitisha Mungu yupo au hayupo. Maneno haya yametumika kama maneno mengine yanavyotumika, tukiamini yanafahamika vizuri. Vinginevyo, tusishangse mtu mwingine naye akaja kuuliza maana ya "sidhani", " vizuri" ama "kutokushangaa".
 
Hawa watu kutoijua misingi ndio huwa kuna waangusha sana,huishia kuyasema yale ambayo kiuhalisia hawawezi kuyathibitisha hata kwa dakika moja.

Mathalani huwa wanasema Uwepo wa Mola ni matokeo ya fikra za mwaadami,ukiwauliza kivipi ? Bro hapo nanga itapaa hupati jibu.
Ndugu, kabla ya uwepo wako, kulikuwa na Mungu? Ulimwengu je?, wanadamu walikuwepo? Unayo kumbukumbu yoyote ya uwepo wa Mungu kabla ya kuwepo kwako?
 
Unarudia rudia tu maswali yale yale, tushajadili haya.

Awali kabisa, uthibitisho ni lazima uweze kupimika. Usipoweza kupimika hauwezi kuwa uthibitisho.

Pili, uthibitisho ni lazima uwe logically consistent. Sio uthibitisho hauna logical consistency. Sio nakuuliza kuthibitisha kwa njia inayoweza kuwa falsified, wewe unahubiri kwa ushairi vague ambao hausemi lolote linaloweza kuwa fasified.

Tatu, uthibitisho ni lazima usiwe self contradictory, usiwe na elements zinazojipinga zenyewe. Sio tunathibitisha wewe umeoa, unaniambia umeoa, halafu hapo hapo unniambia wewe ni bachelor huna mke.This is a special case of lacking logical consistency.

Nne, uthibitisho ni lazima uweze kutabiri vitu specific, kwamba vitatokea mbeleni, katika muda specificna realistic, kwa namna specific,vinayoweza kupimwa, katika maisha yetu haya na si habari za baada ya kufa ambako hatujui hata kama tutaweza kupima chochote.

Tano, uthibitisho ni lazima uwe na ushahidi usiopingika kimantiki katika fremu yenye kukubalika na pande zote. Sio unathibitisha mambo kwa mistari ya Quran, wakati Quran yenyewe kwangu ni kitabu chenye makosa mengi sana ya kujipinga chenyewe.

Hayo ni machache tu kwa sas.
Hapa naendelea pale nilipoishia.

Vipimo vya ushahidi / uthibitisho /Ithibati.

1. Nafsi

Hiki ni kipimo madhubuti na chenye nguvu sana katika katika kuhakiki ukweli wa mambo jinsi ulivyo. Naposema nafsi ni kile kinachotafutiwa uthibitisho kinasemaje au kinajielezeaje. Hapa nakupa mfano. Kwa mfano wewe kiranga unajijua zaidi kuliko mtu mwingine yeyote. Kwahiyo nikitaka kumjua Kiranga kwa uhalisia wake,lazima nikuulize wewe mwenyewe kisha wafate wale wanao kujua.

Mathalani sisi tunao muamini Mola muumba tunapata ushahidi wa uwepo wake kwanza kutokana na yeye alovyojipambanua kwetu sisi kupitia wateule wake ambao ni mitume na manabii.

Sasa swali linakuja kwako wewe,unathibitishaje kutokuwepo kwake kinyume kwake kwa kutumia hisia na akili tu ? Akili ambayo ni dhaifu na hisia ambazo si kamilifu ?

2. Maumbile

Naendelea......
 
Yani kila kitu kinaanza kuwepo baada ya wewe kuwepo. Usipokuwepo, hakuna kilichopo, hakikuwahi kuwepo na hakitakaa kiwepo, had I utakapokuwepo.
 
Hii ina maana gani, hata Mungu yupo kwa kuwa watu wapo. Tafsiri ya mbele kidogo ni kuwa, Mungu ni matokeo ya uwepo wetu. Huu ndio uthibitisho nilio nao.

Thibitisha kuwa mtu ambaye hajazaliwa anatambua uwepo wa Mungu na kila kitu kilichopo. Ukishindwa ujue unakubaliana nami kubwa, ili kutambua Mungu yupo, lazima uwepo. Na usipokuwepo milele, tafsiri yake ni kwa, hakuna kitu Mungu kiliwahi kuwepo kabla ya wewe kuwepo.
 
Ndugu, kabla ya uwepo wako, kulikuwa na Mungu? Ulimwengu je?, wanadamu walikuwepo? Unayo kumbukumbu yoyote ya uwepo wa Mungu kabla ya kuwepo kwako?
Umeuliza swali rahisi nina kujibu swali lako hili. Na mimi nikikuuliza swali bro naomba unijibu.

Mim sio binadamu wa kwanza kuumbwa,kwa maana kabla yangu mimi kulikuwepo wazazi wangu.

Mola alikuwepo sababu alikuwa ameshawaumba walionitangulia.

Sina kumbukimbuku sababu sababu sikuwepo na hili halibadilishi ukweli.

Kwani Mola wenyewe anasema "Ilipita kitambo dahari binadamu hakuwa ni kiumbe chenye kujulikana...."

Akasem tena Mola muumba katika sura hiyo hiyo :

"Kisha tukampa uongofu wa njia,akipenda ashukuru na akipenda akufuru"

Hapa nakupa hoja ya kiakili tena ya kihesabu.

Chukulia una seti A yenye elementi a,b,c,d,e. Tunasema seti A imeundwa na elementi hizo nilizo zitaja. Katika seti hii kuna vitu viwili,kuna tokeo la kupatikana seti A iliyoundwa na vijenzi tajwa na kuna kile chanzo kilichopelekea kuwepo kwa seti A.

Kawa maana kupatikana kwa seti A lazima kuwepo na yule mfanyaji ambaye nyuma yake hakuna mwingine.

Hapa kimahesabu tuna sema kuna Universal set,seti ambayo imejumuisha seti nyingine kama vile B,C,D,E,F....

Hii universal set ndio ambaye kutoka kwake amepatikana A,B,C,D,E,F na wengine. Sasa kwenu nyie mnaojiita wafikiriaji wakuu fikra zenu zimeishia hapo.

Mchakato wa ujenzi wa seti A ni ule ule mchakato wa ujenzi wa Universal se (U). Kama una amini A,B,C,D,.... ni matokeo ya U. Basi lazima kutakuwa na yule aliyekuwepo kabla ya U.

Ukikataa kuwepo yule aliye nyuma ya U. Basi inabidi ukubuli kuna seti zaidi ya U na itaendelea.

Na je zaidi ya U kuna nini ?

Mathalani,ikitoka 1 inafata 2 kisha inafata 3. Je nyuma ya moja nini ? Bila shaka ni 0 na hi sifuri ni kitu gani ?

Mfano mwingine ni huu :

1+1+1= 3 je inawezekana 1+1+1=0 ?

Ukinipa jibu nakuja kumalizia kazia yangu.
 
Hii ina maana gani, hata Mungu yupo kwa kuwa watu wapo. Tafsiri ya mbele kidogo ni kuwa, Mungu ni matokeo ya uwepo wetu. Huu ndio uthibitisho nilio nao.

Thibitisha kuwa mtu ambaye hajazaliwa anatambua uwepo wa Mungu na kila kitu kilichopo. Ukishindwa ujue unakubaliana nami kubwa, ili kutambua Mungu yupo, lazima uwepo. Na usipokuwepo milele, tafsiri yake ni kwa, hakuna kitu Mungu kiliwahi kuwepo kabla ya wewe kuwepo.
Bro hujatoa bado uthibitisho.

Ukisema hivyo swali linakuja,mimi nimetoka wapi ikiwa hapo kabla sikuwepo ?

Nasubiri jibu.
 
Msingi wa dhana ya Mungu ni ukomo wetu wa kufikiri. Basi!. Na huu ni utumwa mkubwa sana.

Ndugu, jiulize, kwa nini Mungu wa upendo aliacha kivuko kinachobeba watu mia kubeba watu mia mbili? Alishindwa kuzuia hilo pamoja na uwezo na upendo wake wote?

Ndugu, jioe muda wa kujitumia. Tafakari sana. Wanaopaswa kuwa na upendo ni wanadamu ambazo wangeamua kusimamia taratibu, ajali hiyo isingetokea.

Kusema Mungu kapanga ni ukomo mbaya sana wa kifikra. Ni umbumbumbu unaotufanya kuwa utumwani milele. Hicho kivuko kilizidisha watu na waliosimamia kujaa hivyo ni watu, siyo Hugo Mungu. Ila, kwa mini Mungu wa upendo muweza vyote hakuzuia? Au ndicho alichoweza? Kuangamiza watu 200 kwa pamoja? Hakuna na huruma na familia, watoto, wahitaji wanaoachwa?

Jibu rahisi in kuwa kila jambo lipo ndani ya uwezo wetu wanadamu. Tunayasabisha sisi, ila kwa kuwa yupo Mungu, yakitokea ni mipango yake. Aibu, utumwa, ujinga, umbumbumbu!
Unasema msingi wa dhana ya Mungu ni ukomo wetu wa kufikiri.

Una maanisha nini unaposema ukomo wetu wa kufikiri?
 
Unasema msingi wa dhana ya Mungu ni ukomo wetu wa kufikiri.

Una maanisha nini unaposema ukomo wetu wa kufikiri?
Kaka usitegemee kupata jibi hapo. Wao wanapenda kuuliza wao maswali na kujibiwa ila ukiwauliza wao hawajibu.

Hapa kuna maswali nasubiri majibu sijapewa mpala muda huu.

Kwa ufupi wakanungu wana ugonjwa wa akili.
 
Yani kila kitu kinaanza kuwepo baada ya wewe kuwepo. Usipokuwepo, hakuna kilichopo, hakikuwahi kuwepo na hakitakaa kiwepo, had I utakapokuwepo.
Nikikwambia kuwa unaongea kitu ambacho haujawahi kuexperience utakataa? Unaweza kuelezea experience yako ya kutokuwepo ilikuwaje?
 
Nikikwambia kuwa unaongea kitu ambacho haujawahi kuexperience utakataa? Unaweza kuelezea experience yako ya kutokuwepo ilikuwaje?
Hapana. Ninaongea kitu ambacho Nina uzoefu nacho. Sikukaa kuwepo hadi pale nilipokuwepo. Je, una uzoefu wowote wa kutambua uwepo wa Mungu kabla ya wewe kuwepo? Fikiria mwenye uzoefu wa kutokuwepo milele, kwake Mungu yupo? Anamtukuza vipi?
 
Hapana. Ninaongea kitu ambacho Nina uzoefu nacho. Sikukaa kuwepo hadi pale nilipokuwepo. Je, una uzoefu wowote wa kutambua uwepo wa Mungu kabla ya wewe kuwepo? Fikiria mwenye uzoefu wa kutokuwepo milele, kwake Mungu yupo? Anamtukuza vipi?
Ndiyo maana nikauliza unaweza kuelezea uzoefu wako wa kutokuwepo ulikuaje?
 
Back
Top Bottom