shululu
JF-Expert Member
- Jan 26, 2015
- 28,137
- 109,911
Uko sahihi kabisa, fanya siku moja utumegee japo kwa uchache mambo ya DNAHili bado ni fumbo kubwa. Wanasema kuwa siku tukiweza kusoma kila code na kuelewa kila kitu kilichomo basi si ajabu tutaweza kufumbua mafumbo yote ya maisha yetu - tumetoka wapi? Kwa nini tuko hapa? Kwa nini tunazeeka? Kwa nini huwa tunaugua? Twaweza kuishi milele? The possibilities are endless! Wanasema siri zote - ikiwemo kama kuna ndugu zetu wengine huko katika sayari na malimwengu (universes) mengine pengine zimefichwa katika DNA zetu. Ndiyo maana Genetics bado ni mojawapo ya nyanja za sayansi zinazosisimua sana tangu mlango ufunguliwe na mtawa Gregory Mendel zaidi ya miaka 120 iliyopita.
