Makapuku Forum

Makapuku Forum

1969 - Abdallah Kassim Hanga anapelekwa Zanzibar kujibu mashtaka yake ua Uhani dhidi ya Serikali ya Rais Abeid Amani Karume.

Hanga alikuwa ni mmoja kati ya Wanamapinduzi wa Zanzibar walioshiriki kikamikifu katika kuondoa utawala dhalimu wa Mwarabu visiwani humo.

Baada ya mapinduzi akawa Waziri Mkuu wa kwanza wa Zanzibar kwa miezi mitatu kabla ya kukosana na Karume na kuhamishiwa Bara ambapo baadae akenda kuwa Balozi.

Baada ya tuhuma za Uhaini, kujaribu kupindua serikali ya Karume akarudishwa nyumbani na kuwekwa kizuizini Tz Bara.

Karume akamuimba Nyerere apelekewe Hanga ili akajibu tuhuma zake.

Nyerere akakubali kumpeleka Kassim Hanga Zanziba, ambapo hakuwahi kupandishwa mahakamani waka hakuwahi kuonekana tena mpaka leo. Aliuwawa na kuzikwa kusikojulikana.
096c1f9fac33f207ae883058bc093a35.jpg
d0004d518b2096ca8ad4bb0715eab1be.jpg
ed3ff91d23c099896ffea84740df8229.jpg
Nyerere na Karume walikuwa na mapungufu yao
.......
 
9bb4134b836540294f8bb4c5f81ed8e5.jpg
384579732c3884e53230c6e7c8540e04.jpg
f13055077d378594802955ebd1c55551.jpg
a522f78565a478d3639ccf5eb55c1d9f.jpg

Picha zinaonyesha kimada wake(Marilyn Monroe) alihudhuria na hata kuhutubia
.......
Ndio maana mke wa JFK akaona kuliko kwenda kuadhirika na kuumia moyo akawachukua watoto na kwenda kuangalia mbio za farasi.

Jambo pekee la kumtenganisha JFK na Ms Monroe ilikuwa ni kifo tu.
Na hapo ndipo dikteta John Edgar Hoover alipotekeleza majukumu yake.
 
1979 - Andrea Pirlo anazaliwa.

Kiungo wa zamani wa Italy na vilabu vya Juventus, Ac Milan, Inter Milan na L.A Galaxy.

Maarufu kama " The architecture " ni moja kati ya viungo bora kuwahi kutokea katika mchezo wa kabumbu.

Ameshinda karibu kila taji katika soka.
ff2f1d4799f62527ae4a9fc6c10fcf2e.jpg
f35f80f97b73626a19d8c71ed2a61d65.jpg
6e1d19bee672f6e74d26cb60dafcc278.jpg

Ni mmoja kati ya wachezaji bora zaidi niliobahatika kuwaona wakicheza soka katikati ya Simba
......
 
91161e5250adfa4dd77b84a08e37f457.jpg
d72dccf615a4503f94f9bcc40b86dce7.jpg
f5f31ac62f94e9a7a8ddaa4509030839.jpg
a5bc4032f2621be0aa72cec3ca458e2b.jpg

Enzi za babu hilo la FBI watu wengi walikuwa wananyamazishwa kimyakimya
.......
Malcom X enzi za uhai wake aliwahi kukanyaga Zanzibar na kufanya mazungumzo na msomi mahiri kuwahi kutokea Zanzibar na mwanamapinduzi Abdulrahman Mohamed Babu kuhusu masuala ya Ujamaa na haki za watu weusi.

Bahati mbaya Babu hakuwahi kupatana na Karume na akahamishiwa Bara kikazi baada ya Muungano. Ni mmoja kati ya waasisi wa Muungano.

Bitoz tunaomba picha za Malcom X na Babu.
 
NUKUU YA LEO


“The pain of life overrides the joy to the point that joy does not exist.”

Maumivu ya maisha yametowesha furaha kiasi kwamba hakuna furaha tena


Haya ni maandishi wala sio maneno, ni maandishi yaliyoachwa kwenye ujumbe kabla ya kifo ( suicidal note) na mwanajeshi/ maandishi na mpiga picha maarufu Bw. Kevin Carter.

Kevin Carter alizaliwa nchini Afrika ya kusini tar. 13/9/1960 na kufariki tar 27/07/1994 kwa kujifungia kwenye gari yake na kuvuta hewa ya carbonmonoxide.

Kevin carter alikuwa na mwanajeshi wa jeshi la wakaburu miaka ya 1980, alifanya kazi kamandi ya infantry kabla ya kukimbilia kamandi ya anga baada ya kutoweza kuvumilia mauaji ya watu weusi.

Kevin aliumizwa sana na ubaguzi wa watu weusi, kevin aliumia sana namna watu weusi wivyouliwa, wanawake kibakwa n.k

Baadaye kevin aliondoka jeshini nila ruhusa (Awol) absence without leave.

Kevin alipata umaarufu mwaka 1993 baada ya picha yake aliyopiga nchini sudan , kevin alimpiga picha mtoto mwenye njaa na mdhoofu akiwa anafuatiliwa na kunguru.

Kevin alitumia zaidi ya dakika 10 kupiga picha hiyo...ambayo ilikuja kuwa maarufu duniani kote na kupelekea kupata tuzo ya Pultizer Prize ya upigajipicha.

Kevin aliumizwa na maisha waliyoishi watu weusi..

6c1367d89d8db1f0cb74185eb0d69b67.jpg
picha aliyopiga Kevin Carter nchini sudani


Back to Jf and kapukuz...

Ktk maisha ya kila siku kuna watu wanaishi maisha ya tabu kwa kukosa chakula, kwa kudhulimiwa na kifanyiwa fitina katika maisha..

Kama utashindwa kuwasaidia kwa nafasi yako, basi jitahidi usiwe sehemu ya watesaji.
f195c07455d789dfc4951f9c7ef5fa1c.jpg
kevin Carter mwenyewe.

Jtatu nitaendeleza Suicide note ya Kevin Carter.
Ahsante sana boss

Natumai ulifurahia usiku wa jana

Siku njema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom