Makonda apiga simu Clouds Tv 360 kukemea ushoga

Makonda apiga simu Clouds Tv 360 kukemea ushoga

Binafsi sikuona Shida, nilipata muda nzuri wa kujifunza kuwa hawa jamaa wanahitaji msaada. kuna muda alisema kabisa hawezi kuacha ushoga ila akipata daktari(psychologist) may be anaweza akachukia ushoga na kuacha.

Kuna muda pia alisema Kama angekuwa na mtoto has a wa kiume basi angemlea, kumfuatilia na kuwa naye makini Sana NADHANI HAPO KATUFUNDISHA KITU NA KUASHIRIA KUWA KWAKE HAIKUWA HIVYO.

WATAnzania tusipende kulalamika na kukimbia matatizo, hiyo yamii ya watu IPO na wasagaji na machangu na mateja pia. Hizo jamii zina Shida kubwaaa zinapooneshwa hadharani na ishara kuwa tuwe na strategies za kuwasaidia na kuondoa tatizo na sio kuwalaani bila kuchukua hatua
Lazima utakuwa mfuasi wa hayo mambo.Badala ya kuangalia bunge unaangalia mashoga.
 
Binafsi sikuona Shida, nilipata muda nzuri wa kujifunza kuwa hawa jamaa wanahitaji msaada. kuna muda alisema kabisa hawezi kuacha ushoga ila akipata daktari(psychologist) may be anaweza akachukia ushoga na kuacha.

Kuna muda pia alisema Kama angekuwa na mtoto has a wa kiume basi angemlea, kumfuatilia na kuwa naye makini Sana NADHANI HAPO KATUFUNDISHA KITU NA KUASHIRIA KUWA KWAKE HAIKUWA HIVYO.

WATAnzania tusipende kulalamika na kukimbia matatizo, hiyo yamii ya watu IPO na wasagaji na machangu na mateja pia. Hizo jamii zina Shida kubwaaa zinapooneshwa hadharani na ishara kuwa tuwe na strategies za kuwasaidia na kuondoa tatizo na sio kuwalaani bila kuchukua hatua
Ki ukweli yule kijana (shoga) anahitaji msaada wa phycologist aweze kuondokana na tatizo lile. Pale UDSM kuna wataalamu wa phycologist watusaidie kwa kijana huyu. Tumieni taaluma zenu tuwakombea hawa vijana.
Tusiwe watu wa kulalamika watanzania wenzangu.
 
Lazima utakuwa mfuasi wa hayo mambo.Badala ya kuangalia bunge unaangalia mashoga.
Siwezi kuwa mfuasi wa hizo kharam za sodoma, ila sasa Kama tatizo lishaingia ndani ya nyumba yako unafanya nn? Bila Shaka lazima ulitafutie tiba hata Kama linaaibisha

Anayekemea ushoga na kuulani bila kuchukua hata Hana tofauti na anayemfungia mlemavu ndani ya nyumba ili asionekane njee

Bunge nalifuatilia redioni live maana kwa TV wenye nchi washali-ban
 
Pia wazo zuri sana kuwaombea watoto lakini sio wakina mama bali pia wakina baba wanajukumu hilo swala la malezi ni vyema likahusisha wazazi wote.

Jambo la msingi hapa niumakini katika malezi ya watoto.
Haswaa hilo ndilo ninaloliamini pia
 
Hao Clouds wanapews mshiko mkubwa kutangaza huo ushoga. Ndivyo vipindi anavyopenda kuangalia magufuli
 
Jamani jamani huyo shoga alihojiwa nar anatamani kubeba mimba azae loooh
 
Kama hukuona hicho kipindi kaa kimya.
Watu humu mnakuwa wajinga wakujadili vitu bila ya kufatilia
Kama ulikiona kipindi lazima utamsapot makonda kushauri viongezwe hivyo vipindi ili vielimishe athari za ushoga
Kwangu Mimi nikipindi bora kwani kimeonesha chanzo cha watoto na wajukuu zetu kuwa mashoga
Mbona hawaweki mahiójiano na waliofungwa kwa uhaini. Au hata waliokuwepo wakati Mzee karume anauwawa?
Tusiletewe unafiki hapa. Ukizidi kuwaonyesha watu hawa, tena na tena unawafanya watoto waone ni watu wa kawaida. Hayo mafunzo au mafundisho unayoyasema kwa watu wazima sawa, lakini kwa watoto wataona ndo mtindo. Kwamba siku wakifukuzwa nyumbani kumbe wanaweza kuishi kwa mtindo huo.

Tusijidai kuelewa zaidi ya wengine. Clouds ni waandishi wasiojifahamu kwa kiasi kikubwa sana na na bahati mbaya sana wakishangiliwa wanadhani wako sahihi.
 
Ndo shida ya kuwa na watu wasio na maadili kuendesha sehemu ya gurudumu la jamii. Wanatakiwa wafungiwe lkn sidhani kama chama kitadhubutu.
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam amepiga simu moja kwa moja (live) kwenye kipindi cha Clouds 360 kinachomhoji mtayarishaji wa kipindi kilichorushwa jana cha Take one Zamaradi. Kipindi hicho kilimuonyesha maisha ya shoga almaarufu KAOGE.
Mahojiano yaliyokemewa na Makonda haya


Kaongea nini baada ya kupiga hiyo simu?
 
Simu inatosha wapi....? Tcra wapo wapi....??? Station ifungiwe sio kipindi tu
 
Kile hakikuwa kipindi cha kujenga na kuelimisha bali kilitumika kumtangaza yule filauni,kipindi kingekuwa na maudhui mazuri endapo yule bwana angekuwa ameamua kuachana na hayo mambo sasa anawapa darasa wengine waache,na siyo kuelezea sijui anataka afanyiwe upandikizaji wa mimba,MAONI naona hiki kituo kingejipambanua kama kimeanza kupigania haki za mapenzi ya jinsia moja,Serikali kemeeni hili na muwachukulie hatua.

Dunia ya sasa hivi utandawazi umeenea hivyo kitendo cha kurusha kipindi kama kile clip zinaenea mitaani na zitawaathiri watu wengi zaidi tofauti na mawazo ya muandaaji na mtangazaji
 
Back
Top Bottom