
ZABURI 143
8.Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi ,Kwa maana nimekutumainia Wewe Unijulishe njia nitakayoiendea ,Kwa maana nakuinulia nafsi yangu.
TUOMBE
Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu Bwana Mungu wa majeshi asante kwa siku mpya ya leo na kutuamsha salama,wapo watu wengi walitamani kuiona siku ya leo walikua na mipango mingi na maono mbalimbali lakini hawajaweza ,wengine umewaita,wengine ni mahututi vitandani,wengine wanachangamoto mbalimbali Baba sisi ni nani hatuna cha kukupa zaidi ya kusema Asante
Tunaomba utusamehe makosa yote tunayotenda kwa mawazo maneno na matendo uturehemu twa kusihi.
Waponye wagonjwa,fariji wafiwa,watie nguvu yatima,wajane ,wahitaji wakutumainie wewe tu.
Tunakabidhi mapito yetu yote,nyoosha njia zetu Baba tunajikabidhi kwako tujulishe njia sahihi ya kuiendea siku yaleo
Tunaomba maafa ya mvua yaishe ponya majeraha yote ya mafuriko,maporomoko,mvua isiyokoma ,neema yako itawale.
Bariki wasafiri majini ,nchi kavu na angani wafike salama
Tunaomba Amani na Upendo vitawale
Tunaomba bariki kazi za mikono yetu
Tunaomba Roho Mtakatifu atuongoze ,tusipungukiwe.
Katika jina la Yesu tunaomba na kushukuru Amen
Raha ya milele uwape marehemu wote,na mwanga wa milele uwaangazie wapumzike kwa Amani Amen
SIKU NJEMA WAPENDWA