Makapuku Forum

Makapuku Forum

Bunge la Cameroon limeanza kujadili muswada wa marekebisho ya katiba unaolenga kurudisha nafasi ya Makamu wa Rais baada ya nafasi hiyo kufutwa mwaka 1972.

Nafasi hiyo itamwezesha Makamu wa Rais kushika madaraka endapo Rais Paul Biya (93), ambaye ameiongoza nchi hiyo tangu mwaka 1982, hatokuwepo au kushindwa kutekeleza majukumu yake.
swahilitimes-20260403-0001.jpg
 
Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Comoro, ambaye sasa amehamishiwa Ufaransa, Saidi Yakub anatarajia kuvishwa nishani na Rais wa Comoro, Azali Assoumani kutokana na mchango mkubwa aliotoa tangu apewe wadhifa huo Aprili 2024.

Nishani hiyo ya kitaifa hutolewa kwa mtu mwenye mchango wa kipekee kwa taifa hilo, na mtu wa mwisho kupewa ni Rais Mstaafu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Akinwumi Adesina, mara baada ya kumaliza kipindi chake mwaka 2025.
swahilitimes-20260403-0002.jpg
 
Wakati bei ya gesi ya kupikia (LPG) ikiendelea kupanda katika soko la dunia, kampuni ya Taifa Gas imesema haitapandisha bei ya nishati hiyo kwa watumiaji wa majumbani, ikilenga kulinda wateja dhidi ya makali ya ongezeko hilo.

Hatua hiyo inakuja kufuatia ongezeko la takribani asilimia 43 ya bei ya gesi ya kupikia katika wiki za hivi karibuni, hali iliyosababisha kupanda kwa gharama za ununuzi na usambazaji katika minyororo ya ugavi duniani.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari leo Ijumaa Aprili 3, 2026, Meneja Mkuu wa Taifa Gas, Devis Deogratius amesema kampuni hiyo imeamua kubeba athari za ongezeko hilo ili kuhakikisha wateja wanaendelea kupata huduma kwa bei nafuu na uhakika.

“Katika mazingira haya ya sasa, tunayo dhamira ya dhati ya kuwasaidia wateja wetu kwa kubeba athari za ongezeko la gharama ya nishati ya kupikia kwa kutokuongeza bei huku tukihakikisha upatikanaji endelevu wa gesi safi na ya kuaminika,” amesema.

Ameeleza kuwa gesi ya kupikia ni nishati muhimu kwa kaya nyingi na biashara ndogo ndogo nchini, hivyo uamuzi huo unalenga pia kuchochea shughuli za kiuchumi kwa kupunguza mzigo wa gharama kwa watumiaji.
mwananchi_official-20260403-0001.jpg
 
Mwonekano wa hali ilivyo katika Stendi ya Kabwe jijini Mbeya baada ya daladala kurejesha huduma za usafiri kutokana na mgomo uliotokea kwa muda jana Aprili 2, 2026 kushinikiza kupandisha nauli baada ya mafuta kupanda bei.

Mkoani Mbeya bei ya petroli inauzwa Sh3,952 na diseli inapatikana kwa Sh3,938.
mwananchi_official-20260403-0002.jpg
mwananchi_official-20260403-0003.jpg
 
Kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL) imewakutanisha wadau kutoka tasnia mbalimbali kama vile ulimbwende, mavazi, ubunifu, ujasiriamali na taaluma katika kikao maalum cha kimkakati, ikiwa ni hatua ya kujenga hamasa na kutoa ufahamu wa kutosha kuelekea uzinduzi wake rasmi, unaolenga kusherehekea wanawake jasiri, wenye kujiamini na kusherehekea mafanikio yao.

Kupitia tukio hili liliratibiwa kwa umakini, SBL inaendelea kuibua na kusimulia hadithi zinazoakisi wanawake wa kisasa wa Kitanzania, wenye ndoto kubwa, wanaojinasibu kwa uhuru, na wanaojiamini katika kila hatua ya maisha yao.


mwananchi_official-20260403-0004.jpg
mwananchi_official-20260403-0005.jpg
mwananchi_official-20260403-0006.jpg
 
Machi 30, 2026, dunia iliadhimisha Siku ya Kimataifa ya Ugonjwa wa Akili ujulikanao kama Bipolar, siku inayolenga kuongeza uelewa kwa jamii, kupunguza unyanyapaa na ubaguzi pamoja na kuhimiza upatikanaji wa huduma za afya ya akili.

Siku hii huchaguliwa kwa heshima ya siku ya kuzaliwa ya msanii maarufu wa Uholanzi, Vincent van Gogh, ambaye alihusishwa na ugonjwa huo baada ya kifo chake.

Bipolar au Baipola kwa Kiswahili, ni hali ya afya ya akili inayosababisha mabadiliko makubwa ya hisia. Mabadiliko hayo hujumuisha vipindi vya furaha iliyopitiliza na huzuni kali, hali inayoweza kuathiri maisha ya mhusika kwa kiasi kikubwa.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), takribani watu milioni 40 duniani wanaishi na ugonjwa huu, huku tafiti zikionesha kuwa waathirika wanaweza kufariki mapema kwa wastani wa miaka 10 ikilinganishwa na watu wengine.

Wagonjwa wa Bipolar hukumbana na changamoto nyingi, hasa katika jamii zenye uelewa mdogo wa afya ya akili. Unyanyapaa, ubaguzi na kutengwa na familia au jamii ni baadhi ya matatizo yanayowakabili.

mwananchi_official-20260403-0007.jpg
 
Panya wanaimba, lakini kwa sauti za juu sana ambazo binadamu hatusikii bila vifaa maalum.

Panya hutumia sauti hizi kuwasiliana na wenzao, hasa wakati wa kuvutia majike au kuonyesha hisia.
Screenshot_20260403_115120_InstaPro%20.jpg
 
Ndio maana unashauriwa, siku zote unapoenda kuonana na mtu kwa mara ya kwanza ni muhimu kuwa katika muonekano mzuri na wenye staha.

Kisaikolojia mtu atakutafsiri kwa namna yake mwenyewe ndani ya sekunde 7 tu atazokuona kwa mara ya kwanza, na kama kakutafsiri kwa namna mbaya, itamchukua miezi mingi kuja kukubali kwamba alikosea.
fahamuzaidi-20260403-0001.jpg
 
Kuna sababu nyingi, ila mojawapo ni ndoa huleta mtu wa karibu wa kushirikiana furaha na changamoto na husaidia kupunguza msongo wa mawazo pamoja na magonjwa.
fahamuzaidi-20260403-0002.jpg
 
Kwa kiasi kidogo, bia husaidia kuongeza ubunifu na kutatua matatizo, lakini inategemea na aina ya kazi na mtu mwenyewe pia.

Kivipi inaweza kusaidia?

- Hupunguza vizuizi vya kiakili: Pombe kidogo hupunguza aibu na hofu, hivyo mtu anaweza kufikiri kwa uhuru zaidi.

- Huongeza uwezo wa kufikiria nje ya box zaidi: Unaweza kupata mawazo ya kipekee au suluhisho lisilotarajiwa ukinywa pombe kidogo, hufaa zaidi kwa kazi za ubunifu.

- Hupunguza msongo wa mawazo: Akili iliyotulia huweza kufikiri kwa urahisi na kwa ubunifu.

NB; Kunywa mara kwa mara kunaathiri afya ya ubongo na uwezo wa kutatua matatizo.
Screenshot_20260403_115818_InstaPro%20.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom