NUKUU YA LEO
“The pain of life overrides the joy to the point that joy does not exist.”
Maumivu ya maisha yametowesha furaha kiasi kwamba hakuna furaha tena
Haya ni maandishi wala sio maneno, ni maandishi yaliyoachwa kwenye ujumbe kabla ya kifo ( suicidal note) na mwanajeshi/ maandishi na mpiga picha maarufu Bw. Kevin Carter.
Kevin Carter alizaliwa nchini Afrika ya kusini tar. 13/9/1960 na kufariki tar 27/07/1994 kwa kujifungia kwenye gari yake na kuvuta hewa ya carbonmonoxide.
Kevin carter alikuwa na mwanajeshi wa jeshi la wakaburu miaka ya 1980, alifanya kazi kamandi ya infantry kabla ya kukimbilia kamandi ya anga baada ya kutoweza kuvumilia mauaji ya watu weusi.
Kevin aliumizwa sana na ubaguzi wa watu weusi, kevin aliumia sana namna watu weusi wivyouliwa, wanawake kibakwa n.k
Baadaye kevin aliondoka jeshini nila ruhusa (Awol) absence without leave.
Kevin alipata umaarufu mwaka 1993 baada ya picha yake aliyopiga nchini sudan , kevin alimpiga picha mtoto mwenye njaa na mdhoofu akiwa anafuatiliwa na kunguru.
Kevin alitumia zaidi ya dakika 10 kupiga picha hiyo...ambayo ilikuja kuwa maarufu duniani kote na kupelekea kupata tuzo ya Pultizer Prize ya upigajipicha.
Kevin aliumizwa na maisha waliyoishi watu weusi..
picha aliyopiga Kevin Carter nchini sudani
Back to Jf and kapukuz...
Ktk maisha ya kila siku kuna watu wanaishi maisha ya tabu kwa kukosa chakula, kwa kudhulimiwa na kifanyiwa fitina katika maisha..
Kama utashindwa kuwasaidia kwa nafasi yako, basi
jitahidi usiwe sehemu ya watesaji.
kevin Carter mwenyewe.
Jtatu nitaendeleza Suicide note ya Kevin Carter.