Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu Watanzania,
Mheshimiwa Paul Makonda Mwamba na Jabali la siasa na kijana jasiri kusini mwa jangwa la sahara hapo jana aliitetemesha Mbeya kwelikweli,alilisimamisha jiji na kuteka mioyo ya wananchi , shughuli zote zilisimama na kubaki na shughuli moja tu ya kutega masikio kwa Mwamba Mwenyewe Makonda.
Akiwa katika viwanja vya Rwanda nzovwe maarufu kama viwanja vya CCM aliwalipua Wana Mbeya kwa vicheko visivyokatika pale alipowaambia kuwa CHADEMA wameacha na kukimbia kabisa kufanya mikutano ya hadhara na sasa wameanza kulilia vyombo vya habari ili wafanyiwe mahojiano.akasema walitaka mikutano ya hadhara Mheshimiwa Rais akawaruhusu lakini Mwamba mwenyewe Makonda alipoingia mitaani CHADEMA wote wakatimua mbio kali sana kwenda kujificha, ambapo hadi sasa hawaonekani mitaani na sasa wanaanza kuvamia ofisi za watu wakililia kutaka kufanya mahojiano.
Ndugu zangu hata mimi niliona CHADEMA na Lissu wake ni kama watu ambao hawapo sawa kichwani na ni watu wasio jitambua kabisa.hivi unaanzia wapi kulazimisha kuhojiwa kwenye chombo binafsi? Kama mhusika kakupigia simu ukiwa kwako kwamba usije kwenye mahojiano mpaka wakati mwingine,sasa kwanini ulazimishe kwenda kuvamia ofisi za watu na kusimamisha shughuli za watu eti unataka uelezwe sababu za kufutwa kwa mahojiano yako? Kwani uliopitwa mara ya kwanza uliambiwa kwa nini unataka kufanyiwa mahojiano? Kwani ni lazima wewe kuhojiwa?
Je kile chombo cha habari ni mali ya CHADEMA? Kama siyo mali ya CHADEMA unataka kulazimisha ili iweje? Kwanini msifungue Tv yenu ndio muwe mnakwenda wakati wote kuhojiwa au muwe mnajirusha hata mnapokura chakula na familia zenu? Miaka yote mmepokea mamilioni kwa mamilioni ya pesa za Ruzuku kwanini mmeshindwa kuanzisha Tv au redio yenu? Hapa majuzi tu si mmetoka kutafuna zaidi ya Billion tatu kasoro kidogo tu pesa za Ruzuku? Je fedha hizo zilikuwa hazitoshi kuanzisha Tv mnazolilia Lilia kama watoto walio kliniki kutaka kuhojiwa?
Hivi Lissu na CHADEMA yake watakuwa lini na kukomaa kiakili? Halafu wafuasi wao walivyo mazuzu eti wanahangaika mitandaoni kulalamika kwanini Lissu hajahojiwa? Sasa kuhojiwa ni lazima? Je hakupewa taarifa kuwa kipindi kimefutwa? Hii yote ni kuonyesha CHADEMA hasa viongozi wake hawana kazi za aina yoyote ile wanazofanya za kuwapatia kipato zaidi ya kutegemea kupiga porojo ,Makele na uzushi midomoni pao,kwa sababu mtu mwenye kazi zake tulitegemea alipopewa taarifa tena kabla ya siku husika kufika basi angeendelea na kazi zake na shughuli zake kama kawaida na kufurahi kuwa kazi zake hazitasimama kwa siku hiyo.
Sasa kwa kuwa CHADEMA ni madalali wa kisiasa na wamefanya siasa kama sehemu ya kuneemesha matumbo yao na kuponya njaa zao ndio maana mtu anachukua gari na kufunga safari kwenda kuvamia ofisi za watu na kuanza kulilia eti anataka aambiwe sababu za kufutwa mahojiano .hivi huu siyo ujinga kweli? Siyo uwendawazimu huu? Siyo ugonjwa huu kweli? Siyo kujikatia tamaa huku kweli? Siyo kukosa kazi huku? Siyo kwamba hawa jamaa wamechanganyikiwa?
Mimi naona kuna namna mambo hayapo sawa katika vichwa vya CHADEMA,Lissu ameathirika kisaikolojia na anahitaji ushauri kumsaidia kupona .maana hili siyo jambo la kawaida hata kidogo.yaani chombo cha habari siyo chako,siyo mali yao,huna hisa wala wewe siyo mwana hisa,huchangia chochote katika chombo hicho,huwasaidia kulipa hata bili ya maji tu halafu unatoka huko mbio mbio eti nataka nielezwe kwanini hamtaki kunipa nafasi ya kufanya mahojiano na ninyi? Sasa ni lazima kufanya hivyo? Vipi kama wangeamua wakae kimya tu kama mabubu na kuweka headphone ili wasikilizage hata nyimbo za injili? Je angebaki anaongea pekee yake kama kichaa au mwendawazimu? Vipi kama maiki yake wangeiondoa sauti? Angesikika kwa nani zaidi ya kuonekana kama picha tu?
Kwanini CHADEMA wanakuwa na utoto kiasi hiki? Kwanini hawakui kiakili ? Kwanini hawakomai kifikira? Kwanini wanafanya mambo kama watoto wadogo? Kwanini wasifungue Tv zao? Ruzuku na michango kibao inakwenda wapi? Kama wanapenda sana sura zao kuonekana kwenye Tv kwanini wasifungue zaooooo? Ndio maana watanzania wanaendelea kuwapuuza sanaa CHADEMA. ila ukweli ni kuwa nje ya siasa viongozi wa CHADEMA hawana kazi zozote zile za kiuchumi wanazozifanya huku mitaani,hakuna kitu wanachozalisha kuchangia katika uchumi wetu wala kutoa hata ajira kwa vijana kumi tu.ndio maana kwa kukosa kwao kazi wanaanza kufunga safari kwenda kung'ang'ania kwenye ofisi za watu.
CHADEMA acheni kupenda vya dezo na mteremko ,kama mnapenda sana kuonekana katika Tv basi fungueni zenu na siyo kutafuna pesa zote halafu muanze kuleta usumbufu kwa watu waliofanya uwekezaji kwenye Tv na radio zao.acheni kuharibu biashara za watu,acheni kuvuruga shughuli za watu,acheni vurugu na utoto wenu.fanyeni vitu kama watu wazima na siyo kama watoto wadogo waliozibuka akili.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Mheshimiwa Paul Makonda Mwamba na Jabali la siasa na kijana jasiri kusini mwa jangwa la sahara hapo jana aliitetemesha Mbeya kwelikweli,alilisimamisha jiji na kuteka mioyo ya wananchi , shughuli zote zilisimama na kubaki na shughuli moja tu ya kutega masikio kwa Mwamba Mwenyewe Makonda.
Akiwa katika viwanja vya Rwanda nzovwe maarufu kama viwanja vya CCM aliwalipua Wana Mbeya kwa vicheko visivyokatika pale alipowaambia kuwa CHADEMA wameacha na kukimbia kabisa kufanya mikutano ya hadhara na sasa wameanza kulilia vyombo vya habari ili wafanyiwe mahojiano.akasema walitaka mikutano ya hadhara Mheshimiwa Rais akawaruhusu lakini Mwamba mwenyewe Makonda alipoingia mitaani CHADEMA wote wakatimua mbio kali sana kwenda kujificha, ambapo hadi sasa hawaonekani mitaani na sasa wanaanza kuvamia ofisi za watu wakililia kutaka kufanya mahojiano.
Ndugu zangu hata mimi niliona CHADEMA na Lissu wake ni kama watu ambao hawapo sawa kichwani na ni watu wasio jitambua kabisa.hivi unaanzia wapi kulazimisha kuhojiwa kwenye chombo binafsi? Kama mhusika kakupigia simu ukiwa kwako kwamba usije kwenye mahojiano mpaka wakati mwingine,sasa kwanini ulazimishe kwenda kuvamia ofisi za watu na kusimamisha shughuli za watu eti unataka uelezwe sababu za kufutwa kwa mahojiano yako? Kwani uliopitwa mara ya kwanza uliambiwa kwa nini unataka kufanyiwa mahojiano? Kwani ni lazima wewe kuhojiwa?
Je kile chombo cha habari ni mali ya CHADEMA? Kama siyo mali ya CHADEMA unataka kulazimisha ili iweje? Kwanini msifungue Tv yenu ndio muwe mnakwenda wakati wote kuhojiwa au muwe mnajirusha hata mnapokura chakula na familia zenu? Miaka yote mmepokea mamilioni kwa mamilioni ya pesa za Ruzuku kwanini mmeshindwa kuanzisha Tv au redio yenu? Hapa majuzi tu si mmetoka kutafuna zaidi ya Billion tatu kasoro kidogo tu pesa za Ruzuku? Je fedha hizo zilikuwa hazitoshi kuanzisha Tv mnazolilia Lilia kama watoto walio kliniki kutaka kuhojiwa?
Hivi Lissu na CHADEMA yake watakuwa lini na kukomaa kiakili? Halafu wafuasi wao walivyo mazuzu eti wanahangaika mitandaoni kulalamika kwanini Lissu hajahojiwa? Sasa kuhojiwa ni lazima? Je hakupewa taarifa kuwa kipindi kimefutwa? Hii yote ni kuonyesha CHADEMA hasa viongozi wake hawana kazi za aina yoyote ile wanazofanya za kuwapatia kipato zaidi ya kutegemea kupiga porojo ,Makele na uzushi midomoni pao,kwa sababu mtu mwenye kazi zake tulitegemea alipopewa taarifa tena kabla ya siku husika kufika basi angeendelea na kazi zake na shughuli zake kama kawaida na kufurahi kuwa kazi zake hazitasimama kwa siku hiyo.
Sasa kwa kuwa CHADEMA ni madalali wa kisiasa na wamefanya siasa kama sehemu ya kuneemesha matumbo yao na kuponya njaa zao ndio maana mtu anachukua gari na kufunga safari kwenda kuvamia ofisi za watu na kuanza kulilia eti anataka aambiwe sababu za kufutwa mahojiano .hivi huu siyo ujinga kweli? Siyo uwendawazimu huu? Siyo ugonjwa huu kweli? Siyo kujikatia tamaa huku kweli? Siyo kukosa kazi huku? Siyo kwamba hawa jamaa wamechanganyikiwa?
Mimi naona kuna namna mambo hayapo sawa katika vichwa vya CHADEMA,Lissu ameathirika kisaikolojia na anahitaji ushauri kumsaidia kupona .maana hili siyo jambo la kawaida hata kidogo.yaani chombo cha habari siyo chako,siyo mali yao,huna hisa wala wewe siyo mwana hisa,huchangia chochote katika chombo hicho,huwasaidia kulipa hata bili ya maji tu halafu unatoka huko mbio mbio eti nataka nielezwe kwanini hamtaki kunipa nafasi ya kufanya mahojiano na ninyi? Sasa ni lazima kufanya hivyo? Vipi kama wangeamua wakae kimya tu kama mabubu na kuweka headphone ili wasikilizage hata nyimbo za injili? Je angebaki anaongea pekee yake kama kichaa au mwendawazimu? Vipi kama maiki yake wangeiondoa sauti? Angesikika kwa nani zaidi ya kuonekana kama picha tu?
Kwanini CHADEMA wanakuwa na utoto kiasi hiki? Kwanini hawakui kiakili ? Kwanini hawakomai kifikira? Kwanini wanafanya mambo kama watoto wadogo? Kwanini wasifungue Tv zao? Ruzuku na michango kibao inakwenda wapi? Kama wanapenda sana sura zao kuonekana kwenye Tv kwanini wasifungue zaooooo? Ndio maana watanzania wanaendelea kuwapuuza sanaa CHADEMA. ila ukweli ni kuwa nje ya siasa viongozi wa CHADEMA hawana kazi zozote zile za kiuchumi wanazozifanya huku mitaani,hakuna kitu wanachozalisha kuchangia katika uchumi wetu wala kutoa hata ajira kwa vijana kumi tu.ndio maana kwa kukosa kwao kazi wanaanza kufunga safari kwenda kung'ang'ania kwenye ofisi za watu.
CHADEMA acheni kupenda vya dezo na mteremko ,kama mnapenda sana kuonekana katika Tv basi fungueni zenu na siyo kutafuna pesa zote halafu muanze kuleta usumbufu kwa watu waliofanya uwekezaji kwenye Tv na radio zao.acheni kuharibu biashara za watu,acheni kuvuruga shughuli za watu,acheni vurugu na utoto wenu.fanyeni vitu kama watu wazima na siyo kama watoto wadogo waliozibuka akili.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.